Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa ziara hiyo, Afisa TEHAMA Mwandamizi wa e-GA, Bw. Juvenali Tarimo, alisema mafunzo hayo yataimarisha utoaji wa huduma za Serikali kwa wananchi kupitia matumizi ya teknolojia za kidijitali na kuchochea maboresho ya huduma katika taasisi za umma.
Matumizi ya teknolojia zinazochipukia yana nafasi kubwa katika kuboresha utoaji wa huduma za Serikali kwa njia za kidijitali, kuongeza uwazi, ufanisi na usalama wa taarifa.