Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa viongozi wa nchi za Afrika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya miundombinu, akisisitiza kuwa maendeleo ya Bara hilo hayatapimwa kwa mipango na sera pekee, bali kwa matokeo yanayoonekana katika maisha ya wananchi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Afrika inapaswa kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya miundombinu na uwekezaji ili kufikia malengo ya maendeleo na kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja na matokeo yake.
Viongozi wa Afrika wamesema umefika wakati wa kuelekeza nguvu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kupitia uwekezaji katika miundombinu, nishati na matumizi ya rasilimali za ndani, badala ya kujikita zaidi katika kuandaa maono na mikakati.
