Katika tamasha la Kizimkazi, Mfuko umewajibika kwa jamii kupitia utoaji wa majiko janja (80L Electric Pressure Cooker) yanayotumia umeme kidogo sana wastani wa ‘units’ 2 kwa saa nzima, ni salama na yanajizima yakiivisha ambayo yametolewa kwa shule za sekondari sambamba na kushiriki, pamoja na wadau wengine wa maendeleo, katika Kongamano la Nishati Safi lililofanyika hapa Kizimkazi.
Utoaji wa majiko janja na ushiriki wa Mfuko kwenye Kongamano la Nishati safi ni hatua zinazoonesha dhamira ya NSSF ya kuunga mkono ajenda ya kitaifa ya Nishati Safi ya kupikia, inayolenga kuongeza matumizi ya nishati safi kwa ajili ya kuboresha afya, kulinda mazingira na kuchochea maendeleo endelevu.