Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, ana kesi ya kujibu katika shauri la uhaini linalomkabili. Akisoma uamuzi huo leo Ijumaa, Agosti 21,2026, Jaji Dunstan Ndunguru, anayeongoza Jopo la Majaji watatu linalosikiliza kesi hiyo, amesema Mahakama baada ya kupitia ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka imejiridhisha kuwa kuna ushahidi unaotosha kumtaka Lissu atoe utetezi wake.
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, leo Agosti 21, 2026 imemkuta na kesi ya kujibu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu katika kesi ya uhaini inayomkabili.