Simba imeonekana kuwa na shughuli nyingi katika dirisha hili ili kujenga kikosi kipana kinachoweza kushindania mataji ya Ligi Kuu Tanzania Bara, Kombe la Shirikisho (FA Cup), na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Dhamira yetu ni kuona Simba inakuwa na kikosi imara chenye uwezo wa kushindana na kutwaa mataji yote msimu ujao.