Mtaalam huyo anaonya kuwa mjadala haupaswi kujikita katika idadi ya ATM pekee bali gharama za huduma za kifedha zinazotozwa na benki wakati watu wakifanya miamala kwa njia ya kidijitali.
Kupungua kwa ATM pia kunaakisi mabadiliko ya tabia za Watanzania ambapo kwa miaka 10 iliyopita ATM na matawi ya benki zilikuwa kama njia kuu ya kufanya miamala.