Wachimbaji wadogo wa Mgodi wa Namungo wameiomba Serikali kupitia Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kuendelea kuwapatia mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi ili kuwawezesha kufanya shughuli za uchimbaji na uchakataji madini kwa kuzingatia viwango bora vya usalama.
“Binafsi nawashukuru OSHA kwa kuja kututembelea leo, kifupi tumejifunza mambo mengi sana kupitia wao hivyo tunaomba isiwe mwisho leo na tunaomba utaratibu huu uwe endelevu katika vipindi tofauti tofauti,” ameeleza Salum Mfaume.