Amesema elimu na mafunzo ya ufundi stadi ni nyenzo muhimu katika kujenga viwanda vya kisasa, uchumi wa kidijitali na uwezo wa Taifa kuzalisha bidhaa na huduma kwa kutumia maarifa, teknolojia na ubunifu wa ndani.
Amesema Serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za elimu na sekta ya viwanda kupitia Mpango wa Kitaifa wa Ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Sekta ya Viwanda katika Ukuzaji wa Ujuzi na Uwezeshaji wa Ajira, uliozinduliwa Februari 9, 2026, jijini Dar es Salaam.