Amesema kwa kuanzia, eneo hilo litatumika kuhudumia makontena ya mizigo inayoingia nchini (import containers), huku mpango wa kushughulikia mizigo ya nje (export containers) ukifuatia baada ya changamoto zilizopo kutatuliwa.
maboresho hayo yanalenga kuongeza uwezo wa bandari kuhudumia shehena kubwa zaidi, kupunguza msongamano wa meli na kuiwezesha Bandari ya Dar es Salaam kuwa miongoni mwa bandari zenye ushindani mkubwa zaidi katika ukanda wa Bahari ya Hindi.