Ameongeza kuwa pamoja na kuongeza uzalishaji, kuna haja ya kuwekeza zaidi katika utangazaji wa bidhaa, kuimarisha mifumo ya masoko na kuboresha mazingira ya biashara ili bidhaa za Kitanzania zipate nafasi kubwa katika masoko ya kikanda na kimataifa.
Amesema kuwa lengo la ukaguzi huo ni kuangalia namna bidhaa zilivyofungashwa na kuwashauri wajasiriamali kuhusu maboresho yanayoweza kufanyika ili bidhaa zao ziweze kupata soko ndani na nje ya nchi.