Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mhandisi Athumani Kilundumya, amewahamasisha wakulima, wafugaji na wavuvi kutumia fursa ya maonesho hayo kujifunza teknolojia za kisasa zitakazoongeza tija, uzalishaji na ushindani Katika kilimo cha kibiashara.
Amesema Nanenane imekuwa jukwaa muhimu la kuwaunganisha wakulima, wafugaji, wavuvi, taasisi za serikali na sekta binafsi kwa ajili ya kubadilishana ujuzi, kujifunza teknolojia mpya na kupata fursa za kibiashara.