Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila ameshiriki katika hafla ya kuadhimisha miaka 25 ya kampuni ya Azania Group tangu kuanzishwa kwake iliyofanyika Agosti mosi 2026 katika ukumbi wa mlimani city Jijini Dar es Salaam.
Kwa kipindi cha robo karne, Azania Group imejijengea rekodi ya mafanikio kupitia uwekezaji katika viwanda, uongezaji wa thamani ya malighafi za ndani, utoaji wa maelfu ya ajira na mchango mkubwa katika mapato ya Serikali kupitia kodi.