Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe.CPA Amos Gabriel Makalla, amefunga rasmi Maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na sherehe za Wakulima Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayojumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara kwenye viwanja vya Themi -Njiro mkoani Arusha leo Agosti 08,2026.
Jumla ya waoneshaji 466 walijitokeza kushiriki Maonesho ya 32 ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na Sherehe za Wakulima Nanenane Kanda ya Kaskazini mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara, kwenye viwnaja vya Themi Njiro Mkoa wa Arusha kuanzia tarehe 01 - 07, 08,2026.
