Maonesho ya 32 ya Kilimo na Mifugo na Sherehe za Wakulima Nanenane Kanda ya Kaskazini 2026, yatafunguliwa rasmi kesho rasmi tarehe 01 Agosti 2026, kwenye viwanja vya Themi Njiro Mkoani Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ametoa wito kwa Viongozi, watendaji na wananchi wa Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro kujitokeza kwa wingi kwenye maonesho ya 32 ya Kilimo na mifugo na sherehe za nanenane, Kanda ya Kaskazini, zinazotarajiwa kuanza Agosti Mosi, 2026 kwenye Viwanja vya Themi Njiro Jijini Arusha kuanzia Agosti Mosi hadi 09, 2026.