
Gundua
4614 habariHabari mpya, uchambuzi wa kina, na maarifa kutoka Nukta
Unaona habari zinazohusishwa na Habari Leo chini (pamoja na mengine ya Gundua).


DODOMA; Serikali imewapa siku saba wamiliki wa viwanda vya kuzalisha saruji nchini kuwasilisha mapendekezo ya namna ya kutatua changamoto ya bei ya saruji inayotajwa kuwa juu katika soko pamoja na upatikanaji wake. Hatua hiyo imefikiwa baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum, kukutan…

DODOMA; Wizara ya Afya imehimiza Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Ebola huku ikisisitiza kuwa bado Tanzania ni salama na wageni kutoka mataifa mengine waje bila hofu. Waziri wa Afya, Mohammed Mchengerwa alibainisha hayo jijini Dodoma alipotoa taarifa kwa kikosi kazi cha wanahabari kuhusu mwe…

MOROGORO: CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),kupitia Ndaki ya Tiba ya Wanyama na Sayansi za Afya kimeendelea kutoa watafiti bora na bobezi wanaofanya mambo makubwa katika kulisaidia taifa na nchi nyingine barani Afrika kwenye kudhibiti magonjwa ya wanyama na yale yatokayo kwa wanyama kwenda kwa binadamu. Rasi wa …

DAR ES SALAAM: MENEJA Mwekezaji wa Bohari ya Mafuta ya MOIL Energies Dk Sajad Habib Rai, amesema Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua hatua kuhakikisha mafuta yanaendelea kupatikana nchini huku ikidhibiti makali ya ongezeko la bei linalochochewa na mgogoro wa Mashariki ya Kati unaohusisha Iran, Israel na Marekani.…

UFARANSA: Rais wa Marekani na Rais wa Iran wameripotiwa kusaini makubaliano ya awali ya amani yanayolenga kumaliza vita, makubaliano yanayoanza mara moja. Makubaliano hayo yanajumuisha kufunguliwa tena kwa Mkondo wa Bahari wa Hormuz, mpango wa takribani Dola bilioni 300 kwa ajili ya ujenzi upya wa Iran na Marekani kuo…

WASHINGTON, Marekani — Israel imesema haitajadili sitisho la vita na kundi la Hezbollah wakati wa mazungumzo na maafisa wa Lebanon yatakayofanyika Marekani wiki ijayo. Balozi wa Israel, Yechiel Leiter, alisema mazungumzo hayo yatakuwa mwanzo wa majadiliano rasmi ya amani kati ya Israel na serikali ya Lebanon, licha ya…

KYIV, UKRAINE : MKUU wa Utawala wa Rais wa Ukraine, Andriy Yermak, amesema shambulio lililolenga jengo la serikali mjini Kyiv mwishoni mwa wiki lilikuwa la kwanza la aina hiyo tangu vita vya Ukraine kuanza zaidi ya miaka mitatu iliyopita. Yermak alibainisha kuwa kombora la aina ya Iskander ndilo lililotumika kushambul…

SERIKALI imetaja vipaumbele vitano katika mapendekezo ya mfumo na ukomo wa bajeti kwa mwaka 2026/2027. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar alisema hayo wakati wa kuwasilisha mapendekezo ya Mfumo na Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2026/2026 katika mkutano wa wabunge wote Dodoma jana. Balozi Omar alisema ser…

MWAKA 2022 kwenye fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Qatar, Morocco ilifika nusu fainali na kuwa taifa la kwanza kutoka Afrika kufanya hivyo. Imeweka rekodi inayoweza kudumu vizazi na vizazi na pengine, kama kuna taifa kutoka Afrika itakayoweza kuivunja rekodi hii, basi ni Morocco yenyewe. Rekodi ya kuwa taifa la…

MTWARA: KAMPUNI ya Ujenzi na Ukarabati wa Miundombinu ya Usafirishaji na Usambazaji wa Umeme (ETDCO) imekamilisha ujenzi wa laini maalum ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 33 kutoka Masasi hadi Newala, Mkoa wa Mtwara, ndani ya miezi saba badala ya miezi 12 iliyokuwa imeainishwa kwenye mkataba. Hatua hiyo imep…

MWANZA: MKOA wa Mwanza umeandika historia mpya baada ya kutwaa ubingwa wa jumla wa Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISETA) 2026, yaliyoshirikisha wanafunzi kutoka mikoa yote 26 ya Tanzania Bara pamoja na Zanzibar. Katika mashindano hayo yaliyohitimishwa leo mjini Iringa, Mwa…

DODOMA:WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof Kitila Mkumbo, ameweka wazi mambo sita ya msingi ambayo Taifa linapaswa kuyazingatia ili kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, akisisitiza matumizi ya mitaji na teknolojia, ushirikiano wa sekta ya umma na binafsi, pamoja na kujenga…

MTWARA: MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma Nchini (PPRA) Dennis Simba amesema lengo la mamlaka hiyo ni kuhakikisha wanasajili vikundi zaidi ya laki moja hadi kufikia Disemba 2026. Hayo yamejiri wakati Mwenge wa Uhuru mwaka 2026 ulipowasili mkoani humo Mei 3, 2026 ukitokea mkoani Lindi na kuanza …

IRINGA: KATIBU wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi amewataka Watanzania kutowasikiliza wanasiasa wanaotumia majukwaa ya siasa kubeza na kupunguza thamani ya maendeleo yaliyofanya ya serikali. Kihongosi amesema hayo Juni 20,2026 alipokuwa akizungumza na wananchi katik…

KIGOMA: MADIWANI katika halmashauri za wilaya, miji na majiji wametakiwa kutokuwa chanzo cha vurugu zinazoweza kuchangia kuzorotesha uhusiano baina ya watendaji na madiwani na kukwamisha shughuli za maendeleo nchini na ukusanyaji mapato. Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Sospeter Mtwale amesema hayo aki…

IRINGA: Mkoa wa Iringa umeingia katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025–2030 ukiwa na taswira ya mafanikio yanayoonekana kwa macho: mapato ya Serikali yameongezeka, fedha za maendeleo zimeongezeka, na miradi ya afya, elimu, maji na miundombinu inaendelea kubadili maisha ya wananchi. Taar…

MAREKANI: Serikali ya Tanzania imeeleza mafanikio makubwa iliyoyapata katika kuimarisha ustawi na ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu, huku ikisisitiza umuhimu wa kuongeza upatikanaji wa vifaa na teknolojia saidizi ili kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi. Akihitimisha ushiriki wa Ta…

DODOMA: MGANGA Mkuu wa Serikali, Dk Grace Magembe amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa (RMOs) na Waganga Wakuu wa Wilaya (DMOs) kuhakikisha wanaendeleza mafanikio yaliyopatikana kupitia Programu ya Kukuza Huduma za Uzazi wa Mpango (SuFP) hata baada ya kufungwa rasmi kwa mradi huo. Dk Magembe alitoa maelekezo hayo juzi Ji…

SIMIYU: Benki ya NMB kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, imeendelea kutekeleza mfumo mpya wa utolewaji mikopo ya halmashauri asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu katika halmashauri hiyo. Ikiwa ni awamu ya pili benki hiyo kuwezesha kutoa mikopo hiyo ndani ya Halm…

ENGLAND: Mabao mawili aliyofunga dhidi ya ‘Spurs’ yanamfanya mshambuliaji wa Arsenal, Viktor Gyokeres kuwa wenye mabao mengi kuliko mchezaji yoyote Ligi Kuu ya England kwa mwaka 2026 katika michuano yote. Gyokeres amefikisha mabao 8, akifuatiwa na Joao Pedro wa Chelsea, Anthony Gordon wa Newcastle wenye 7, Igor Thiago…

UFARANSA: Rais wa Marekani, Donald Trump ametishia kurejea katika mashambulizi na kuwaua maofisa wa Iran iwapo hawatafuata masharti ya makubaliano hayo ya kumaliza vita yaliyosainiwa jana katika mkutano wa G7 nchini Ufaransa. Makubaliano hayo ya vipengele 14 yanaongeza muda wa kusitishwa kwa mapigano uliotangazwa Apri…

GEITA; TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Geita imewafikisha mahakamani watumishi sita wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Geita kwa tuhuma za ubadhirifu wa Sh milioni 261.4 za mirathi. Watumishi hao wa mahakama na watumishi wanne wa idara zingine za serikali pamoja na wafanyabiashara wanne wal…

PWANI: Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amesema wakuu wa wilaya, wakurugenzi na watendaji mbalimbali wa serikali wanapaswa kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa wakati na kwa kuzingatia kanuni na taratibu ili kuondoa urasimu unaochelewesha huduma kwa wananchi na kukwamisha wawekezaji. Kunenge ametoa kauli …

JUMUIYA ya Kikristu Tanzania (CCT) imepongeza jitihada za Serikali kukuza ari ya mahusiano miongoni mwa jamii ya kitanzania hatua itakayosaidia kuleta utengamano na mshikamano wa kidugu. Hatua hiyo imekuja wakati Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu alipokutana na Viongozi wa CCT…

MGOMBEA urais Kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan leo anatarajiwa kuomba kura kwa wananchi kisiwani Pemba. Samia tayari ameacha ahadi nane katika Kisiwa cha Unguja. Akiwa Unguja amefanya mikutano miwili ukiwemo uliofanyika Uwanja wa Kajengwa, Jimbo la Makunduchi, Wilaya ya Kusini mkoani Kusini…

IRINGA: Ndoto za mamia ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika Manispaa ya Iringa za kujikwamua kiuchumi zimeendelea kupata uhai baada ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kukabidhi mikopo ya Sh milioni 402.26 kwa vikundi 28 vilivyokidhi vigezo, huku Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo, akitekeleza ahadi …

JANA Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza Mahakama ya Tanzania itekeleze mambo 12 kuchangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2050. Rais Samia aliyasema hayo kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria na uzinduzi wa …

Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) zimeagizwa kuwa na mkakati wa kuwawezesha wakulima kuanzia uzalishaji ukusanyaji hadi uuzaji ili kuleta tija na bei nzuri ya mazao. Vilevile Serikali imetoa rai kwa wakulima na wafanyabiashara kuwa waaminifu …

DAR ES SALAAM: MAADHIMISHO ya Siku ya Mazingira yaliyofanyika katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yamekuwa jukwaa muhimu la kuhamasisha wananchi, hususan vijana na wadau mbalimbali, kushiriki kikamilifu katika uhifadhi wa mazingira kupitia ubunifu, urejeleaji wa taka na matumizi …

AFRIKA imeendelea kusisitiza umuhimu wa kuunganisha nguvu za kiuchumi miongoni mwa nchi zake ili kuchochea maendeleo ya viwanda, kuongeza thamani ya rasilimali za ndani na kujenga ushindani wa pamoja katika soko la dunia.

KATIKA siku 100 za mwanzo za uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea na Halmashauri jirani ya Madaba wameanza kushuhudia kile kinachoweza kuitwa mwanzo wa mapinduzi ya kilimo Mkoani Ruvuma. Serikali imepeleka jumla ya matrekta 15 katika mkoa huo, matano yakielekezwa Halmashauri…

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala,Ridhiwani Kikwete amesema Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kina nafasi ya kipekee katika kujenga na kuendeleza uwezo wa kiutendaji wa watumishi wa umma ambao ndio watekelezaji wa majukumu ya serikali kila siku. Kikwete al…

KILIMANJARO: Jumuiya ya Wanawake katika Nyuklia Tanzania (WiNTz) imetembelea Hospitali ya KCMC na kufanya mazungumzo na wanawake wanaofanya kazi katika Kitengo cha Tiba ya Mionzi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Jumuiya hiyo kuwawezesha wanawake katika sekta ya sayansi na teknolojia ya nyuklia kupata fursa za masomo na m…

DAR ES SALAAM: WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeendelea kuimarisha usimamizi wa ubora wa miradi ya ujenzi wa miundombinu nchini kupitia maabara zake za kisasa zinazofanya uchunguzi na uhakiki wa vifaa vya ujenzi pamoja na kazi zinazotekelezwa, hatua inayolenga kuhakikisha miundombinu inakuwa imara,…

TABORA; Kamandawa Polisi Mkoa wa Tabora (RPC), Richard Abwao amefariki dunia leo Juni 20, 2026 akiwa kwenye matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amesema Kamanda Abwao alikuwa akipatiwa matibabu kwenye hospitali hiyo, lakini leo wamepokea taarifa hizo za kusikitisha.…

Katika kipindi cha miaka mitano, Serikali ilitenga zaidi ya Sh trilioni 228 kwenye bajeti zake huku Sh trilioni 76.3 zikielekezwa kwenye maendeleo. Je fedha hizo zimeleta matokeo gani katika maisha ya wananchi na uchumi wa Taifa? Ungana na SYLIVESTER DOMASA katika makala haya. Mwaka 2021, mkazi wa Sumbawanga aliyekuwa…

TANGA: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkoa wa Tanga, imekuja na mkakati wa kuhifadhi mazingira kwa kuzindua kampeni ya upandaji wa miti 1,000 katika shule mbalimbali za msingi na sekondari jijini hapa. Zoezi hilo, lililolenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira dhidi ya athari za mabadiliko y…

KATAVI: Zaidi ya wananchi 850 waliokuwa wakisumbuliwa na maradhi mbalimbali wamepatiwa huduma za matibabu na uchunguzi wa afya bila malipo kupitia kambi maalumu ya afya iliyoendeshwa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Empower Society Build the Nation (ESBN) mkoani Katavi. Kambi hiyo ya siku saba imehitimishwa jana baad…
KIGOMA: Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Kigoma imetoa rai kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa miundombinu ya barabara kushiriki kikamilifu katika kulinda na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuendelea kuwa salama kwa watumiaji. Rai hiyo imetolewa na Me…

BODI ya Usimamizi wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza rasmi utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba, yenye lengo la kuimarisha usimamizi wa mfumo huo na kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinapatiwa ufumbuzi bila kurejea kwenye biashara holela ya mazao. Akitoa taarifa baada…

Unguja. Kampuni ya Floton Africa imetoa msaada wa Sh30 milioni kwa ajili ya kusaidia uanzishwaji wa Kituo Maalumu cha Upandikizaji wa uloto na Matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya uchangishaji fedha inayolenga kupanua upatikanaji wa huduma za matibabu bingwa nchin…

DAR ES SALAAM: Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za magonjwa yasiyoambukiza makali kwa kusogeza huduma hizo karibu na wananchi, hususan katika hospitali za wilaya na vituo vya afya vilivyochaguliwa nchini. Hatua hiyo imeelezwa kuwa imewezesha wagonjwa wengi kupata huduma za uchunguzi, matibabu na uf…

WAZIRI MKUU, Dk Mwigulu Nchemba, amemwagiza mkandarasi anayejenga uwanja wa Mashindano ya Mataifa ya Afrika(AFCON)2027 ahakikishe mradi huo unakamilika kwa wakati. Ujenzi wa uwanja huo unaojengwa katika kata ya Olomoti, jijini Arusha ni sehemu ya maandalizi ya Mashindano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, yakayofanyik…

DODOMA: MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka walipakodi na wananchi wote kujitokeza kwa wingi kushiriki katika matembezi na Mbio za Shukrani kwa Mlipakodi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Tuzo kwa Mlipakodi Bora na maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa mamlaka hiyo. Kwa mujibu wa TRA, tukio hilo linatara…

WADAU wa siasa na wananchi wamewatwika mzigo wa majukumu viongozi wapya walioteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, wakiwataka watekeleze majukumu yao kwa weledi, uadilifu na kuweka mbele maslahi ya taifa badala ya binafsi.

MWANZA; Fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB 2026/27 ni kati ya Simba na Azam FC, baada ya Azam FC kuifunga Yanga mabao 3-2 katika mchezo wa nusu fainali uliomalizika muda mfupi uliopita Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza. Ilikuwa mechi yenye kila aina msisimko ambapo hadi dakika 90 zinamalizika miamba hiyo ilikuwa imefu…

DODOMA: Serikali imesema haijauza wala kukabidhi rasilimali za misitu au maliasili za Tanzania kwa mataifa ya nje kupitia makubaliano ya biashara ya kaboni. Akizungumza na waandishi wa habari Juni 26, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, am…

MOROGORO: WANANCHI wa Kata ya Kinole, Tarafa ya Mkuyuni, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro wameipongeza Serikali kwa ujenzi wa Kituo cha Afya Kinole kitakachotoa huduma bora za afya. Wametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti baada ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2026, Wazo Mwang’onda kuweka Jiwe la Msing…

MTWARA: HALMASHAURI ya Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara imepata hati safi ya ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Yamejiri hayo wakati wa kikao maalumu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo ya Wilaya ya Tandhahimba kuhusu kujadili hoja za hesabu z…

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Halotel imesema hadi kufikia Septemba mwaka huu imefanikiwa kufikia wateja milioni 16.5 kupitia huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo. Akizungumza leo Oktoba 16,2025 katika maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo nchini Tanzania, Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara H…

ISLAMABAD, Pakistan — Iran imesema haitashiriki mazungumzo na Marekani bila kusitishwa kwa mapigano nchini Lebanon, ikisisitiza kuwa hali ya vita huko ni sehemu ya makubaliano ya sitisho la muda yaliyotangazwa hivi karibuni. Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, alisema Tehran haitakubali kuingia katika maz…

DAR ES SALAAM: SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) wamezindua Nyumba Janja yenye mfumo wa kisasa wa utakaosaidia kuongeza uslaama wa nyumba kwa kupunguza hatari za majanga kama moto na ajali nyingine zinazosababishwa na hitilafu za umeme. Akizungumza katika maonesho ya 50 ya biashara ya kimataifa ya Dar es salaam (sab…

WABUNGE wamepongeza Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kuendelea kupanua wigo wa huduma za hifadhi ya jamii kupitia Skimu ya Hifadhi kwa Wananchi Waliojiajiri, wakisema mpango huo unatoa fursa kwa mamilioni ya Watanzania kunufaika na huduma za hifadhi ya jamii. Aidha, wamepongeza uwekezaji uliofanywa na Mfu…
MOROGORO: WANAFUNZI wakike wa shule za msingi na sekondari mkoani Morogoro wameshauriwa kujiepusha na matumizi yasiyo sahihi ya simu kwa vile zimebainika ni vichocheo vya wao kujingiza kwenye uhusiano wa kimapenzi wakiwa kwenye umri mdogo, kufanyiwa ukatili wa kigono na wengi wao kupata mimba. Mwenyekiti wa Kampeni ya…

DAR ES SALAAM; Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, amelitaja Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwa ni nguzo kuu ya kulinda afya za walaji na kuchochea ustawi wa viwanda nchini. Amebainisha hayo leo jijini Dar es Salaam katika hafla maalumu ya maadhimisho ya Miaka 50 ya TBS pamoja na utoaji wa tuzo kwa …

DAR ES SALAAM; RAIS wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na uhamisho wa viongozi. Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bakari Machumu, ikinukuu taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka, imesema, Rais Samia amemteua Dk Eveline Munisi kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri …

NAIBU Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wazazi na walezi kuimarisha malezi ya watoto na kushiriki kikamilifu kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyoathiri wanawake na watoto.

TANGA: Waziri Mkuu Dk Mwigulu Nchemba amefichua namna baadhi ya watendaji wa serikali wanavyotumia ujanja kuhalalisha upotevu wa fedha katika miradi. Dk Mwigulu alieleza hayo jana baada ya kukagua na kufanya uzinduzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilindi ukiwa ni mwendelezo wa ziara yake iliyoanza juzi mkoani Tanga. Alise…

TARIME: KIASI cha Sh bilioni 9.4 zimeelekezwa kuboresha shule, makazi ya walimu na kuwawezesha watoto kupata mazingira bora ya kujifunzia Katika vilima vya Tarime ambako dhahabu imekuwa uti wa mgongo wa uchumi wa eneo hilo, hazina nyingine yenye thamani kubwa zaidi inaendelea kung’ara. Hazina hiyo si dhahabu inayochim…

RAIS wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Francisco Chapo, amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Julai 2 hadi 4, 2026.

DAR ES SALAAM; Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limetangaza fursa 12 zitakazotokana na Tanzania kuwa mwenyeji mwenza wa Mashindano ya Mataifa ya Afrika AFCON 202, ambazo zitafungua zaidi milango ya maendeleo ya uchumi, ajira, biashara, utalii na uwekezaji nchini. Akizungumza kuhusu fursa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Mawa…

DAR ES SALAAM: Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Mwanga, Mchome Lemburus, amewataka Watanzania kuendelea kulinda amani ya nchi. Aidha amesisitiza zaidi watu kujiepusha na maandamano yasiyo na tija kwa taifa ambayo yanaweza kuchochea vurugu na kusababisha uharibifu. Akizungum…

Kampuni ya Vodacom imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama kinara wa mageuzi ya kidijitali nchini baada ya kutembelewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji, Daniel Chapo, katika banda la kampuni hiyo wakati wa ufunguzi wa Maonesho ya 50 ya Kimataif…

Ni alasiri ya Jumamosi katika moja ya maeneo yanayokua kwa kasi pembezoni mwa Jiji la Dodoma. Chini ya kivuli cha mti mkubwa wa mwembe, wanaume wawili wasimama. Mmoja wao ana bahasha ya kaki iliyovimba fedha, na chupa ya maji na mwingine akiwa na karatasi moja iliyokunjwa mara mbili na kijiti mdomoni na fimbo mkononi …

DAR ES SALAAM: Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetangaza nafuu kwa waajiri wenye malimbikizo ya michango kwa kuwapatia fursa ya msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango, huku ukiwataka kuchangamkia fursa hiyo ili kupunguza mzigo wa madeni, kuimarisha uzingatiaji wa sheria na kulinda haki za w…

VIONGOZI wa dini nchini wametakiwa kuendelea kuimarisha uhusiano kati ya Serikali na wananchi kwa kuhamasisha umuhimu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa ili kuzuia vitendo vya vurugu vinavyoweza kukwamisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

MOROGORO: WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amemuagiza mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa barabara ya Bigwa–Kisaki (km 78) kuhakikisha anafanya matengenezo ya mara kwa mara katika maeneo yanayotumiwa na wananchi wakati ujenzi ukiendelea, ili kuondoa adha ya usafiri na kupunguza gharama za usafirishaji. Ulega alitoa ag…

DAR ES SALAAM: Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba, amesema Serikali itachukua hatua za kuimarisha taaluma ya uchukuzi nchini, ikiwemo kuharakisha mchakato wa kuanzisha Bodi ya Usajili wa Wataalamu wa Uchukuzi, ili kuongeza ubora wa huduma na ufanisi wa sekta hiyo. Akizungumza wakati wa kufungua kongamano la wataalamu wa …

DAR ES SALAAM: Waziri wa Ulinzi na JKT, Dk Rhimo Nyansaho amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kupitia Shirika lake la Uzalishaji Mali (SUMAJKT) kwa kuendelea kutoa ajira kwa vijana hapa nchini. Dk Nyansaho ameyasema hayo Julai 06, 2026 alipotembelea banda la JKT kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (Sa…

DAR ES SALAAM: Ujumbe wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) ukiongozwa na Thabo Letjama umekutana na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ikiongozwa na Kamishna Mkuu, Yusuph Juma Mwenda jijini Dar es Salaam kuhusu masuala mbalimbali ya kikodi. Katika mazungumzo hayo kiongozi wa ujumbe wa I…

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi ameonya watu wanaotumika kuichafua nchi. Katambi amesema hayo kwenye mkutano wa hadhara aliouandaa kushukuru wananchi kumpa ridhaa ya kuwa mbunge wa Shinyanga Mjini.

DODOMA: BODI ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) imeanza mazungumzo na wazalishaji wa parachichi katika wilaya za Mufindi na Njombe kwa lengo la kuanzisha mfumo wa ubunifu utakaoruhusu shamba kutumika kama ghala la bidhaa hai ili kuongeza ufanisi wa biashara ya zao hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa WRRB, Asangye Ban…

BALOZI wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, amesema lugha ya Kiswahili inaendelea kukua duniani, ikiwa sasa inazungumzwa na zaidi ya watu milioni 200 katika nchi 14 na kutumika rasmi katika jumuiya mbalimbali za kikanda na kimataifa.

TEHRAN — Kiongozi Mkuu mpya wa Iran, Mojtaba Khamenei, anaendelea kupata nafuu baada ya kujeruhiwa vibaya usoni na miguuni, lakini bado anashiriki kikamilifu katika maamuzi makubwa ya kitaifa, vyanzo vimeeleza. Kwa mujibu wa taarifa hizo, Khamenei, mwenye umri wa miaka 56, hajaonekana hadharani tangu mashambulizi ya a…

MAKAMU wa Rais Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Peter Nalitolela, mazungumzo yaliyofanyika leo Februari 13, 2026, Dodoma. Katika Mazungumzo hayo, Makamu wa Rais amewahimiza watendaji DSE kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa wabunifu…

DAR ES SALAAM: Kampuni ya Tanzania Breweries PLC (TBL) imetangaza kuongezeka kwa mapato yake kwa asilimia 13 mwaka 2025 huku faida ya uendeshaji ikiongezeka kwa asilimia 35. Kampuni ilieleza kuwa matokeo hayo yalitokana na kuongezeka kwa mahitaji ya bidhaa zake, usimamizi wa gharama na maboresho katika mfumo wa usamba…

DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imejadili rasimu ya mpango mkakati mpya wa mamlaka wa miaka mitano unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050. Haya yalijiri wakati Menejimenti ya TMDA ilipokutana mkoani Morogoro Februari 2 hadi 3, 2026. Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dk Adam Fimbo, aliwaeleza wajumbe…

MKURUGENZI wa Sayansi wa Taasisi ya Afya Ifakara (IHI), Dk Ally Olotu, amesema taasisi hiyo imeendelea kushiriki katika tafiti na ubunifu mbalimbali unaolenga kufikia lengo la kutokomeza malaria nchini Tanzania kupitia uzalishaji wa ushahidi wa kisayansi na maendeleo ya teknolojia za afya.

CHAMA cha ACT Wazalendo kimesisitiza umuhimu wa kulinda na kuendeleza amani ya Tanzania kwa kutumia mazungumzo na maridhiano, kikieleza kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuwa chanzo cha migogoro bali fursa ya kutafuta mwafaka kwa maslahi ya taifa. Katibu wa Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma wa ACT Wazalendo Taifa, S…

SONGEA: Wadau wa mradi wa Dumisha Amani unaotekelezwa na VETA na wamepanga kuanzisha vituo vya vijana (Youth Centres) katika vyuo vya VETA mkoani Mtwara, Lindi, Kigoma na Wilaya ya Songea ili kuwasaidia vijana wenye ujuzi kujiajiri au kuajiriwa. Mradi huo unafadhiliwa na mashirika ya kimataifa ya UNPDF, UNDP-Tanzania,…

DODOMA: JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limesema litaendelea kuwa shamba darasa la kilimo, mifugo na uvuvi hata baada ya kufungwa kwa Maonesho ya Nanenane 2026, kwa lengo la kuwajengea wananchi uwezo wa kuongeza tija katika uzalishaji. Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajab Mabele alisema hayo alipotembelea banda la jeshi hilo…

ARUSHA; SERIKALI imeanza rasmi kutoa mikopo kupitia Programu ya Sh bilioni 200 chini ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, huku Mkoa wa Arusha ukiwa wa kwanza kunufaika kwa kupokea Sh milioni 730 ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango. Mpango wa awamu ya kwanza unalenga kuwawezesha vijana kujiajiri na…

MJIOLOJIA kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Njombe, Abbas Mruma, amesema Tanzania inaendelea kujijengea nafasi muhimu duniani kutokana na kuwa na hifadhi kubwa ya madini ya kimkakati, yakiwemo graphite, lithium na rare earth elements, yanayotumika katika teknolojia za kisasa na nishati safi.

DODOMA; Mkurugenzi wa Wasafi Media, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, ameipongeza Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kwa utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, huku akiahidi kuwa tayari kufuata matakwa yote ya kisheria yanayohusu sekta ya habari na watumishi wake. Akizun…

DAR ES SALAAM: KATIKA jitihada za kuzuia uharibifu wa barabara na kuhakikisha zinapitika wakati wote, hususan kipindi cha mvua, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeanzisha mpango wa Vikundi vya Jamii (Community Based Routine Maintenance) unaolenga kutunza na kuboresha zaidi ya kilomita 15,000 za barab…

RAIS Samia Suluhu Hassan amewahimiza Watanzania kuendelea kuliombea Taifa ili amani, upendo, ustahimilivu na mshikamano viendelee kudumu nchini.

DAR ES SALAAM: Wadau wa maendeleo ya ujuzi nchini wameeleza kuwa kuimarishwa kwa mfumo wa uanagenzi (apprenticeship) unaozingatia mwongozo wa kimataifa wa mafunzo ya uanagenzi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) kutasaidia kuongeza ajira kwa vijana na kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji halisi ya soko la aj…

DAR ES SALAAM: TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imechukua hatua kubwa ya kuimarisha elimu ya msingi kwa kuboresha mitaala na kuwajengea uwezo wa kutumia mifumo ya kidijiti kupitia ushirikiano na Kampuni Sahara Consult. Hatua hiyo ilifikiwa jana Dar es salaam pande hizo mbili ziliposaini mkataba wa makubaliano (MoU)wa k…

DAR ES SALAAM: Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA), Mhandisi Charles Sangweni, akishiriki katika Kongamano la Siku ya Nishati (Energy Day) linaloendelea katika Ukumbi wa Mwandoro, Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Sabasaba, jijini Dar es Salaam. Mhandisi Sangweni ameeleza kuhusu naf…

MTWARA: BAADHI ya Wakulima wa zao la Korosho katika kata ya Naliendele Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara wameishukuru serikali kwa kuendelea kuwaletea pembejeo za korosho bure ili kuwapunguzia gharama za uzalishaji. Hayo yamejiri wakati wa zoezi la ugawaji wa pembejeo hizo za korosho lilipofanyika kwa wakulim…

DAR ES SALAAM: SERIKALI imeitaka Tume ya Ushindani (FCC) kuimarisha na kupanua matumizi ya teknolojia za kisasa katika uchunguzi, ufutiliaji wa udhibiti wa bidhaa bandia katika masoko ya kidijitali. Pia FCC imetakiwa kuongeza kasi ya uratibu na ushirikiano wa karibu na taasisi zingine za udhibiti, ikiwemo vyombo ya do…

DAR ES SALAAM: MASHINDANO ya Kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF 2026) awamu ya nane yanatarajiwa kuanza Julai 6, mwaka huu. Mechi ya ufunguzi iitachezwa uwanja wa Azam complex,Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Michuano hiyo, Brigedia Jenerali Saidi Hamisi Saidi ameeleza hayo kwenye viwanja vya Gofu vya L…

DAR ES SALAAM: Matumizi ya dawa za antibiotiki kiholela yamepungua kwa 80%, hivyo kupelekea pia kupunguza vifo kwa 14% vitokanavyo na usugu wa vimelea dhidi ya dawa kwa binadamu. Aidha, upande wa usugu wa vimelea dhidi ya dawa kwa wanyama kumekuwa na juhudi kuhakikisha wafugaji wanahamasishwa kufuga kisasa kwa kuzinga…

DAR ES SALAAM: MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema msimu wa 11 wa mashindano ya waongoza watalii ya Safari Field Challenge utakuwa wa kipekee, ukitoa nafasi kwa washiriki kujifunza kwa vitendo utalii wa wanyamapori, historia na urithi wa eneo hilo. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Kamishna …

IRINGA: Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Jackson Kiswaga ameendelea kuunga mkono maendeleo ya wananchi baada ya kukabidhi mifuko 120 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Kituo cha Afya katika Kata ya Masaka jimboni humo. Hatua hiyo imekuja baada ya hivikaribuni kukabidhi msaada wa mifuko 200 ya simenti katika Shule ya…

SERIKALI juzi iliwasilisha bungeni Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/2027 –2030/2031 unaotarajiwa kugharimu Sh trilioni 477. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji), Profesa Kitila Mkumbo pia aliwasilisha Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051, Mpango wa Nne w…

ARUSHA: Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, amewataka Mawakili wa Serikali kuimarisha uwezo wao katika usimamizi wa mikataba mikubwa ya kiuchumi na uwekezaji ili kulinda maslahi ya taifa, huku wakihakikisha Tanzania inaendelea kuwa na mazingira bora yanayovutia wawekezaji. Pia amesema sheria na mikataba bora n…

ARUSHA: HOSPITALI ya Karoleni jijini Arusha imeendelea kuonyesha mafanikio makubwa katika sekta ya afya na kuibuka kuwa miongoni mwa vituo vinavyochangia ukuaji wa utalii wa afya nchini Tanzania, baada ya kuhudumia wagonjwa wageni zaidi ya 1,110 kutoka nje ya nchi. Hayo yamebainishwa leo Juni 6,2026 Katibu wa NEC, Iti…

ZANZIBAR : RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar itaendelea kuwakaribisha wawekezaji wa kimataifa kutokana na uwepo wa fursa nyingi za uwekezaji zinazohitaji nguvu ya wadau na taasisi za nje.

TANZANIA imeitaka jumuiya ya kimataifa kuongeza uwekezaji, teknolojia na rasilimali fedha kwa ajili ya kurejesha ardhi iliyoharibika na kukabiliana na kuenea kwa hali ya jangwa na ukame, huku ikisisitiza umuhimu wa kulinda maeneo ya malisho, misitu na vyanzo vya maji. Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Mak…

DAR ES SALAAM: TANZANIA imeendelea kung’ara katika anga la kimataifa baada ya kuingiza vipengele 41 katika Tuzo za Utalii na Usafirishaji Duniani (World Travel Awards), hatua inayoimarisha nafasi yake kama moja ya vinara wa utalii barani Afrika. Akizungumza, leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa…

DAR ES SALAAM; Wafanyabiashara wapatao 500 jijini Dar es Salaam wameshiriki mafunzo maalumu ya ununuzi wa umma yaliyoendeshwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA). Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za serikali kuwawezesha wazawa kushiriki kikamilifu katika zabuni za miradi ya umma. Akizungumza wakati wa …

DAR ES SALAAM: TAASISI ya Utamaduni na Maendeleo Afrika Mashariki (CDEA) imeendelea kuhamasisha matumizi ya urithi wa Afrika katika usanifu wa majengo na ubunifu wa ndani (interior design), kwa lengo la kuhakikisha utambulisho wa Mwafrika unazingatiwa katika ujenzi wa Afrika ya sasa na kizazi kijacho. Akizungumza kati…

MANYARA: CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewataka wamiliki wa vitalu na kampuni zinazojihusisha na uchimbaji na biashara za madini wanakamilisha kikamilifu dhana ya uwajibikaji kwa jamii(CSR), kikisisitiza fedha hizo si hisani bali ni wajibu wa kisheria kwa wananchi. Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa,…

KIGOMA: Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, MaryPrisca Mahundi ameitaka jamii kuwatenga watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, ubakaji na ulawiti. Naibu Waziri Mahundi amesema hayo wakati wa kongamano la wadau wa kupinga ukatili mkoani Kigoma akijibu tuhuma na malalamiko yal…

DAR ES SALAAM: Serikali imewahimiza wafanyabiashara na wawekezaji nchini kuchangamkia fursa za kiuchumi nchini China ili kukuza biashara zao na kuongeza mauzo ya bidhaa za ndani nje ya nchi. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo wakati akizindua Siku ya Huduma (Clinic Day) iliyoandali…

Chini ya kivuli cha miti mikubwa, meza ya plastiki ya buluu iligeuka kuwa ukumbi wa muda wa kusikiliza ushahidi. Juu yake kulikuwa na kompyuta mpakato, mafaili yaliyofungwa kwa utepe, nakala za hati za ardhi na nyaraka za mahakama zilizokusanywa kwa zaidi ya miongo mitatu. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalami…

RAIS wa Marekani, Donald Trump, amelihutubia taifa leo Alhamisi, akieleza mipango yake ya kuifanya Marekani kuwa imara zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

KATIBUMkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo inaendelea kuimarisha sekta ya elimu nchini kupitia matumizi ya teknolojia za kidijitali.

DAR ES SALAAM: KAMPUNI ya Oryx Tanzania imezindua kitabu cha Mwongozo wa Matumizi Salama ya Gesi ya LPG na kusaini mkataba wa ushirikiano wa miaka mitatu na Chama cha Skauti Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha elimu ya matumizi salama ya gesi ya kupikia kwa wananchi kupitia mtandao wa vijana wa skauti nchini. Akizun…

BENKI ya Maendeleo ya TIB imeahidi kuongeza juhudi katika kusaidia upatikanaji wa nishati safi ya kupikia katika maeneo ya vijijini na maeneo mengine ambayo bado hayajafikiwa kwa urahisi na huduma hiyo. Ahadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Deogratius Kwiyukwa, wakati wa mjadala wa jopo kuhusu nishati sa…

TANGA: Ili kudhibiti uingizwaji wa bidhaa za magendo katika mpaka wa Horohoro, Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Serikali imetangaza operesheni kabambe ya kusambaratisha magendo na biashara haramu zinazotishia usalama wa taifa na kupoteza mapato ya Serikali. Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa …

RWANDA; Dereva wa mbio za magari kutoka Tanzania, Ahmed Huwel, ameshika nafasi ya pili katika mashindano ya Rwanda Mountain Gorilla Rally, ikiwa ni sehemu ya Mashindano ya Afrika ya Mbio za Magari (African Rally Championship – ARC) yaliyofanyika nchini Rwanda mwishoni mwa wiki. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Rwanda, Huw…

MOROGORO: WIZARA ya Madini imesema mapato ya fedha yatokanayo na makusanyo ya madini yamevuka lengo la makadirio yaliyowekwa ya Sh trilioni 1.2 na kufikia Sh trilioni 1.36 katika kipindi cha Januari 2025 hadi Juni 23, 2026 ikiwa sawa na asilimia 113.34. Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Yahya Samamba amesema hayo J…

TANZANIA imepongezwa kwa utendaji mzuri wa kushughulikia changamoto za kiusalama katika Kanda ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya kuwa Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Pongezi hizo zimetolewa Agosti 15, 2025, wakati wa Mkutan…

DAR ES SALAAM: Wakulima na wanachama wa vyama vya ushirika nchini wanatarajiwa kunufaika na ongezeko la upatikanaji wa huduma za kidijitali na kifedha kupitia jukwaa la M-Kulima kufuatia Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC leo kusaini hati ya makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC) yenye l…

TANGA: WIZARA ya Maji imetangaza mikakati ya kuanzisha mfumo mpya wa upatikanaji wa fedha ujulikanao kama Alternative Financing, ikiwa ni jitihada za makusudi za kuharakisha ukamilishaji wa miradi mikubwa ya maji nchini na kuwaondolea wananchi kero ya ukosefu wa huduma safi na salama kwa wakati. Hayo yamebainishwa na …

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Wagombea wa Nafasi ya Urais na Wagombea Wenza kutoka vyama vya Siasa 16 vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi Oktoba, 2025. Mazungumzo hayo yalifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi, 2026.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Ali Mwinyi amesema njia bora ya kuuenzi urithi wa Hayati Rais Benjamin Mkapa ni kuendelea kuwekeza katika uongozi, kuimarisha sekta ya afya na kuwawezesha vijana kushiriki katika maendeleo ya Afrika.

DAR ES SALAAM: FAINALI za Kombe la Dunia 2026 zinatarajiwa kuvunja rekodi mpya duniani baada ya idadi ya timu kuongezeka kutoka 32 hadi 48 huku mechi zikiongezeka kutoka 68 hadi 104 katika mashindano yatakayofanyika kwa mara ya kwanza katika mataifa matatu ya Marekani, Canada na Mexico. Kutokana na ukubwa huo wa mashi…

DAR ES SALAAM; MKURUGENZI wa Mashitaka (DPP) amesema hana nia ya kuendelea kuwashitaki washitakiwa 20 kati ya 22 walioko katika kesi ya uhaini inayomkabili mfanyabiashara Jennifer Jovin(26) na wenzake 21. Hayo yameelezwa Wakili wa Serikali, Titus Aaron leo Novemba 25,2025 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es…

IRINGA: Wakulima waliojitokeza katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika kwa mara ya kwanza mkoani Iringa wameendelea kuvutiwa na teknolojia bunifu zinazowasilishwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), huku taasisi hiyo ikisisitiza kuwa matumizi ya matokeo ya tafiti ndiyo njia ya kuongeza uzalishaji, thama…

BUNDA: CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kitahakikisha kinatoa msukumo kwa serikali ili kuhakikisha mradi mradi wa maji kutoka Butiama hadi Nyamuswa unakamilika kwa wakati ili kutimiza azma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya Kumtua mama ndoo kichwani. Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Magunzo wa CCM, Kihongosi ameeleza h…

MTWARA: KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2026, Wazo Mwang’onda ameridhishwa na mradi wa ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Mbawala iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini mkoani Mtwara uliyogharimu Sh milioni 49.5. Mwenge wa Uhuru umepokelewa jana katika kijiji cha maili kumi kilicho…

IRINGA: MKOA wa Iringa umeingia katika hatua nyingine ya mapambano dhidi ya utapiamlo na lishe duni baada ya Mkuu wa Mkoa, Kheri James, kutangaza sera ya uwajibikaji mkali kwa watendaji wote wanaosimamia masuala ya lishe. Aidha, ameonya halmashauri itakayoshindwa kufikia asilimia 95 ya viashiria vya utekelezaji italaz…

IRINGA: UHUSIANO uliokuwa na uhasama kati ya wananchi na Hifadhi ya Msitu wa Makere Kusini, maarufu Kagera Nkanda, wilayani Kasulu mkoani Kigoma, umeanza kuimarika kufuatia utekelezaji wa mradi wa uhifadhi shirikishi unaowakutanisha wananchi wa vijiji vinne vinavyozunguka hifadhi hiyo pamoja na mamlaka za usimamizi wa…

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi, amewataka wahitimu wa Taasisi ya Teknolojia ya India Madras (IIT Madras) kutumia elimu, maarifa na ubunifu wao kama nyenzo za kutatua changamoto za jamii, kuboresha maisha ya wananchi na kuchangia maendeleo endelevu.

TANGA: JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limeendelea kudhibiti vitendo vya uhalifu, baada ya kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa 200 katika operesheni maalumu zilizofanyika kuanzia Juni 1 hadi Julai 16, 2026. Akizungumza leo Julai 17, 2026 Tanga, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi, amesema kuwa Katika kipin…

DAR ES SALAAM: Katika hatua muhimu kwa sekta ya benki nchini na uongozi wa taasisi za kibiashara barani Afrika, Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna anatarajiwa kuzungumza katika Jukwaa la Mkutano wa Biashara Afrika 2026 utakaofanyika Mei 30, 2026 nchini Uingereza. Katika jukwaa hil…

MAREKANI imewataka raia wake wanaoondoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kukaa nje ya nchi hiyo kwa siku 21 kabla ya kuruhusiwa kuingia nchini. Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia tahadhari ya Vituo vya Marekani vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) iliyosema wasafiri wanaotoka DRC, Uganda na Sudan Kusini watafua…

ARUSHA: Wagonjwa 258 waliobainika kuhitaji upasuaji mkubwa katika Kambi ya Matibabu ya Bure iliyoratibiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Paul Makonda, wanatarajiwa kuanza kupatiwa matibabu ya kibingwa wiki ijayo katika hospitali mbalimbali za rufaa nchini. Akizu…

SERIKALI ya Tanzania na Misri zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya kilimo, hususan kilimo cha umwagiliaji, kwa lengo la kuongeza uzalishaji wa chakula na kuimarisha usalama wa chakula nchini.

ARUSHA: Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Dk, Toba Nguvila, amewasisitiza watendaji wa serikali katika mkoa huo, kuanzia sekretarieti ya mkoa, halmashauri taasisi na mashirika yote ya umma, kufanya kazi kwa ushirikiano kisekta ili kutimiza adhma ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati. Dk …

MANYARA: UBORESHAJI wa miundombinu ya huduma za afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vifo vinavyotokana na ajali za barabarani na dharura mbalimbali, kutokana na kuongezeka kwa uwezo wa hospitali kutoa huduma za haraka na za kibingwa. Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi n…

DAR ES SALAAM: Ubunifu wa Saratani AI na Dawa Mkononi ni miongoni mwa miradi iliyoanzia katika tukio la Winning Line Academic Event la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), ambayo sasa imeendelea kutoa suluhisho kwa wananchi ndani na nje ya Tanzania. Ubunifu huo umetajwa kuwa sehemu ya mafanikio…

UFILIPINO; TIMU ya taifa ya wanawake ya mchezo wa Futsal ya Tanzania, imeaga michuano ya kombe la dunia baada ya kufungwa mabao 9-0 na Japan kwenye Uwanja wa Philsports mjini Manila, leo Novemba 29, 2025. Michuano hiyo inafanyika kwa mara ya kwanza na Tanzania ikiwa miongoni mwa timu zilizoweka historia kushiriki baad…

SHINYANGA: KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, ameweka Jiwe la Msingi katika jengo la wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Kakola, Kata ya Bulyanhulu, Halmashauri ya Msalala, Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, lililogharimu zaidi ya Sh milioni 269. Akisoma taarifa ya ujenzi huo kabla ya kuwek…

TABORA: Utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha kutoka Makutopora – Tabora unatarajiwa kukamilika mwaka 2028 huku kazi za ujenzi zikiendelea kwa kasi katika maeneo mbalimbali ya mradi. Meneja wa Mradi huo, Mhandisi Christopher Kalisti anasema mradi huo unahusisha ujenzi wa kilomita 294 za nj…

DAR ES SALAAM: Simba SC wametanga kumnasa mshambuliaji, Ibrahim Doumbia kutoka QS Korofina ya Mali kwa mkataba wa miaka miwili. Simba SC wanaendelea kutambulisha wachezaji wapya kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu. Hadi sasa wamewatambulisha wachezaji wanne. Wachezaji hao ni Bakari Msimu, Kelvin Nashon, Nathaniel Chilambo…

TIMU nne za Tanzania zinazoshiriki mashindano ya kimataifa za Yanga, Simba, Azam FC na Singida Black Stars zimeanza vizuri mashindano hayo mwishoni mwa wiki iliyopita. Timu hizo zote zilicheza mechi zake hizo za kwanza ugenini na kuanza vizuri kwa ushindi wa mabao tofauti, huku Yanga wakishinda mabao 3-0 ambapo walich…

NAIBU Waziri wa Afya, Dk Florence Samizi, kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa, ametembelea na kuwajulia hali majeruhi wa ajali ya basi na lori iliyotokea usiku wa Desemba 31, 2025 katika kijiji cha Maseyu, mkoani Morogoro. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Dk Samizi amesema hadi Januari 2, majeruhi 5 w…

WAKATI Tanzania ikiendelea kupata mafanikio katika mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI (UNAIDS) limeonya kuwa kupungua kwa ufadhili wa kimataifa kunaweza kuhatarisha mafanikio hayo.

ARUSHA: SERIKALI itaendelea kuongeza nguvu katika uhifadhi wa wanyamapori aina ya faru ambao wapo haratini kutoweka kwa kuimarisha Mradi wa Kimkakati wa Uhifadhi wa Faru Weupe ili kuongeza chachu ya ongezeko la uhifadhi na utafiti wa wanyamapori waliopo nchini. Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ha…

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amezindua huduma za usafiri wa umma kwa kutumia mabasi ya umeme pamoja na Kituo cha Mabasi cha Malindi, ikiwa ni hatua muhimu katika kuboresha mfumo wa usafiri na kuhamasisha matumizi ya nishati safi visiwani Zanzibar.

“WALINIAMBIA sitafika mbali. Wengine walisema bora nipewe mtaji niuze machungwa kuliko kuendelea kuota ndoto za kurudi shule.”

KILIMANJARO; WATU watatu, akiwemo Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kotela Mashariki, wamefariki dunia kwa madai ya kujinyonga katika matukio tofauti yaliyotokea Julai 21 na 22, 2026 katika Kata za Mamba Kaskazini na Kilema Kati, Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, amethi…

ZANZIBAR; Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewahakikishia wananchi kuwa Serikali itawalipa fidia wote waliopisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, akisisitiza kuwa hakuna mwananchi atakayodhulumiwa haki yake. Rais Mwinyi amesema hayo leo tarehe 6 Janua…

SERIKALI ya Tanzania imeibuka mshindi wa tuzo ya kimataifa ya fedha za miundombinu kwa mwaka 2026, kufuatia mafanikio yake katika kupata mkopo wa masharti nafuu kwa ajili ya ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Umeme (SGR).

DAR ES SALAAM; MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru maelezo ya mashahidi na idadi ya vielelezo katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia (CHADEMA), Tundu Lissu kutopelekwa mubashara, kuchapisha wala kuhaririwa isipokuwa kwa amri ya mahakama. Mahakama hiyo imeeleza amri huyo imezingatia …
DODOMA; WIZARA ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imesema kufuatia utekelezaji wa vipaumbele vya wizara na kwa kuzingatia Malengo ya Kimkakati ya Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001, Toleo la Mwaka 2024, mafanikio mbalimbali yamepatikana. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa…

VIONGOZI wa masoko mkoani Dar es Salaam wamesema kupanda au kushuka kwa bei ya vyakula kunategemea zaidi upatikanaji wa bidhaa husika sokoni.

MOROGORO: MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amewaagiza watendaji wa mitaa, vijiji na kata za mkoa huo kushughulikia kikamilifu migogoro ya ardhi inayowakabili wanawake wanaponyang’anywa umiliki baada ya wanaume wao kufariki au kutengena pamoja na kudhibiti unyanyasaji wa kijinsia Malima ametoa agizo hilo katika ho…

WIZARA ya Madini imeingiza Sh trilioni moja katika makusanyo ya maduhuli ya sekta hiyo kati ya Julai mwaka jana na Juni 30, mwaka huu. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema makusanyo ya kiasi hicho hayajawahi kufanyika katika sekta hiyo.

NAFASI ya vyombo vya ulinzi na usalama inaendelea kuwa mhimili muhimu katika kulinda amani na utulivu wa muda mrefu nchini. Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano, Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Shule ya Sheria, Esaka Mugasa amesema utulivu wa nchi unatokana na juhudi za pamoja za taasisi zina…

MSANII nyota wa muziki wa Bongo Fleva na Mkurugenzi Mtendaji wa Wasafi Media, Diamond Platnumz anajiandaa kuachia wimbo wake mpya wa kimahaba uitwao ‘Natulizana’ ikiwa ni maalum kwa msimu wa Valentine. Hata hivyo, mbali na mashabiki kusubiri kwa hamu wimbo huo , gumzo kubwa limeibuka kuhusu saa ya kifahari inayoonekan…

PWANI: KAMPUNI ya Oryx Gas imekabidhi mitungi ya gesi ya kupikia 600 kwa makundi mbalimbali ya wajasiriamali wakimo mama lishe huku Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Subira Mgalu akieleza kuwa uamuzi wa Oryx kugawa mitungi hiyo kunakwenda kuondoa athari za kiafya zinazotokana na matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa. …

Na Frank Leonard, Mufindi Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Mufindi Kusini, David Kihenzile, ameongoza mamia ya wananchi wa jimbo hilo katika mkutano wa kufunga kampeni uliojaa hamasa na matumaini, akiwataka Watanzania wote kujipanga kwa amani, umoja na maendeleo kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29.…

RUSHA; Zaidi ya wakulima 2,000 Wilaya ya Monduli mkoani Arusha wanatarajiwa kunufaika na ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Bonde la Mto wa Mbu, mradi unaolenga kuimarisha kilimo endelevu cha mazao ya chakula. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Raymond Mndolwa, wakati akisoma taarifa ya …

ZAIDI ya vijana 8,600 wamefikiwa na Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kupitia programu za ujasiriamali na ubunifu, hatua iliyowezesha vijana 1,520 kubuni mawazo ya biashara na kuanzisha zaidi ya biashara 50, huku kampuni 12 zikisajiliwa rasmi.

DAR ES SALAAM: Uteuzi wa jaji kutoka Tanzania kujiunga na jopo la Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) umeibua mjadala miongoni mwa wachambuzi wa sheria na watetezi wa haki za binadamu barani Ulaya, hali inayoonyesha mvutano mpana kuhusu uhusiano wa mahakama hiyo na mataifa ya Afrika pamoja na wasiwasi kuhus…

DODOMA. Waziri Mkuu Dk Mwigulu Nchemba amezitaka wizara na taasisi zinazonufaika na fedha za NBC Marathon zihakikishe zinatumika kwa uwazi na kwa kuzingatia thamani ya fedha, ili malengo yaliyokusudiwa yaweze kuleta matokeo, tena matokeo yanayopimika. Amesisitiza kuwa kila shilingi inayowekezwa katika mbio hizo zinapa…

DAR ES SALAAM: MCHAMBUZI maarufu wa Michezo nchini, Ansibert Rafael ‘Hans Rafael’ ametoa tathmini yake kuhusu Simba SC kushindwa kurudisha ubora wao ndani ya ligi na michuano ya kimataifa pia. Akitoa tathmini yake kupitia mtandao huu wa HabariLeo mapema leo Aprili 15, Hans Rafael amesema changamoto kubwa ya Simba SC n…

ARUSHA: Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya utalii katika Destination Tanzania Stakeholders Forum 2026 iliyofanyika jengo la Ngorongoro, Arusha, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika kuitangaza Tanzania na kuongeza ushindani wa sekta ya utalii duniani. Jukwaa hilo liliwakutan…

DAR ES SALAAM : DURU ya nne ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu kwa mwaka 2025/2026 imezinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku waandishi wa habari wakihimizwa kujiandaa na kuwasilisha miswada yao kwa ajili ya kushiriki katika mchakato wa ushindani.

DAR ES SALAAM: NAIBU Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile, amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kuwachukulia hatua watumishi wanaoshindwa kutoa huduma bora kwa wananchi. Kihenzile ametoa agizo hilo wakati akizungumza na wafanyakazi wa ATCL, ambapo amesisitiza umuhimu wa watumishi kuwaheshim…

DAR ES SALAAM: Mkurugenzi wa Monti International School, Fatma Fernandez, amesema shule hiyo imeanzisha mpango maalumu wa kuimarisha mchezo wa kuogelea nchini kwa kumwalika kocha wa kimataifa, Ben Lee kutoka Marekani, mwenye uzoefu wa kufundisha katika kiwango cha NCAA na Olimpiki. Amesema lengo la ujio wa kocha huyo …

NOVEMBA 4, mwaka 2025 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilimtangaza Miguel Gamondi kuwa Kaimu Kocha Mkuu wa Taifa Stars, akichukua nafasi ya Mtanzania Hemed Suleiman ‘Morocco’. TFF na Morocco walifikia makubaliano ya pande zote mbili kuvunja mkataba baina yao na sasa TFF chini ya Rais wake, Wallace Karia ku…

DODOMA:Serikali imesema itatoa kipaumbele kwenye sekta ya kilimo katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2026/27, ikiitaja kuwa miongoni mwa sekta zitakazochochea mageuzi ya uchumi, kuongeza uzalishaji na kufungua fursa za ajira nchini. Akiwasilisha mpango huo bungeni, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na U…

SHINYANGA: ZAIDI ya wanafunzi 600 wa shule za msingi katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga wamenufaika na huduma ya miundombinu ya mazingira baada ya Shirika la Water for Good kujenga vyoo 22 vyenye matundu 93. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi kutoka Shirika la Water for Good nchini Tanzania Devocatus Kamara katika ha…

DAR ES SALAAM: Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19. Katika hukumu iliyotolewa Juni 1, …

WATUHUMIWA wawili, Marco Maginga (47) na Mwita Maginga (45), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Musoma, mkoani Mara, wakikabiliwa na shtaka la mauaji ya mwanamke Rodha Jonathani (42).

KIKOSI cha awali cha wachezaji 30 wa timu ya taifa ya wanawake kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanawake (WAFCON 2026) kimetangazwa. Wachezaji walioitwa katika kikosi hicho kitakachokuwa chini ya Kocha Mkuu Bakari Shime ni Najiath Abbas, Asha Mrisho, Nusrat Jafar, Husna Mtunda, Enekia Kasonga, Li…

MSEMAJI wa chama tawala cha Uganda, National Resistance Movement (NRM), amesema kuwa wapiga kura wa nchi hiyo wako tayari kumuunga mkono mgombea wa urais kutoka katika mazingira yoyote, mradi awe na sifa zinazokubalika za uongozi.

DAR –ES-SALAAM : VYAMA vikuu vya siasa nchini vimeweka upatikanaji wa Katiba Mpya kama kipaumbele katika ilani zao kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, hatua ambayo imeibua matumaini mapya ya kufufua mchakato huo uliochukua zaidi ya muongo mmoja bila mafanikio.

DAR ES SALAAM; Rais wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa nchini, Ikulu Dar es Salaam, Julai 30, 2026.

MBEYA: Watu wanne wamefariki na wengine 29 kujeruhiwa kufuatia ajali ya basi la abiria iliyotokea mkoani Mbeya baada ya gari hilo kuacha njia na kupinduka katika eneo lenye kona kali kwenye barabara ya Mbeya kuelekea wilayani Chunya. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga, amesema ajali hiyo ilitoke…

DAR ES SALAAM; TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Sahara Ventures, imezindua rasmi programu ya kitaifa ya kuharakisha ukuaji wa biashara changa na kuimarisha mfumo wa ubunifu nchini (Tanzania Ventures Lab). Mfumo huo utalenga kuunganisha wabunifu, watafiti, wawekezaji kutoka sekta bin…

VIENNA, AUSTRIA : TANZANIA imeahidi kuendeleza mapinduzi ya kidigitali katika sekta ya elimu kupitia ushirikiano na Kampuni ya eee Austria.

DAR ES SALAAM:RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kesho Machi 3, 2026 katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa matenki 15 ya kuhifadhia mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari wa habari leo Machi 2, 2026 na Waziri wa Uchukuzi, Makame Mbarawa…

MTOTO njiti ni mtoto anayezaliwa kabla ya muda wa kawaida wa mjamzito kujifungua wa wiki 37 za ujauzito. Inakadiriwa watoto njiti milioni 13.4 walizaliwa mwaka 2020, ikiwa ni takribani mtoto mmoja kati ya 10.

MOROGORO: MKUU wa Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, Maulid Dotto amewataka wananchi wa wilaya hiyo kuacha kufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji na misitu ya asili. Aidha, amewataka wajenge tabia ya kuhifadhi mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabiachi na kuondokana na changamoto za kimazingir…

DAR ES SALAAM: Wanawake, vijana na watu wenye ulemavu wameendelea kunufaika na programu za uwezeshaji zinazolenga kuwajengea uwezo wa kiuchumi kupitia mafunzo ya ujasiriamali na matumizi ya teknolojia za kifedha. Meneja wa Vodacom Tanzania Foundation, Sandra Oswald, amesema taasisi hiyo inaendelea kutekeleza programu …

DAR ES SALAAM; Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali itaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya wanaojihusisha na utoroshaji wa madini, baada ya kukamatwa kwa dhahabu yenye uzito wa kilogramu 4.4 iliyokuwa ikisafirishwa kinyume cha sheria, yenye thamani ya Shi bilioni 1.38. Akizungumza na waandishi wa habar…

SHINYANGA: MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita amesema maofisa maendeleo ya jamii na madiwani wasikwepe kusimamia mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri ili vikundi mbalimbali vyenye sifa vinufaike na mikopo hiyo. Mboni Mhita amesema hayo kwenye mkutano wa hadhara alipokuwa akisikiliza kero mbalimbali kat…

DODOMA: MBUNGE wa Jimbo la Malinyi, Dk. Mecktridis Mdaku, ameiomba Serikali kuchukua hatua za makusudi za kuboresha Sekta ya kilimo wilayani humo, akisisitiza kuwa maboresho ya miundombinu na upatikanaji wa ardhi ndiyo suluhu ya kuinua uchumi wa wakulima wadogo na wa kati. Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya…

DODOMA; TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), imetoa ufadhili wa Sh milioni 400 kwa ajili ya Mradi wa kuimarisha uwezo wa wafugaji kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi unaotekelezwa na Watafiti wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), ikilenga kutatua changamoto ya upatikanaji wa malisho kwa wafugaji …

Samia anadi sera za CCM Uyole

Tukio Kubwa Zaidi la Kilimo Barani Afrika: Fursa ya Kipekee Kuingia katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Chakula Inayokua kwa Kasi Tanzania 2–3 Septemba 2026 | Viwanja vya Maonesho vya Biashara vya Mwalimu J.K. Nyerere, Dar es Salaam, Tanzania Sekta za kilimo, mifugo na usindikaji wa chakula barani Afrika zinaendelea kus…

DODOMA: Shirika la AGRA limeanza kutoa mafunzo maalum ya uchambuzi wa hatari za tabianchi kwa wadau wa sekta ya kilimo nchini, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kusaidia Tanzania kujenga mifumo ya chakula na kilimo inayohimili mabadiliko ya hali ya hewa. Mafunzo hayo ya siku mbili kuhusu Climate Vulnerability Mapping and R…

DODOMA: SERIKALI imewataka viongozi wa vyama vya ushirika nchini kuendesha taasisi hizo kwa uwazi, uwajibikaji na uadilifu, huku ikionya kuwa haitasita kuwachukulia hatua kali za kisheria watakaobainika kujihusisha na ubadhirifu wa fedha za wanachama. Aidha, serikali imewaagiza wakurugenzi wa halmashauri pamoja na waa…

KAGERA: Wadau wa kahawa mkoani Kagera kupitia kikao cha wadau wa zao hilo wamepongeza mabadiliko ya kimfumo ya ununuzi kwa njia ya mnada na kudai kuwa mfumo huo umeongeza uwazi wa bei na ushawishi wa kulima kwa wingi. Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Yahya Kido amesema Mkoa wa Kagera unaendelea kufanya vizuri katika uzalishaji…

ARUSHA: KATIKA jitihada za kukuza ushirikiano kati ya taasisi za mafunzo na wenye viwanda na waajiri, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Hussein Mohamed Omar amehimiza Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kushirikiana na wamiliki wa viwanda. Hususani Dk Omar aliiisisitiza VETA k…

DAR ES SALAAM: Serikali imesema imekamilisha maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Afrika50 na Jukwaa la Miundombinu Afrika, utakaofanyika Agosti 5 hadi 6, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam. – Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 1,20…

DAR ES SALAAM: Kampuni ya Teknolojia na Mawasiliano Vodacom Tanzania imeendelea kujikita katikati kukuza uchumi kupitia maendeleo ya kidijiti kwa kutumia teknolojia bunifu kuongeza ujumuishwaji kifedha kwa Watanzania. Kampuni hiyo imedhihirisha hayo leo Aprili 2,2026 kupitia uwekezaji wa mabadiliko ya mifumo katika hu…

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba amesema maendeleo ya kudumu ya Taifa hayawezi kupatikana bila kujenga wananchi wenye maadili, uzalendo, uwajibikaji na mshikamano, sambamba na kuendelea kuimarisha utawala wa sheria na taasisi za umma.

WAKALA wa Vipimo (WMA) umesisitiza kuendelea kufanya ukaguzi wa matumizi ya vipimo sahihi kwenye maeneo ya uzalishaji, maghala yanayouza bidhaa kwa ujumla na masoko ili kukuza uchumi imara, jumuishi na ushindani. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Meneja wa WMA Mkoa wa Dodoma, Saidi Ibrahimu, wakati wa kukabidh…

GEITA: SERIKALI kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) imeweka mpango wa muda mrefu wa kuchimba visima 150 katika halmashauri za mkoa wa Geita ili kukuza sekta ya kilimo kupitia wakulima wadogo. Mradi wa visima ni sehemu ya mradi kilimo cha umwagiliaji unaohusisha usanifu na ujenzi wa mabwawa, visima na skimu za …

dodoma; MAMLAKA ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), imewahimiza wakulima na wafanyabiashara wa mazao nchini kuhakikisha wanaingia katika kilimo cha mkataba kupitia wadau waliosajiliwa na mamlaka hiyo, ili kujiepusha na hasara na migogoro inayotokana na mikataba isiyo rasmi. Rai hiyo imetolewa na Ofisa…

DAR ES SALAAM: Tanzania imeendelea kung’ara kimataifa baada ya Benki ya Dunia (World Bank – WB) kuitaja kuwa miongoni mwa nchi zilizo na ukomavu wa juu wa matumizi ya TEHAMA katika sekta ya umma, hatua inayothibitisha mafanikio ya mageuzi ya kidijitali yanayoendelea kutekelezwa na Serikali. Kwa mujibu wa Ripoti ya Uko…

DODOMA: Serikali imefungua fursa za biashara kwa Watanzania katika migodi, huku vijana na wanawake wakipewa kipaumbele ili kuongeza ushiriki wao katika Sekta ya Madini na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Hatua hiyo inalenga kujenga uchumi shindani na jumuishi unaowezesha Watanzania kushiriki k…

SERIKALI juzi imezindua Mpango wa ushirikiano baina ya waajiri, vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi na taasisi za elimu ya juu, ambao imesema ni wa lazima ili stadi zinazozalishwa ziwiane na mahitaji halisi ya soko la ajira. Imeeleza kuwa Sera ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inabainisha wazi kuwa ushirik…

PWANI: JESHI la Polisi Mkoani Pwani limemebaini baadhi ya wanafunzi walioshindwa kuripoti shuleni kunatokana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na migogoro ya kifamilia. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Salim Morcase, amesema kuwa hayo yamebainika mwe…

KIASI cha mazao yaliyouzwa kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala kimeongezeka kwa asilimia 43.6 katika mwaka wa fedha 2025/26.

WAHITIMU wa kozi mbalimbali katika Chuo Cha Usimamizi cha Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAMI) wametakiwa kukumbatia mageuzi ya kidigitali bila woga kwa uadilifu na maadili kwa maslahi ya Afrika ikiwa ni njia mojawapo ya kuinua uchumi wa bara hilo. Hayo yalisema jana katika mahafali ya 23 ya ESAMI ambapo wahi…

DAR ES SALAAM: Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba ameupongeza Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kwa utendaji kazi mzuri katika kuhakikisha nchi inakuwa na akiba ya mafuta ya kutosha. Salome Makamba ameyasema hayo alipozungumza na Menejimenti ya PBPA leo Desemba 6, 2025 jijini Dar es Salaam. “Nawapo…

TAASISI ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi, wakulima na wadau wa sekta ya kilimo kuhusu utambuzi wa mbegu bora, taratibu za usajili wa wazalishaji wa mbegu, pamoja na namna ya kuepuka mbegu bandia sokoni.

RAIS wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, amewasili jijini Dar es Salaam kwa ziara rasmi ya siku mbili kuanzia Agosti 5 hadi 6, 2026, kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan.

TANZANIA imehitimisha kwa mafanikio Jukwaa la Miundombinu Afrika na Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50, huku mikataba na makubaliano matatu muhimu katika sekta za umeme, gesi na afya yakisainiwa ili kuimarisha uwekezaji na maendeleo ya miundombinu nchini.

DAR ES SALAAM: Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeendesha mafunzo maalum kwa waandishi wa habari kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uelewa wa umma na wanachama kuhusu huduma, haki na wajibu unaotolewa na Mfuko huo. Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyoanza A…

JUHUDI za kupanua ujumuishaji wa kifedha nchini Tanzania zinaendelea kuimarika huku serikali na wadau wa sekta ya fedha wakitafuta njia mbalimbali za kuwafikia wananchi wengi zaidi wanaofanya shughuli zao katika sekta isiyo rasmi. Hatua hizi zinaonekana kuwa muhimu katika kuhakikisha kuwa Watanzania wengi wanapata fur…

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, ameteua wabunge sita kuingia katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Moses Kusiluka imeeleza kuwa uteuzi huo unaanza leo Novemba 10.

MOROGORO: Serikali imeeleza kuwa itaendelea kuweka mazingira wezeshi katika vituo vya ubunifu na kongani za biashara ili kuhakikisha havibaki kuwa maeneo ya mafunzo pekee, bali vinakuwa chachu ya kuzalisha biashara zinazokua, kutengeneza ajira, kuongeza mauzo ya nje na kuchangia ukuaji wa uchumi na pato la taifa. Naib…

MOROGORO: SERIKALI inaendelea kuweka jitihada kubwa katika kuzuia maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU) kwa kununua na kufunga mashine za kutolea huduma za kinga na Kipimo vitepe vya JIPIME kupitia mashine ya Ugavi wa Kidijitali kwenye vyuo vya elimu juu . Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Urati…

MTWARA: JAMII mkoani Mtwara imetakiwa kuhakikisha watoto wananyonyeshwa maziwa ya mama pekee bila kuchanganya na kitu chochote ili aweze kupata mkuzi sahihi. Hayo yamejiri wakati wa kikoa cha wadau mbalimbali mkoani humo wakiwemo asasi za kiraia cha robo mwaka kuhusu kufanya tathmini ya shughuli zilizofanyika kuanzia …

DODOMA:WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umebainisha kuwa umefanya maboresho makubwa katika mfumo wake wa usajili ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi. Akizungumza katika maonesho ya wakulima nane nane jijini Dodoma, Ofisa Usajili wa BRELA, Yusuf Mwasakafyuke, amesema wananchi wanaweza kupa…

DAR ES SALAAM: ZAIDI ya watu 2,000 wanatarajiwa kushiriki mbio za Dar Night Run 2026 zilizoandaliwa na The Runners Club zitakazofanyika Agosti 29, mwaka huu katika Viwanja vya Police Officers Mess, Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti wa Dar Night Run, Godfrey Mwangungulu, amesema maandalizi ya mbio hizo kwa msimu wa tisa…

DAR ES SALAAM:CHAMA Cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) na Chama Cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) wameiomba serikali kurejesha mfumo wa kutoa mizigo kidogo kidogo ili kusaidia kupunguza gharama kwa wafanyabiashara. Hayo ameyasema leo Aprili 24 na Mwenyekiti wa Chama Cha Mawakala Wa Forodha Tanzania(TAFFA),…

MWANZA: WAKULIMA kutoka Kanda ya Ziwa na mikoa jirani wamehimizwa kujifunza mbinu mpya za kidijitali kugundua mbegu feki na halisi za mazao kupitia Maonesho ya Wakulima ya Nane Nane yanayoendelea viwanja vya Nyamongolo jijini Mwanza. Akizungumza Agosti 3, 2026, Meneja wa Taasisi ya Udhibiti wa Ubora wa Mbegu Tanzania …

RAIS Samia Suluhu Hassan amewaapisha mawaziri na naibu mawaziri huku akiwataka kutenda kazi kwa kwenda mbio na kutafuta fedha za ndani kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo. Akizungumza baada ya kuwaapisha mawaziri 27 na Naibu mawaziri 29 katika Ikulu ya Chamwino, Rais Samia amesema changamoto iliyopo ni uchache…

KAGERA: Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk. Bashiru Kwakurwa, amevitaka vyama vya ushirika kushirikiana na wakulima wao kutafuta taasisi za kifedha kwa ajili ya kupata elimu ya mikopo ili kuendeleza sekta ya kilimo, kuongeza thamani na ubora wa mazao pamoja na kutafuta masoko ya ndani na nje ya nchi yanayozingatia ubora. A…

Dodoma: Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imepanga kushiriki Maonesho ya Kilimo ya Nanenane Kitaifa 2026 yatakayofanyika kuanzia Agosti 1, 2026 kwenye viwanja vya Dk John Malecela, Dodoma, ikiwa na mpango maalumu wa kuwaunganisha wadau wa sekta ya nafaka na mazao mchanganyiko na fursa za maso…

DODOMA; KUPITIA Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Yas Kanda ya Kati, Said Idd ameeleza namna Yas inavyochangia mageuzi ya sekta ya kilimo kupitia mawasiliano bora na ya kisasa kwa wakulima kote nchini. Akinukuu ripoti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo iliyoishia Juni 2025…

MAKAMU wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema viongozi wa dini wana wajibu wa pekee wa kuliombea taifa kama ambavyo Biblia Takatifu ilivyoelekeza. Dk Nchimbi aliyasema hayo wakati wa hafla ya kusimikwa Uongozi wa Kitaifa wa Awamu ya Tano wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPTC) iliyofanyika katika Uk…

SIMIYU : BAADHI ya wajumbe wa Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii wamewasili mkoani Simiyu kwa ajili ya kutoa elimu ya uhifadhi kwa jamii.

MULEBA: Mkoa wa Geita umekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Kagera katika hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Nyakabango, Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, huku viongozi mbalimbali na wananchi wakishiriki mapokezi hayo. Mwenge huo umekabidhiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita, Mohamed Gombati, kwa Katibu Tawala wa M…

DODOMA: WIZARA ya Viwanda na Biashara imeeleza kuwa inaendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza tija, hatua inayolenga kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Imeelezwa kuwa Serikali inaweka mazingira yatakayomwezesha Mtanzania kuongez…

BARIADI; MKUU wa Mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha, ametoa wito kwa wakazi wa mikoa ya Kanda ya ziwa Mashariki na maeneo jirani kujitokeza kwa wingi katika maonesho ya Nanenane yatakayofanyika kwenye viwanja vya Nyakabindi, Simiyu. Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya wakuu wa mikoa ya Kanda ya ziwa Mashariki…

ZANZIBAR: WASANII na vikundi 19 kutoka Tanzania, Afrika Kusini, Burundi, Mexico, Chile na Canada wanatarajiwa kupanda jukwaani katika msimu wa pili wa Tamasha la FuTopia. Tamasha hilo litakalofanyika kwa siku mbili, Agosti 8 na 9 katika eneo la Fumba Town, Zanzibar limeandaliwa na Busara Promotions, waandaaji wa Sauti…

UFARANSA: RAIS wa Ufaransa, Emmanuel Macron, anakabiliwa na changamoto kubwa ya kidiplomasia wakati nchi hiyo ikijaribu kujenga upya uhusiano wake na Afrika baada ya miaka kadhaa ya kupungua kwa ushawishi, kuongezeka kwa hisia za kupinga Ufaransa na ushindani kutoka kwa mataifa makubwa yanayotaka kuongeza uwepo wao ba…

DAR ES SALAAM; MECHI ya Simba dhidi ya Yanga Ligi Kuu Tanzania Bara itachezwa Jumapili Mei 3, 2026 kuanzia saa 12 jioni, Ilikuwa inaonekana mbali sana. Ipo hivi Mei 3, 2026 ilikuwa inaonekana mbali sana, baadaye ikaja mechi wiki ijayo, kuanzia Jumatatu wafurukutwa wa mpira wakaanza kusema wiki hii, baadaye ikawa inata…

DAR ES SALAAM: Mamia ya wanafunzi wanatarajia kwenda masomoni kwenye vyuo vikuu mbalimbali nchini India kuanzia wiki ijayo kupitia Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL). Wanafunzi hao na wazazi wao walihudhuria mkutano uliofanyika katika ofisi za GEL mwishoni mwa wiki kwaajili ya kupewa mafunzo ya na…

DODOMA: NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Denis Londo, amepongeza Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) kwa mpango wake wa kuwajengea watoto uelewa wa vipimo, akisema hatua hiyo imezaa mabalozi wanaoweza kueneza elimu hiyo kwa jamii. Londo alitoa pongezi hizo baada ya kupokea elimu kuhusu umuhimu wa kutumia vipimo sahihi…

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Ali Mwinyi, amesema Taasisi za Elimu ya Juu zina mchango mkubwa katika kukuza sekta ya elimu na kuandaa rasilimali watu wenye ujuzi, maarifa na weledi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Dk Mwinyi ameyasema hayo leo Desemba 17, 2025, alipokuwa mgeni rasmi …

DAR ES SALAAM; Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)-Mloganzila imepandikiza figo wagonjwa wanne katika kambi maalumu iliyofanyika Agosti 16 hadi 19, mwaka huu, huku jumla ya wagonjwa 28 wakifanyiwa huduma hiyo tangu kuanza Aprili 2023. Akizungumza baada ya kutembelea wagonjwa hao, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Upasua…

WAANDISHI wa Sheria kutoka Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) wamefanya ziara ya mafunzo nchini Uingereza, ikiwa ni sehemu ya ushiriki wao katika Mkutano wa Jumuiya ya Waandishi wa Sheria wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth Association of Legislative Counsel – CALC), Kanda ya Ulaya. Ziara hiyo ni utekelezaji wa m…

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu pamoja na wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba katika futari ya pamoja aliyowaandalia.

DAR ES SALAAM: Tanzania inalenga kuvutia mitaji mikubwa zaidi kutoka Ulaya kwa kuimarisha mazingira ya uwekezaji kwa sekta binafsi, hatua inayotarajiwa kuongeza ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi. Waziri wa Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo ameeleza hayo leo Agosti 27, Dar es Salaam, katika mkutano wa masha…

DODOMA; WAZIRI wa Uchukuzi, Prof Makame Mbarawa ametoa maagizo kadhaa kwa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA kuhakikisha yanatekelezwa ili kukabiliana na changamoto za usafiri kwa wanafunzi. Ametoa kauli hiyo leo Februari 4, 2026 mjini Dodoma alipokuwa akizungumzia picha mjongeo ya mwanafunzi wa Shule ya Sekon…

WATU watatu wa familia moja wamekufa na mmoja kunusurika baada ya ajali ya moto iliyotokea katika moja ya nyumba zilizopo katika Mtaa wa National, Kata ya Magu, Halmashauri ya Wilaya ya Magu mkoani Mwanza.

Bodi ya Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC), ikiongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Joseph Msambichaka, imefanya ziara ya kikazi katika Bandari ya Dar es Salaam kwa lengo la kujionea namna ukaguzi wa makasha kwa kutumia teknolojia ya skana unavyotekelezwa na jinsi TAEC inavyosimamia matumizi salama ya mionzi katika vi…

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Maendeleo na Mitaji (UNCDF) limesema kuwa linaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2030. Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Peter Malika amesema baada ya shirika hilo kutoa majiko ya kisa…

DAMASCUS : RAIS wa Syria, Ahmed al-Sharaa, amesema juhudi za kuunganisha taifa hilo baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe hazipaswi kufanyika kwa njia ya umwagaji damu.

KLABU ya Yanga imemtambulisha rasmi mshambuliaji mpya Laurindo Dilson Maria Aurélio maarufu kama Depu, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha kikosi chake katika dirisha dogo la usajili. Depu amesajiliwa akitokea Ligi ya Poland, hatua inayodhihirisha dhamira ya mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuongeza nguvu katika safu …

MOROCCO; HATUA ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) mwaka 2025 imekamilika na sasa macho yote michezo ya usu fainali itakayofanyika Jumatano Januari 14, 2026. Kwa mujibu wa ratiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Senegal itacheza na Misri kuanzia saa mbili usiku, kisha saa tan…

ZANZIBAR: Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Ali Abdulgulam Hussein amesema serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya michezo ikiwa pamoja na ujenzi wa viwanja na kuangalia fursa mbalimbali ili kuendeleza vipaji kwa vijana. Naibu Waziri huyo ametoa kauli hiyo katika uzinduzi wa Mash…

DAR ES SALAAM; WANANCHI wa maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam na mikoa mingine ya Tanzania, kuanzia jioni ya leo Septemba 7, 2025, hadi usiku huu, wameshuhudia hatua kwa hatua tukio la kupatwa kwa mwezi, ambalo pia limeshuhudiwa na maeneo mbalimbali duniani. Tangu jana Daily News Digital iliweka video fupi za mtaalamu…

DAR ES SALAAM: SHIRIKA la Uvuvi Tanzania (TAFICO), limesaini mkataba wa ujenzi wa meli mbili za uvuvi wa bahari kuu na Kampuni ya Rongcheng Xinyang Ship Industry Limited ya China, ikiwa ni hatua ya kuimarisha na kuongeza tija katika sekta ya uvuvi nchini. Mkataba huo umesainiwa leo, Agosti 24, 2026,Jijini Dar es Salaa…

WANANCHI wa Kata ya Msangamkuu, Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara mkoani Mtwara, wameishukuru Serikali kwa kuwajengea Kituo cha Afya cha Msangamkuu, kilichogharimu zaidi ya Sh milioni 25, wakisema kimewaondolea changamoto ya kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya. Wakizungumza wakati Waziri wa Viwanda na Biashara,…

ZANZIBAR; Rais wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, Agosti 14, 2026, amemkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, Cheti cha shukrani kwa kutambua ushiriki na mchango wa NSSF katika Tamasha la Kizimkazi 2026. Cheti hicho ni ishara ya kutambua mchango wa NSSF katika kuunga mko…

DODOMA; SERIKALI imesema ufanisi wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka 2026/27 utajengwa katika misingi mbalimbali ikiwemo kuendelea kuwepo kwa demokrasia, amani, usalama na utulivu wa ndani na katika nchi jirani. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji), Prof Kitila Mkumbo, ametoa kauli…

DAR ES SALAAM: SHIRIKA la My Legacy limekutana na asasi za kiraia zinazoshughulika na masuala ya wanawake, watoto na makundi maalumu kwa lengo la kuutambulisha mradi wa Mialo ya Kijani unaolenga kupaza sauti za wanawake wanaokabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kupitia filamu. Akizungumza wakati wa mkutano huo jana D…

MOROGORO; Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuweka mazingira bora na salama ya kazi kwa walimu wote nchini na kushirikiana bega kwa bega na Chama cha Walimu Tanzania (CWT)na vyama vyote ambavyo ni halali vya wafanyakazi, ili kuimarisha amani na utulivu mahala pa kazi ambayo ndio chimbuko la ustawi wa kiuchumi na ki…

ZANZIBAR: MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeahidi kuendeleza ushirikiano na Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar katika kutoa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yenye ubora kwa kwa wananchi wa pande zote mbili za Tanzania bara na Zanzibar. Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore amesema hayo Agost…

DAR ES SALAAM: Wanafunzi zaidi ya 95 kutoka Tanzania wameondoka nchini kwenda India kwa ajili ya kuendelea na masomo ya elimu ya juu katika vyuo mbalimbali, ikiwa ni kundi la kwanza kati ya wanafunzi 198 wanaotarajiwa kusafiri kwenda India kupitia Global Education Link mwaka 2026. Wanafunzi hao wameondoka kupitia Kitu…

DAR ES SALAAM: Serikali imesema imefanikiwa kuwaendeleza wabunifu 70 waliotokana na mashindano ya Sayansi na Teknolojia (MAKSATU), huku ikiwa katika hatua za mwisho za kufanya marekebisho ya Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia ili iwe Sera ya Sayansi, Teknolojia, Ubunifu na Ujuzi, hatua inayolenga kuendana na mahit…

DAR ES SALAAM: Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Kairuki, amesema upanuzi wa huduma za intaneti kupitia mkongo wa Taifa wa fiber optic ni hatua muhimu ya kufungua fursa za elimu, ajira, biashara, ubunifu na huduma bora kwa wananchi Kairuki amesema hayo Leo wakati wa uzinduzi wa awamu ya pili ya m…

HIVI karibuni, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde wakati akiweka jiwe la msingi la kiwanda cha kusafi sha na kusindika madini ya nikeli na shaba kinachojengwa na Kampuni ya Zhongzhou Mining, eneo la Zamahero wilayani Bahi mkoani Dodoma, alisema Tanzania itakuwa kinara wa mapinduzi ya uchumi wa kijani. Alisema katika ki…

DAR ES SALAAM: Mwimbaji maarufu wa Marekani, Trey Songz, anatarajiwa kuwasili Tanzania kesho, Agosti 12, 2026 kutumbuiza katika tamasha la IMBEJU Sauti Moja, litakalofanyika Agosti 14 Viwanja vya TTCL, Kijitonyama, Dar es Salaam. Ujio wa Trey Songz unatarajiwa kuwa kivutio kikubwa katika tamasha hilo litakalowakutanis…

IRINGA: Shule ya Sekondari Tosamaganga imezindua kampeni ya kukusanya Sh bilioni moja kwa ajili ya kuboresha miundombinu yake na kununua basi jipya la wanafunzi, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo mwaka 1926. Uzinduzi huo umefanywa na Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mj…

KAGERA: Timu ya Kamachumu Stars imeibuka bingwa wa mashindano ya Paul Mwijage Cup baada ya kuifunga Kanoni FC kwa bao 1-0 katika mchezo wa fainali na kujinyakulia kitita cha Sh milioni 3. Mashindano hayo yaliyoshirikisha timu 20 kutoka Tarafa ya Kamachumu, Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, yamekuwa kivutio kwa mamia ya…

DAR ES SALAAM: BENKI ya CRDB imetenga zaidi ya Sh milioni 120 kwa washindi wa mbio za marathon zitakazofanyika Agosti 16 Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na mgeni rasmi Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba. Zawadi kwa atakayetwaa medali ya dhahabu kwa mbio za kilometa 42 atazawadiwa Sh milioni 12, huku washindi wengine wa pil…

DAR ES SALAAM; KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imewahakikishia Watanzania kuwa itaendelea kuboresha huduma zake kwa kuboresha miundombinu, kupanua mtandao wa usambazaji, ili kutekeleza ajenda ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwa ajili ya afya bora, mazingira safi, na maendeleo endelevu. Akizungumza leo Desemba 1,2…

ARUSHA: Juhudi za wananchi wa Kitongoji cha Lailupa, Kijiji cha Meirugoi, Kata ya Gelai-Meirugoi wilayani Longido mkoani Arusha, za kujitolea kujenga darasa la shule ya awali (chekechea) lenye thamani ya Sh milioni 12, zimemgusa Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Steven Kiruswa, ambaye ameamua kugharamia hatua ya mwisho ya ukam…

TANGA: MAANDALIZI ya Mashindano ya Ujuzi Kitaifa (WorldSkills Tanzania 2026) yanayotarajiwa kufanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Usagara mkoani Tanga yamefikia hatua nzuri na kuridhisha. Hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Dkt. Mwajuma Li…

DAR ES SALAAM: BALOZI wa Uturuki nchini Tanzania, Bekir Gezer, amesema uhusiano kati ya Tanzania na Uturuki unaendelea kukua na kuimarika katika maeneo mbalimbali, akisisitiza kuwa ushirikiano huo utaendelea kuleta fursa na manufaa kwa wananchi wa nchi hizo mbili. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam baada ya…

ARUSHA: SERIKALI imesema kuwa zaidi ya asilimia 70 ya fedha zinazohitajika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 zinatarajiwa kutoka sekta binafsi, huku Mfuko wa Kukuza Ukuaji wa Uwekezaji Tanzania (TIGF) ukizinduliwa kama jukwaa la kuandaa miradi na kuunganisha fursa za maendeleo na mitaji ya wawekezaji wa ndani…

ARUSHA: Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amewataka vijana kuwa mabalozi wa mapambano dhidi ya dawa za kulevya kwa kuelimisha jamii, kushiriki kikamilifu katika juhudi za kuzuia matumizi ya dawa hizo. Lyimo ametoa kauli hiyo wakati akifunga Jukwaa la Vijana…

CONGO: TANZANIA imeunga mkono ajenda zote muhimu zilizojadiliwa katika Mkutano wa Tisa wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR). Makamu wa Rais, Balozi Dk Emmanuel Nchimbi alisema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye mkutano huo uliofanyika Kinshasha nchini…

TANGA: Ubunifu wa wanafunzi na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) umeendelea kuibua matumaini kwa wananchi katika kutafuta suluhisho za changamoto mbalimbali za afya zinazowakabili katika maisha ya kila siku. Kupitia banda la MUHAS katika Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubu…

DAR ES SALAAM; KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Mipango na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango, Dk Tausi Kida amewataka wavumbuzi, watafiti, wajasiriamali na wadau wa maendeleo kuchunguza namna mawazo mapya, teknolojia, utafiti, ujasiriamali, fedha na ushirikiano wa kimkakati vinavyoweza kuchangia utekelezaji wa Dira…

MBEYA; Serikali imewekeza takribani Sh bilioni 11 katika ujenzi wa Kituo cha Saratani cha Ocean Road (ORCI) Mbeya, kinacholenga kusogeza huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani karibu na wananchi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk Diwani Msemo, amesema kukamilika kwa kituo hicho kuta…

DODOMA: NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (anayeshughulikia afya), Jafar Seif, amesema ugatuzi wa madaraka ni miongoni mwa misingi muhimu ya kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuziimarisha Serikali za Mitaa ili ziweze kutoa huduma bora k…

TANGA; Waziri Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na taasisi zake kuhakikisha bunifu zinazozalishwa na Watanzania haziishii kuoneshwa kwenye maonesho, bali zinaendelezwa, zinalindwa na kupelekwa sokoni, ili zitoe suluhisho kwa changamoto mbalimbali na kuchangia ukuaji wa uch…

SERIKALI imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, ambapo jumla ya shilingi bilioni 4.2 zimetengwa katika kipindi cha miaka minne tangu kuanzishwa kwake.

MGOMBEA wa urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kuunda Tume Maalum itakayofanya tathmini ya kina kuhusu fidia walizolipwa wananchi waliopisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo ya Fumba, …

WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, ameagiza wajumbe wa kamati mapokezi na kamati za ujenzi za mradi wa ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Muheza wakamatwe mara moja na kuhojiwa kuhusu upotevu wa vifaa vya mradi huo.

DAR ES SALAAM; MFANYABIASHARA Jeniffer Jovin, maarufu ‘Niffer’(26)na wenzake 21wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakibabiliwa na makosa matatu yakiwemo ya uhaini. Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mwalimu, Lucianus Luchius (28), Paul Malima (28), Augustino Mulwale (30), Mohamed Kondo…

DODOMA; Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, ikiongozwa na Mwenyekiti wak, Deodatus Mwanyika, imeipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na taasisi zake kwa utekelezaji mzuri wa majukumu yake ya udhibiti ubora kwa ufanisi. Mwanyika amesema kuwa juhudi zinazofanywa na TBS kuhakikisha …

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Dk Bashiru Ally, amefungua Kongamano la Nne la Kimataifa la Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji (4tFAR4ViBE), huku akisisitiza matumizi ya sayansi, teknolojia na ubunifu katika kuendeleza sekta hizo kwa manufaa ya Taifa. Kongamano hilo la siku tatu limeanza leo, Agosti 24, 2026, kati…

MAHAKAMA Kuu Masijala Ndogo Dar es Salaam leo inatarajiwa kuanza kusikiliza ushahidi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu. Kwa mujibu wa Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga katika kikao cha mahakama kilichopita, upande wa Jamhuri unatarajiwa kuwa…

DAR ES SALAAM. RAUNDI ya kwanza ya Ligi Kuu Bara imemalizika, huku Singida Black Stars ikiibuka kinara baada ya kuanza kampeni kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Fountain Gate nyumbani. Ushindi huo umeiweka Singida Black Stars kileleni mwa msimamo wa ligi, ukiipa mwanzo mzuri katika tofauti ya mabao, kitu ambacho…

DAR ES SALAAM: KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Goncalves, amekoshwa na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake akisema wataendelea kupambana kushinda na kulinda heshima ya rangi zake. Kauli hiyo inakuja baada ya Yanga kuibuka na ushindi mnono wa mabao 6-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulioch…

DAR ES SALAAM: LICHA ya Yanga SC kuwa na baadhi ya wachezaji majeruhi, ila mchambuzi maarufu wa michezo, Ansibert Rafael ‘Hans Rafael’ anaamini utendaji wa timu haujaathirika kwani kocha msaidizi Abdihamid Moalin amerejesha chachu benchi la ufundi. Mshambuliaji, Laurindo Depu na Clement Mzie ni majeruhi, beki Dickson …

RUVUMA; Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Wakili Mary Makondo, amezindua mradi wa MsingiTek unaolenga kujenga stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tatu. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika S…

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, ameiagiza Tume ya Ushindani (FCC) kuweka nguvu upya kuhusu udhibiti wa bidhaa bandia sokoni. – Pia ameitaka tume hiyo kuweka mifumo na njia bora za kupokea malalamiko kutoka kwa mlaji wa mwisho wa bidhaa au huduma ili kuongeza ufanisi na ulinzi. – Kapinga a…

TUTAENDELEA kumshangilia Pacome Zouzoua akiwa sehemu ya kikosi cha Ivory Coast kilichofuzu tena fainali za Kombe la Dunia, tangu mwaka 2014 iliposhiriki kwa mara ya mwisho Brazil. Ni miaka 11 imepita tangu taifa hilo kubwa kwenye mchezo wa mpira wa miguu Afrika kufuzu fainali za Kombe la Dunia lakini kwa Tanzania bado…

IRINGA: Wafanyabiashara 40 wa Soko la Mashine Tatu, mjini Iringa, waliopoteza bidhaa na mitaji kufuatia ajali ya moto, wamekabidhiwa hundi ya Sh Milioni 120 kama fidia kutoka Kampuni ya Bima ya Reliance Insurance kwa kushirikiana na Benki ya NMB. Hatua hiyo inalenga kuwasaidia kurejesha mitaji na kuendeleza biashara z…

IRINGA: WAKULIMA mkoani Iringa wamehimizwa kutumia mbegu bora na zilizoidhinishwa ili kuongeza tija na uzalishaji wa mazao, huku Serikali ikiimarisha mikakati ya kudhibiti mbegu bandia na kuwawezesha wakulima kupata pembejeo zenye ubora kwa wakati. Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za kuongeza uzalishaji wa…

PWANI: WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema uzinduzi wa mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) ni hatua muhimu katika kuongeza uwezo wa Tanzania kuzalisha umeme na kuifanya nchi kuwa kitovu cha biashara ya nishati katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini. Akizungumza leo katika uzinduzi wa mradi huo, N…

KATIKA kipindi hiki cha mwisho wa mwaka, kumekuwapo na ongezeko kubwa la wasafiri wa masafa marefu, hasa kwa mabasi wakienda kusherehekea sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya. Ni kipindi ambacho mahitaji ya vyombo vya usafiri huongezeka kiasi cha mamlaka kutoa usajili wa muda wa vibali vya usafirishaji kwa watu wanaotak…

SHINYANGA: Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, ameweka jiwe la msingi la jengo la vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Sekondari Kagongwa iliyopo Manispaa ya Kahama, mkoani Shinyanga. Ujenzi wa jengo hilo ulianza kwa nguvu za wananchi waliotoa mchango wa shilingi milioni saba, huku ukam…

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimedhamiria kuanzisha shamba la nyasi lenye ukubwa wa zaidi ya hekta 20,000 kwa ajili ya kulisha mifugo eneo la Makete. Mgombea mwenza wa urais kupitia CCM, Dk Emmanuel Nchimbi amesema hayo katika mikutano ya kampeni iliyofanyika Wanging’ombe na kwenye Viwanja vya Mabehewani mjini M…

KUTOKA mitaa ya Chicago hadi Ikulu ya Marekani, Michelle LaVaughn Robinson Obama ameendelea kuwa kielelezo cha mwanamke jasiri, mwenye maono na roho ya huduma kwa jamii.

DAR ES SALAAM; SHANGWE la ubingwa. Yanga wakishangilia baada ya kukabidhiwa kombe la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa mwaka 2025/26 kufuatia ushindi wa mabao 0-3 walioupata leo dhidi ya JKT Tanzania mchezo wa mwisho Ligi Kuu Tanzania Bara. Kutokana na ushindi wa mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Meja Jenerali…

ARUSHA; BARAZA la Mitihani la Taifa (NECTA) limesema limejipanga kutumia teknolojia ya Akili Mnemba (AI) kuboresha mifumo ya utahini na tathmini ya elimu nchini, likisisitiza kuwa Tanzania haiwezi kubaki nyuma wakati teknolojia hiyo ikiendelea kubadili sekta mbalimbali duniani. Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said M…

UMOJA wa Afrika (AU) imemthibitisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kuwa Kinara wa Afya ya Mama na Mtoto barani Afrika, kufuatia mafanikio makubwa ya kupunguza vifo vya kina mama na watoto kwa takribani asilimia 80.

DAR ES SALAAM – Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempendekeza Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia kujiuzulu kwa Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi. Pendekezo hilo limetolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro, katika mkutano na waandishi wa habari uliof…

MAKAMBAKO : MGOMBEA Mwenza wa Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema CCM ndicho chama pekee nchini kinachoweza kujivunia uzoefu wa kuongoza serikali na kuwaletea maendeleo wananchi kwa mafanikio makubwa.

DAR ES SALAAM; Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao Maalumu cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 26, 2026.

DODOMA: Tume ya Madini imewaonya wamiliki wa miradi ya uchimbaji mdogo wa madini yenye Mikataba ya Msaada wa Kiufundi (TSA) kuwa itachukua hatua za kisheria, ikiwemo kufuta ridhaa za Msaada wa Kiufundi, iwapo watashindwa kurekebisha mapungufu yaliyobainika ndani ya siku 30. Onyo hilo limekuja baada ya tume hiyo kukagu…

PWANI; Polisi mkoani Pwani inamshikilia dereva Josia Arute (34) mkazi wa Mlandizi, Kibaha kwa tuhuma za kugonga na kusababisha vifo vya askari wawili wa jeshi hilo. Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoa Pwani, Salim Morcase imeeleza kuwa askari hao walifariki dunia baada ya kugongwa na ga…

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imesema fedha za mtandaoni ni hatari. Gavana wa BoT Emmanuel Tutuba amesema fedha hizo hazitambuliki zina vihatarishi vingi kuliko faida na hazina njia za kuzidhibiti. Tutuba amesema hayo ofisini kwake Dodoma wakati wa mahojiano kwenye kipindi cha Kasri la Kikeke kilichorushwa na kituo cha …

DODOMA; Serikali imesema imeandaa Mkakati wa Kudumu Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi. Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Agosti 26, 2026 na Naibu EWaziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Kaspar Mmuya alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Asha Baraka aliyehoji lini serikali itaunda tume itakayotatua migo…
SHINYANGA: WATOTO wenye umri wa kuanzia miaka 0 hadi 10 mkoani Shinyanga wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya Polio ili kuwazuia kupata virusi vya ugonjwa huo nakuweza kuwaepusha na ulemavu wa kudumu au vifo. Hayo yamesemwa leo na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Yudas Ndungile alipokuwa akifungua kikao na waandishi wa…

MOROGORO: MBUNGE wa Jimbo la Mvomero, mkoani Morogoro, Sara Msafiri, amevitaka vikundi ambavyo vitashiriki kwenye tamasha la michezo kwenye jimbo hilo vitakuwa vya kijasiriamali na vitasaidiwa usajili ili vipate kunufaika na fursa ya mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri. Msafiri amesema hayo wakati akizind…

MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa utabiri wa msimu wa masika unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa Februari hadi Mei kwa maeneo yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka. Katika taarifa yake, TMA imetabiri matarajio ya mvua za wastani hadi juu ya wastani kwa maeneo mengi ya Pwani ya Kaskazini na baadhi ya maeneo ya …

DODOMA; Serikali imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Kilimo wa mwaka 2026 (The Agricultural Laws (Amendments) Act, 2026), ambao unapendekeza marekebisho katika Sheria Nne. Akiwasilisha muswada huo leo Agosti 27, 2027, Waziri wa Kilimo, Daniel Chongolo amezitaja sheria hizo kuwa ni, Sheri…

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema eneo la Kurasi Logistics Park linatarajiwa kuanza kutumika kama sehemu ya upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam (Port Extension) kuanzia Novemba mwaka huu, hatua inayolenga kupunguza msongamano bandarini na kuongeza ufanisi wa huduma za mizigo. Akizungumza…

DODOMA; Picha za matukio mbalimbali, wakati Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, akipokea rasmi leo Agosti 28, 2026 jina la Makamu wa Rais Mteule, Deogratius John Ndejembi, lililopendekezwa na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Jina hilo limewasilishwa kwa Spika na Katibu wa Rais, Balozi Ali Jabir Mwadini akiwa am…

MBEYA; Kaimu Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Tiba Asili na Tiba Mbadala ya Wizara ya Afya, DK Winfrida Kidima,amesema jamii bado ina uelewa tofauti kuhusu tiba asili, hivyo Wizara ya Afya inaendelea kutoa elimu kuhusu umuhimu wa huduma hizo, hasa katika kuboresha afya ya wananchi. Dk Kidima amesema hayo wakati aki…

ZANZIBAR: Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba, umeutaka Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kuendelea kuimarisha utoaji wa elimu kwa umma ili wananchi wawe na uelewa mpana kuhusu majukumu ya wakala na mchango wake katika kuhakikisha upatikanaji wa mafuta nchini. Makamba ametoa wito huo alipotembelea banda …

KAGERA: Serikali imezitaka shule nchini kuweka kipaumbele kwenye mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa wanafunzi wao ili kwenda sanjari na dunia ya sasa ya utandawazi na teknolojia inayokua kwa kasi. Serikali imeeleza kwa dunia ya sasa teknolojia inakwenda kwa kasi kubwa hivyo shule zinapaswa kuw…

GEITA; SERIKALI kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) imeanza kutekeleza mradi wa huduma ya intaneti ya bure kwenye maeneo ya wazi ikiwemo masoko na vituo vya afya mkoani Geita. Mkuu wa UCSAF Kanda ya Ziwa, Fredy Kandonga alieleza hayo wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya mawasiliano Mkoa wa…

DODOMA; Serikali imewasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Mikopo kwa Dhamana za Mali Zinazohamishika wa Mwaka 2026. Akiwasilisha bungeni muswada huo leo Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omatr, amesema lengo la kutunga Sheria ya Mikopo kwa Dhamana za Mali Zinazohamishika wa Mwaka 2026 ni kuweka masharti bora ya us…

DODOMA; Bunge limepitisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2026 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2026). Muswada huo uliwasliishwa bungeni leo Septemba 1, 2026 asubuhi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari, aliyesema mapendekezo ya marekebisho ya sheria 21 ni mion…
Habari nyingine
Utakuja AFCON 2027?
Viwanja Kenya · Tanzania · Uganda

Jifunze Kiswahili

Muswada wa Marekebisho Sheria mbalimbali wapitishwa

Marekebisho ya sheria kugusa sura ya jinai kwa watumishi

Fasili ya bangi yapendekezwa kujumuisha majani, mbegu
DODOMA; Serikali imewasilisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2026 (The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2026) ambap

Sheria 21 zapendekezwa kufanyiwa marekebisho

Rika la Erumeruasi lapewa pongezi ujenzi kituo cha afya

Wadau waweka mkakati Kukabiliana na biashara haramu

Akili unde kutumika kupima saratani ya matiti

Serikali yaombwa kuimarisha Chuo cha Ardhi Morogoro

Mbunge ahoji mkakati kuipa hadhi taaluma ya udereva

Jengo ESAMI kuongeza ufanisi mafunzo ya viongozi Afrika
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Juma Mkomi, amesema ujenzi wa jengo jipya la ghorofa tatu lenye thamani ya dola z

Mzee Masabala atunukiwa tuzo mchango wa elimu Kibeta

Mwenge wa Uhuru wazindua kituo janja cha maji Bukoba

Sheria ya ndoa inavyokwamisha ndoto za wasichana

Waganga walivyojisajili Baraza Tiba Asili na Tiba Mbadala

Banana Zoro: Sauti ya kipekee iliyotoka katika familia ya muziki

Akili unde kupima saratani ya matiti

Kanuni ya kikokotoo ni ya wanachama wote wenye sifa
DODOMA; Serikali imesema kanuni ya kikokotoo kwa wastaafu hutumika kwa wafanyakazi wote walioajiriwa sekta ya umma na binafsi. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mk

Muswada wa mikopo kwa mali zinazohamishika watua bungeni

Gharama upimaji kiwanja kimoja Sh 130,000
Importance of Peace for National Development
Spika wa Bunge la Tanzania, Mussa Zungu, amesema nchi haiwezi kujengwa kwa maandamano na kwamba amani ni jambo muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Akizungumza leo Juni 1, 2026 jijini Dodoma kuhusu umuhimu wa amani katika jamii, Msita amesema maendeleo yanapatikana katika mazingira yenye utulivu na mshikamano, akisisitiza kuwa sehemu yenye maendeleo ni sehemu inayompendeza Mungu.
Kihongosi amewataka wananchi kuendelea kulinda amani na mshikamano uliopo nchini, akisema Tanzania imeendelea kuwa mfano wa utulivu kutokana na umoja na upendo wa wananchi wake.
Kibadeni ameyasema hayo katika mahojiano maalumu, akisisitiza umuhimu wa vijana kutumia vyema nafasi wanazopewa na kushirikiana katika kulinda amani, akibainisha kuwa ustawi wa taifa lolote unategemea uwepo wa amani.
He called on Christians and the wider community to embrace forgiveness, love and peace as essential pillars for building a united and harmonious society.
Ameeleza kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo ya Taifa, na kusisitiza kuwa bila amani, jitihada zote za maendeleo haziwezi kufikiwa.
Amani ni zawadi kutoka kwa Mungu na ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa. "Mungu ameturuzuku amani, ni kipaji na kipawa. Tuna kila sababu ya kuitunza na kuilinda, kwani bila amani hakuna maendeleo, wananchi hawatakuwa salama, na tutakimbia nchi yetu wenyewe," amesisitiza.
Amesisitiza kuwa Tanzania ni kivutio cha wivu kwa watu wa mataifa mengine, kutokana na amani na utulivu iliyonayo.
Kuhani Baraka pia amewakumbusha waumini na wananchi wote kudumisha amani wakati wa uchaguzi, akisema amani ni nguzo ya maendeleo na msingi wa haki.
Alisema unaweza kudai vitu vyote kama vile barabara za lami, maji, hospital, katiba mpya, mishara mikubwa lakini kukiwa hakuna amani huwezi kuvitumia vitu vyote hivyo kwa kuwa watu watasambatika huko na kule kwa machafuko ya vita.
Tanzania Fuel Prices Surge Over 30% Due to Middle East Conflict
In April 2026, Tanzanian fuel prices soared over 30 per cent in one month due to the Middle East conflict, despite government assurances of adequate reserves.
The Tanzania Revenue Authority (TRA) has introduced a new billing number system for the loading and offloading of fuel at storage depots, aimed at enhancing transparency, boosting government revenue collection and ensuring compliance without disrupting supply.
Nchi kama Saudi Arabia, UAE, Kuwait, Qatar na Iraq zinapoteza njia yao kuu ya kuuza mafuta.
wanunuaji wa mafuta kwa bei ra rejareja yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam watalazimika kuongeza Sh956 katika kila lita moja ya mafuta baada ya bei kufikia Sh3,820 kutoka Sh2864. Kwa upande wa dizeli, lita moja sasa watanunua kwa Sh3,806 kutoka Sh2,858 ikiwa ni ongezeko la Sh948. Kwa upande wa mafuta ya taa, sasa yatanunuliwa kwa Sh3,684 kutoka Sh2,932 iliyokuwa ikitumika Machi mwaka huu ikiwa ni ongezeko la Sh752.
Ongezeko la bei ya mafuta halipo Tanzania pekee, bali hata katika soko la dunia ambapo bei kikomo kwa Aprili 2026, zimeongezeka kwa asilimia 69.98 kwa mafuta ya petroli, asilimia 114.46 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 120.81 kwa mafuta ya taa.
wanunuaji wa mafuta kwa bei ra rejareja yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam watalazimika kuongeza Sh956 katika kila lita moja ya mafuta baada ya bei kufikia Sh3,820 kutoka Sh2864.
Kwa mujibu wa Ewura, ongezeko hilo la bei za mafuta ni janga la kidunia na Tanzania kama sehemu hiyo inachukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa upatikanaji wa mafuta nchini na katika bei himilivu ili kupunguza madhara ya kiuchumi na kijamii.
Kufungwa kwa mlango huu muhimu wa bahari kunasababisha athari kubwa kimataifa, hasa kiuchumi na kiusalama: 1️⃣ Kupanda kwa bei ya mafuta duniani
Kufungwa kwake kunasababisha uhaba wa mafuta sokoni. Bei ya mafuta na gesi inapanda haraka, na kuathiri gharama za usafiri, umeme na bidhaa nyingine.
Kufungwa kunaweza kusababisha mvutano au mapambano kati ya mataifa yenye maslahi ya kiuchumi na kiusalama katika eneo hilo.
Tumeona bei zimeshaanza kupanda, tutakaa ndani ya Serikali kuhakikisha tunakabiliana nalo vipi suala hili ili wananchi waendelee kupata mafuta kwa bei nzuri na kudhibiti kupanda kwa gharama za maisha.
Dk Mwigulu amesema: “Tumeona bei zimeshaanza kupanda, tutakaa ndani ya Serikali kuhakikisha tunakabiliana nalo vipi suala hili ili wananchi waendelee kupata mafuta kwa bei nzuri na kudhibiti kupanda kwa gharama za maisha.”
Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa ghala la kupokea na kuhifadhi mafuta lenye uwezo wa kupokea tani 308,110 katika Bandari ya Dar es Salaam ambao umefikia asilimia 30.
The authority attributed the rise to the ongoing geopolitical tensions in the Middle East, particularly involving the United States, Israel and Iran, which began on February 28, 2026, and have significantly disrupted global oil supply.
Wakati huohuo, athari za vita hivyo zimeanza kuhisiwa na wananchi wa Marekani, ambapo bei ya mafuta imeendelea kupanda na kufikia zaidi ya dola 4 kwa galoni, kiwango cha juu zaidi tangu mwaka 2022.
Hali hiyo inachangiwa na usumbufu katika eneo la Strait of Hormuz, ambalo ni njia muhimu inayopitisha takriban robo ya mafuta yanayotumika duniani.
TANZANIA INA MAFUTA YA KUTOSHA,LICHA YA BEI KUPANDA KUTOKANA NA VITA YA MASHARIKI YA KATI
Kwa mwezi Aprili 2026, gharama za kuagiza mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es Salaam zimeongezeka kwa wastani wa asilimia 15.3 kwa mafuta ya petroli na asilimia 10.8 kwa mafuta ya dizeli na hakuna mabadiliko ya gharama kwa mafuta ya taa.
Mabadiliko ya bei za mafuta nchini kwa mwezi Aprili 2026 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na vita inayoendelea Mashariki ya kati tarehe 28 Februari 2026.
In his final political move, Bungara announced his resignation from ACT Wazalendo on February 18, 2026. He formally joined CHADEMA, the nation’s largest opposition party, aligning himself with their boycott of elections they deemed fundamentally unfair.
The Court of Appeal here began hearing a critical revision application from the main opposition party, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) on Tuesday, which seeks to overturn a High Court injunction that has barred it from conducting any political activities since June 2025.
Hatima ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuendelea kuzuiwa kufanya shughuli za kisiasa au kurejea ulingoni sasa ipo mikononi mwa Mahakama ya Rufaa, baada ya zaidi ya siku 283 tangu kilipowekewa zuio hilo.
Most remarkably, just one week before his death, Bungara launched an operation to strengthen CHADEMA in the southern regions.
Most remarkably, just one week before his death, Bungara launched an operation to strengthen CHADEMA in the southern regions. He donated his personal vehicle and fuel to party organisers and handed over resources to young CHADEMA activists, resulting in thousands of people switching from other parties to join CHADEMA within that single week.
Mgawanyiko huo umejidhihirisha kupitia makundi mawili yenye mitazamo tofauti kuhusu mustakabali wa chama.
Sifuna alisisitiza kuwa yuko tayari kusimama imara kulinda misingi ya chama, akipinga kile alichodai ni juhudi za kukisogeza karibu na mamlaka ya serikali.
Gachagua ameanza kujijenga kama sauti mbadala ya kisiasa, hasa kwa vijana, akishambulia sera za serikali kwa madai ya kushindwa kuboresha maisha ya wananchi wa kawaida.
Kutokuwepo kwake katika mstari wa mbele wa siasa za uchaguzi wa 2027 kumeacha pengo ambalo sasa linajazwa na makundi yenye mitazamo tofauti.
All Parliamentary Standing Committee meetings have been suspended today, March 25, 2026, following the death of Isimani MP and Minister of State in the Prime Minister’s Office, William Lukuvi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema taifa limepoteza kiongozi shupavu, mahiri na mzalendo kufuatia kifo cha William Vangimembe Lukuvi.
William Lukuvi afariki dunia kwa mshituko wa moyo
PRESIDENT Samia Suluhu Hassan has announced the death of the former Minister of State in the Prime Minister’s Office, (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities) William Lukuvi, who passed away this morning, March 25, 2026.
Mbunge wa Isiman, William Lukuvi amefariki dunia, huku aliyekuwa mshindani wake katika mchakato wa ndani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa ubunge wa Isimani, Festo Kiswaga, akifunguka mambo atakayoyakumbuka.
Kiswaga, amesema anamkumbuka kiongozi huyo kwa utendaji wake Isimani, kwani aliingia likiwa jipya na halikuwa na hata shule moja ya sekondari, lakini sasa zimefika zaidi ya 10.
Taarifa ya kifo chake imetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kisuluka, akimnukuu Rais Samia Suluhu Hassan, aliyesema amesikitishwa na anatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki.
Ambassador Kusiluka conveyed condolences from President Samia Suluhu Hassan, who announced the death and sent her sympathies to the people of Isimani and to the Speaker of the National Assembly.
Kifo hicho kimetangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka juu ya msiba huo wa Lukuvi aliyezaliwa Agosti 15, 1955.
Additionally, the Head of State extended her condolences to the Speaker of Parliament, the bereaved family, residents of Isimani Constituency, and all Tanzanians mourning the loss.
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani William Vangimembe Lukuvi amefariki duinia akiwa na umri wa miaka 70.
Lema ametumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kuzungumzia kifo cha Lukuvi akisema: “Tunazaliwa bila kitu, na tunaondoka bila kitu, kifo hutukumbusha unyenyekevu wa maisha.
According to a statement issued by the Parliament’s Communications and Public Relations Unit, Mr Zungu invoked Rule 176 of the Standing Orders of the National Assembly (August 2025 edition) to suspend the sittings.
Reports of the death of the Isimani Constituency MP in Iringa Region, who had served in Parliament since 1995, began circulating earlier in the day before being confirmed by the Chief Secretary, Ambassador Dr Moses Kusiluka.
Mr Lukuvi’s death brings to three the number of MPs who have died during the 13th Parliament since its inauguration by President Hassan.
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mussa Azzan Zungu leo Machi 25, 2026, ameongoza kikao cha dharura cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uongozi kilichofanyika katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma, kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Ismani, William Vangimembe Lukuvi.
Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, ametoa salamu za pole kufuatia kifo cha William Vangimembe Lukuvi kilichotokea leo Machi 25, 2026.
Rais Mwinyi amesema taifa limepoteza kiongozi muhimu ambaye amelitumikia kwa uadilifu na kujitolea katika nafasi mbalimbali za uongozi kwa muda mrefu.
WAZIRI LUKUVI AFARIKI DUNIA
William Vangimembe Lukuvi ambaye amefariki leo Machi 25, 2026 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania aliyetoa mchango mkubwa katika siasa za kitaifa.
William Vangimembe Lukuvi ambaye amefariki leo Machi 25, 2026 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania aliyetoa mchango mkubwa katika siasa za kitaifa. Ametumikia nafasi mbalimbali za uongozi serikalini na kujijengea sifa ya uongozi thabiti kupitia utumishi wa muda mrefu serikalini na uwakilishi wake bungeni.
Mpina ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi akizungumza na Mwananchi amesimulia sababu iliyotaka kumfanya kuikataa bajeti hiyo, kwamba Mpango wa Maendeleo ulikuwa unaeleza Serikali itatenga asilimia 35 ya bajeti kutelekezwa kwenye maendeleo lakini yenyewe ikatenga asilimia 22.
Mdee amesema Lukuvi alikuwa akichukua ushauri na mapendekezo ya hotuba za kambi ya upinzani bungeni na kwenda kuvifanyia kazi kwa vitendo.
William Lukuvi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) akiagwa bungeni Dodoma.
Speaker of the National Assembly, Mussa Zungu, has described the death of Minister of State in the Prime Minister’s Office (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities) and Isimani MP William Lukuvi as a major blow not only to his family, but also to the Parliament, government, and Tanzanians at large.
PRIME Minister Mwigulu Nchemba has paid glowing tribute to the late William Lukuvi, saying he has long benefited from the veteran politician’s wisdom, guidance and selfless dedication to public service, especially since his first appointment as Deputy Minister for Finance.
President Samia Suluhu Hassan is expected to join thousands of mourners in Iringa next Tuesday to honour the late Minister of State in the Prime Minister’s Office (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities), who passed away on Wednesday at Benjamin Mkapa Hospital in Dodoma Region.
DODOMA: PRIME Minister Mwigulu Nchemba has paid glowing tribute to the late William Lukuvi, saying he has long benefited from the veteran politician’s wisdom, guidance and selfless dedication to public service, especially since his first appointment as Deputy Minister for Finance.