
Gundua
1087 habariHabari mpya, uchambuzi wa kina, na maarifa kutoka Nukta
Unaona habari zinazohusishwa na Gazetini chini (pamoja na mengine ya Gundua).


KINSHASA, DRC KUNDI la waasi la M23 linajivunia idadi ndogo ya maambukizi ya Ebola katika maeneo yake, likidai kuwa hilo linathibitisha uwezo wake mkubwa wa kuongoza. M23 wanashikilia maeneo mengi ya Kaskazini na Kusini mwa majimbo ya Kivu, pia operesheni yao ya mwaka 2025 ikiwapatia miji mikubwa miwili ya Mashariki, …

WASHINGTON DC, Marekani BEI ya mafuta katika soko la dunia imeshuka kwa asilimia 9, yakiwa ni matokeo ya mashambulizi ya Marekani na Iran kusimamia kwa siku mbili. Kwa sasa, bei ya pipa moja la mafuta ghafi imefikia Dola za Marekani 88, tofauti na zaidi ya Dola 100 wiki iliyopita. Hatua hiyo inakuja baada ya balozi […]

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amezitaka kujiandaa na kibano nchi zitakazoipa ushirikiano Iran. Kauli hiyo ni mwendelezo wa uhusiano mbaya uliopo kati ya mataifa mawili hayo. Katika taarifa yake kupitia mtandao wa kijamii wa Truth Social, Rais Trump amesema Iran imeshindwa kutumia ‘fursa’ ya k…

JERUSALEM, Israel WAZIRI Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amesema wamkataa ombi la Rais wa Marekani, Donald Trump, kuhusu mgogoro wa Gaza. Kwa mujibu wa Netanyahu, hawakubaliani na ombi la Trump kutaka Israel iondoshe wanajeshi wake katika Ukanda huo. Katika maelezo yake, Netanyahu amesisitiza kuwa wanajeshi wa Isr…

LONDON, Uingereza RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, amewasili nchini Uingereza, ambako atakutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu mpya, Andy Burnham. Zelensky atakuwa mgeni wa kwanza wa nje kufika Uingereza tangu Burnham alipoingia madarakani siku chache zilizopita. Burnham ameahidi kuwa Uingereza itaendelea ku…

NYON, Uswis WACHEZAJI wapatao sita wa timu ya soka ya Taifa ya Argentina huenda wakafungiwa kushiriki fainali zijazo za Kombe la Dunia za mwaka 2030. Kwa mujibu wa Gazeti la Sun, nyota walio hatarini kushukiwa na rungu hilo ni Nahuel Molina, Leandro Paredes, Thiago Almada, Cristian Romero, Lisandro Martinez na Giovani…

Na Ramadhan Hassan, Gazetini-Dodoma WAZIRI wa Fedha, Khamis Mussa Omar, amesema Serikali itaendelea kutegemea mapato ya ndani kama chanzo kikuu cha kugharamia matumizi ya kawaida na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, huku ikiweka mkazo katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato hayo ili kuharakisha maendeleo ya taifa. Ak…

MEXICO CITY, Mexico FAINALI za Kombe la Dunia za mwaka huu (2026) zinaendelea kuchanja mbuga, huku baadhi ya timu zikiwa zimeshatinga hatua ya 16 Bora. Baadhi ya mechi kali za hatua hiyo ni ile itakayozikutanisha England ‘Three Lions’ na Mexico ‘El Tri’, ambao ni wenyeji wa michuano kwa kushirikiana na Marekani na Can…

TORONTO, Canada HAKUNA mbabe. Ni dakika 90 za mchezo wa Kundi B uliochezwa Juni 12, 2026, ambapo wenyeji wa michuano ya mwaka huu ya Kombe la Dunia, Canada, wametoka sare ya bao 1-1 na Bosnia. Bosnia walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 21 kupitia kwa Jovo Lukic aliyeunganisha kwa kichwa mpira wa kona, kabla […]

TORONTO, Canada KIUNGO Thomas Partey atakosekana wakati timu ya Taifa ya Ghana itakapocheza mechi ya kwanza ya msimu huu wa Kombe la Dunia. Ni baada ya mamlaka za Canada, moja ya wenyeji watatu wa michuano hiyo, kumnyima kibali cha kuingia nchini humo. Hatua hiyo imetokana na kesi tano za ubakaji zinazomkabili nyota h…

Na mwandishi wetu, Gazetini SERIKALI imepanga kuondoa matumizi ya vocha za kukwangua za muda wa maongezi katika maeneo ya mijini kuanzia Julai 1, 2026, hatua inayolenga kuharakisha matumizi ya mifumo ya kidijitali katika sekta ya mawasiliano na huduma za kifedha. hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha, Khamis Mussa Oma…

SEOUL, Korea Kusini MATAIFA 48 ndani ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika kuanzia Juni 11 – Julai 19, 2026 huko Marekani, Mexico na Canada. Kuelekea michuano hiyo, hawa ndiyo wachezaji 26 walioitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Korea ya Kusini. Makipa: Hyeon-Woo Jo (Ulsan), Seung-Gyu Kim (FC Tokyo), na Bu…

Berlin, Ujerumani MATAIFA 48 ndani ya fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika kuanzia Juni 11 – Julai 19, 2026 huko Marekani, Mexico na Canada. Kuelekea michuano hiyo, hawa ndiyo wachezaji 26 walioitwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Ujerumani. Makipa: Oliver Baumann (Hoffenheim), Manuel Neuer (Bayern Munich), na…

BAGHDAD, Iraq MOJA ya vivutio vya fainali za Kombe la Dunia za mwaka huu zitakazoanza Juni 11, 2026 ni uwepo wa timu ya soka ya Taifa ya Iraq iliyofuzu kwa kuifunga Bolivia. Hii inakuwa mara ya pili kwao kushiriki baada ya mwaka 1986. Katika mashindano hayo, Iraq iliishia hatua ya makundi kwa kupoteza mechi zote […]

MEXICO CITY, Mexico KOCHA wa timu ya soka ya Taifa ya Brazil, Carlo Ancelotti, amethibitisha kuwa mshambuliaji wake, Neymar, anaweza kuwa fiti kuivaa Scotland katika mchezo wa Jumatano ya wiki ijayo. Neymar anayekipiga Santos ya Ligi Kuu ya Brazil, alikosekana katika mechi zote mbili za awali msimu huu wa Kombe la Dun…

Na mwandishi wetu, Gazetini MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Lazaro Twange, amewaondoa hofu wananchi kuhusu matumizi ya nishati ya umeme katika vyombo vya usafiri, akisema kuwa Tanesco imejipanga kujenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima. Mkurugenzi huyo amesema hayo Juni 19, 2026, …

Na mwandishi wetu, Gazetini WANANCHI wa Wilaya za Gairo, Mpwapwa, Kongwa, Chamwino na Kiteto wanatarajiwa kunufaika na huduma ya umeme wa uhakika zaidi kufuatia kukamilika kwa miradi ya kuimarisha mfumo wa usambazaji wa umeme iliyotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa gharama ya zaidi ya Sh bilioni 10.5…

LONDON, Uingereza KAMA ilivyo kawaida, katika kila msimu mpya wa Ligi Kuu ya England (EPL), huwa kuna timu tatu zilizopanda daraja. Safari hii (2026-27), ni Coventry City, Hull City na Ipswich Town. Je, zitakaza na kufanya maajabu EPL msimu ujao wa 2026-27 au zitarudi zilikotoka, kwa maana ya Daraja la Kwanza (Champio…

LOS ANGELES, Marekani TIMU ya soka ya Taifa ya Marekani imeanza na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Paraguay katika mechi ya Kundi D msimu huu wa fainali za Kombe la Dunia. Wakati huo huo, bao la dakika ya saba walilopata Marekani ni la mapema zaidi kwa timu mwenyeji tangu Ujerumani ilipofunga mwaka 2006. Mechi […]

Na mwandishi wetu, Gazetini WAKATI dunia ikiwa kwenye sintofahamu juu ya mustakabali wa vita vya Marekani na Iran, Kundi la kigaidi la Houthi nchini Yemen limeendelea kufanya mambo yawe mengi na magumu zaidi. Iko hivi; Marekani na Iran zinaendelea kushambuliana na mgogoro wao juu ya Mlango-Bahari wa Hormuz imesababish…

Na mwandishi wetu, Gazetini SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi ya OpenMap Development Tanzania (OMDTZ) imechukua hatua mpya za kuimarisha utayari wa jamii kukabiliana na mafuriko katika Jiji la Dar es Salaam kwa kuthibitisha mipango ya kujiandaa na kukabiliana na maafa katika kata tano z…

Na Ramadhan Hassan, Gazetini NAIBU Waziri wa Fedha, Mshamu Ali Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar, ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki Mkutano wa Pamoja wa 9 wa Kamati Maalum ya Mawaziri wa Umoja wa Afrika (STC) unaojadili masuala ya Fedha, Uchumi, Mipango na Mtangamano pamoja na Mkutano …

MIAMI, Marekani AKITOKEA benchi, aliukuta mchezo ukiwa sare ya bao 1-1, kisha akafunga na kuiwezesha timu ya soka ya Taifa ya Ureno kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Croatia, matokeo yaliyowapeleka hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia. Huyo si Cristiano Ronaldo wala Bruno Fernandes, bali ni Goncalo Ramos, akifanya hi…

Na mwandishi wetu, Gazetini RAIS wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania, Wakili Boniventure Mwambaja, amesema anaiona Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kuwa ni miongoni mwa taasisi bora za maendeleo ya miundombinu barani Afrika kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwake mwa…

Na mwandishi wetu, Gazetini KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Richard Abwao, amefariki dunia leo Juni 20, 2026 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam. Kifo cha ofisa huyo kimethibitishwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini,…

Na Ramadhan Hassan, Dodoma HOSPITALI ya Benjamin Mkapa (BMH), kwa kushirikiana na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), imeandika historia kwa kufanikisha kwa mara ya kwanza kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto kutoka Burundi, hatua inayoimarisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha huduma za kibingwa na ubingw…

MIAMI, Marekani JUMAPILI ya wiki hii, Julai 19, 2026, nyasi za Uwanja wa MetLife nchini Marekani zitawaka moto kwa mchezo wa fainali ya msimu huu wa Kombe la Dunia. Argentina dhidi ya Hispania. Ni fainali ya wababe tupu. Argentina ni bingwa mtetezi wa Kombe la Dunia na Copa America, wakati Hispania wanashikilia taji l…

Na Hassan Mwasha DAKIKA 90 tu za mchezo kati ya Fountain Gate na Singida Black Stars ndizo zilizopeperusha ndoto ya Feisal Salum ‘Fei Toto’ kuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2025-26. Kabla ya mechi za mwisho wa msimu kuchezwa jana Juni 30, 2026, Fei Toto wa Azam ndiye aliyekuwa kinara kwa mabao […]

MEXICO CITY, Mexico KOCHA wa timu ya soka ya Taifa ya Argentina, Lionel Scaloni, amethibitisha kuwa atampumzisha nahodha wake, Lionel Messi, katika mchezo wao dhidi ya Jordan. Timu hizo zitakutana kesho Juni 28, 2026, ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kundi lao lenye timu zingine mbili, Algeria na Austria. Argentina ikiwa …

MIAMI, Marekani MECHI za hatua ya 32 Bora msimu huu wa Kombe la Dunia zitaanza kuchezwa usiku wa leo Juni 28, 2026. Colombia baada ya kulazimisha suluhu dhidi ya Ureno, imetinga hatua hiyo ikitokea Kundi K. DRC nayo imeingia baada ya ushindi wake dhidi ya Uzbekistan, kama ilivyo kwa Croatia iliyoifunga Ghana mabao 2-1…

Na Hassan Mwasha, Gazetini ACHANA na ishu ya ubingwa. Ni wazi si Yanga wala Simba inayoweza kufikia idadi ya pointi ilizokusanya msimu uliopita (2024-25) wa Ligi Kuu Bara. Kwa sasa, Yanga iko kileleni mwa msimamo lakini imekusanya pointi 72, wakati Simba wao wana pointi 70, huku kila timu ikiwa imebakiza mechi moja ba…

Na Imani Nathaniel, Gazetini Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Bui Van Thang, ametembelea banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), akijionea huduma mbalimbali za kisasa na suluhisho za kidijitali zinazotolewa kwa Watanzania. Katika ziara hiyo iliyofanyik…

MIAMI, Marekani WENYEJI wa fainali za Kombe la Dunia za mwaka huu, Canada, ambao wanashirikiana na Mexico na Marekani, watakwana na Morocco katika hatua inayofuata ya 16 Bora. Canada chini ya ocha Jesse Marsch, walivuka hatua iliyopita (32 Bora) kwa kuitoa timu nyingine ya Afrika, Afrika Kusini. Bao pekee la mchezo hu…

Na mwandishi wetu, Gazetini Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, George Masaju, ameshauri Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kuendelea kufanya ukaguzi wa mifumo ya usalama na afya katika maeneo ya kazi nchini yakiwemo majengo ya Mahakama kwa mujibu wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura Na. 297, …

Na mwandishi wetu, Gazetini Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dk. Jim Yonazi, amesema maandalizi ya Michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) 2027 yanapaswa kuangaliwa zaidi ya mpira wa miguu, akieleza kuwa ni fursa ya kipekee ya kuitangaza Tanzania kimataifa, kukuza utalii, …

Na mwandishi wetu, Gazetini Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche, amewataka wanachama wa chama hicho kuongeza kiwango cha kujitolea katika harakati za kisiasa, akisema kufanya hivyo kutawapa nguvu viongozi na wanachama wanaobeba gharama kubwa za kupigania mabadiliko nchini. Akiz…

Na Hassan Mwasha, Gazetini HIVI karibuni, Yanga iliachana na mshambuliaji wake raia wa Zimbabwe, Prince Dube, ambaye amejiunga na Hardrock ya Ligi Kuu nchini humo. Amerudi nyumbani. Kwamba nyota huyo amehitimisha safari ya miaka sita ya kucheza Ligi Kuu Bara, tangu aliposajiliwa na Azam mwaka 2020 akitokea Highlanders…

ZEIST, Uholanzi KIUNGO na kocha wa zamani wa Barcelona, Xavi Hernandez, ndiye aliyekabidhiwa benchi la ufundi kwa ajili ya kuinoa timu ya soka ya Taifa ya Uholanzi ‘Oranje’. Xavi ana historia ndefu na Waholanzi. Kocha wa zamani wa Uholanzi, Louis van Gaal, ndiye aliyeibua kipaji chake kwa kumpa nafasi katika kikosi ch…

Na mwandishi wetu, Gazetini BANDARI ya Dar es Salaam imeibuka kinara wa ufanisi wa huduma za bandari katika ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kupanda kwa nafasi 105 katika Ripoti ya Ufanisi wa Bandari Duniani (Container Port Performance Index – CPPI) ya mwaka 2025, hatua inayodhihirisha mafanikio ya mageuzi makubwa …

MEXICO CITY, Mexico UWANJA wa Azteca unaopatikana Kusini mwa Mji Mkuu wa Mexico, Mexico City. Ni moja ya viwanja vya soka vyenye historia ya aina yake. Baada ya Mexico kushinda zabuni ya kuandaa Kombe la Dunia mwaka 1970, muhandisi Pedro Ramirez Vazquez alipewa jukumu la kujenga uwanja wenye uwezo wa kupokea mashabiki…

TEHRAN, Iran JESHI la Marekani limetibitisha kufanya shambulizi la usiku kwa mara ya saba mfululizo nchini Iran. Huo ni mwendelezo wa Iran kushambuliwa usiku tangu Rais Donald Trump alipotangaza kuwa hakuna tena usitishaji wa vita. Katika taarifa yake baada ya shambulizi la usiku wa kuamkia leo Julai 18, 2026, Marekan…

MIAMI, Marekani TIMU ya soka ya Taifa ya Ufaransa imetinga robo fainali ya Kombe la Dunia baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Paraguay. Ni katika mchezo wa hatua ya 32 Bora, ambapo bao pekee la Ufaransa lilifungwa na Kylian Mbappe kwa mkwaju wa penalti. Kwa matokeo hayo, Ufaransa sasa itakwaana na vigogo wa […]

BOSTON, Marekani FAINALI za Kombe la Dunia za mwaka huu (2026) zilizochezwa kwa siku 39, kwenye viwanja 16, zikishirikisha wachezaji 1,039 kutoka timu 48, zilishuhudia mabao 308 yakifungwa katika mechi 104. Je, ni nani aliyeongoza kwa mabao, asisti? Ni timu zipo zilizofunga na kuruhusu mabao mengi? Makala fupi haya ya…

Na mwandishi wetu, Gazetini Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeanzisha utaratibu wa kutoa ithibati ya uanachama wa maisha kwa waandishi wa habari waliokuwa na umri wa miaka 50 au zaidi mwaka 2016, hatua inayolenga kutambua mchango wa wanahabari wakongwe waliotumikia taaluma hiyo kwa muda mrefu na wanaoki…

TEHRAN, Iran Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limetangaza kuwa Mlango Bahari wa Hormuz hautafunguliwa kikamilifu ikiwa vitisho vya kijeshi na kauli za uchokozi kutoka Marekani vitaendelea, likionya kuwa hali ya usalama katika eneo hilo bado ni tete. Kwa mujibu wa shirika la habari la serikali y…

Na mwandishi wetu, Gazetni VIJANA wa Tanzania wametajwa kuwa kundi litakalobeba mafanikio makubwa ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, huku wakihimizwa kuanza kujijengea uwezo na kutumia fursa zinazotengenezwa kupitia mipango ya maendeleo ya Serikali. Mchumi kutoka Tume ya Taifa ya Mipango, Alpha Temu, ameiambia Gazeti…

MIAMI, Marekani LICHA ya kucheza mechi zaidi ya 200 akiwa na timu ya Taifa ya Argentina, Lionel Messi hajawahi kuikabili England. Safari hii, Messi atakutana kwa mara ya kwanza na ‘Three Lions’ katika mchezo wa nusu fainali ya msimu huu wa Kombe la Dunia. Argentina ya Messi imeingia nusu fainali baada ya ushindi wake …

Na Hassan Mwasha, Gazetini BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jumatatu, Mei 18, 2026 limepitisha Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa Mwaka Mpya wa Fedha 2026-27 Bungeni mjini Dodoma iliyowasilishwa Ijumaa Mei 15, 2026 na Waziri wa wizara hiyo, Dk. Ashatu Kijaji, Mei 15, 2026, amewasilisha Katika hotuba y…

MIAMI, Marekani SAHAU kabisa kuhusu matokeo. Fainali ya Kombe la Dunia iliyochezwa jana iliwakutanisha makocha wawili, Luis de la Fuente wa Hispania na Lionel Scaloni anayeinoa Argentina. Ukiweka kando ubora wa mbinu na mafanikio yao, kuna stori nyingine ya kufurahisha kuhusu wawili hao. Stori yao hiyo inaanzia mwaka …

-Yaiwezesha Serikali kupata thamani halisi ya fedha-Wadau ununuzi wa umma 2,600 wafikiwa mafunzo matumizi ya moduli Na Mwandishi wetu, Gazetini Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imefanikiwa kushughulikia rufaa 58 kati ya rufaa 60 zilizowasilishwa katika mwaka wa fedha 2025/26 na kuzitolea uamuzi kwa wakati na…

HAVANA, Cuba KWA miaka mingi, Cuba imekuwa ikisifika kwa ubora wa sekta yake ya afya, huku raia wake wakifurahia huduma ya matibabu bila malipo kwa Serikali kubeba gharama zote. Hata hivyo, kwa sasa mambo yamebadilika na sekta ya afya nchini Cuba iko hoi, au ‘ICU’, kama unavyoweza kuifananisha na mgonjwa anayehitaji u…

Na Ramadhan Hassan, Gazetini-Dodoma WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali itaendelea kuhakikisha hakuna mtoto anayekosa haki ya kupata elimu, ikiwemo mabinti waliopata ujauzito, kama sehemu ya juhudi za kuimarisha usawa na ujumuishi katika sekta ya elimu nchini. Prof. Mkenda amet…

WASHINGRON, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema Marekani inaweza kuanzisha mashambulizi mengine makubwa dhidi ya Iran, akidai kuwa operesheni za kijeshi zilizofanyika usiku uliopita zilikuwa na athari kubwa. Akizungumza na wanahabari alipokuwa akihudhuria mkutano wa NATO, Trump amesema: “Tuliwashambulia s…

Na Hassan Mwasha, Gazetini NI mwanamuziki? Ndiyo. Hiyo ndiyo sura yake ya kwanza iliyomtambulisha Baba Levo mbele ya walio wengi. Achana na maisha binafsi, ambayo ndugu, jamaa na marafiki zake wanaweza kuwa na simulizi yake nyingine. Kwa walio wengi, Clayton Revocatus Chipando aliwahi kuingia na kuishi kwenye orodha y…

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro JESHI la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro limeeleza kuwa limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 188 wa makosa mbalimbali ya jinai, huku mmoja akihukumiwa kunyongwa hadi kufa na mwingine akipewa kifungo cha maisha jela kwa makosa ya mauaji. Hatua hiyo imefikiwa kufuatia operesheni mbalimbali za kiu…

KINSHASA, DRC WATU zaidi ya 1,000 wameshapoteza maisha ndani ya miezi miwili ya ugonjwa wa Ebola nchini DRC, idadi kubwa zaidi, ikilinganishwa na mlipuko wa mwaka 2014 na 2016. Katika ripoti ya Wizara ya Afya ya DRC, visa 2,536 na vifo 1,033 vimejitokeza tangu maambukizi ya Ebola y’all kuripotiwa Mei 15, 2026. Ni tofa…

MIAMI, Marekani ANAITWA Slavko Vincic, mwamuzi wa kati aliyeteuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kucheza mechi ya fainali msimu huu wa Kombe la Dunia (2026). Mchezo wa Julai 19, 2026, utakaozikutanisha Argentina na Hispania katika Uwanja wa MetLife nchini Marekani. Vincic (46), anakuwa mwamuzi wa kati wa …

Na mwandishi wetu, Gazetini TANGU Nasreddine Nabi alipoondoka mwaka 2023, kibarua cha benchi la ufundi la Yanga kimekuwa kigumu kwa kila kocha aliyeingia klabuni hapo. Kwa ufupi, makocha sita wameingia na kutoka Jangwani tangu Nabi alipoiachia Yanga mafanikio makubwa ya kufika fainali ya Kombe la Shirikisho barani Afr…

MIAMI, Argentina ARGENTINA ya kocha Lionel Scaloni itaingia katika mchezo huo wa fainali dhidi ya Hispania ikiwa bingwa mtetezi kwa taji lake la miaka minne iliyopita nchini Qatar. Vijana hao wa Kusini mwa Amerika wanasaka rekodi ya kuwa timu ya pili kutetea ubingwa wa Kombe la Dunia baada ya Brazil kufanya hivyo mwak…

BOSTON, Marekani MSIMU huu wa fainali za Kombe la Dunia umekuwa wa mafanikio makubwa kwa mshambuliaji wa timu ya soka ya Taifa ya Ufaransa, Kylian Mbappe. Si tu Ufaransa yake imetinga hatua ya nusu fainali, bali pia ameshafunga mabao nane kati ya 16 ya timu hiyo. Wakati huo huo, nyota huyo wa Real Madrid ameweka […]

OSLO, Norway SHIRIKISHO la Soka la Norway (NFF) limetangaza nia yake ya kumshitaki Rais Donald Trump kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). Norway wanapeleka barua yao kwa FIFA wakilalamikia Rais Trump kuingilia adhabu ya kadi nyekundu ya mshambuliaji wa timu ya soka ya Taifa ya Marekani, Folarin Balogun, wakati …

BOSTON, Marekani KICHAPO cha mabao 2-1 kutoka kwa Hispania katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Dunia kilihitimisha safari ya ‘kizazi cha dhahabu’ cha timu ya soka ya Taifa ya Ubelgiji kwenye michuano hiyo. Thibaut Courtois, Romelu Lukaku, Kevin de Bruyne na Axel Witsel ndiyo wachezaji pekee waliokuwa wamebaki kw…

Na mwandishi wetu, Gazetini MABINGWA wa Tanzania Bara, Yanga SC, wamekamilisha usajili wa winga wa kimataifa kutoka Zambia, Albert Kangwanda, kwa mkataba wa miaka miwili ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya msimu mpya wa mashindano. Kangwanda (27) ambaye amesaini mkataba usiku wa saa tano, Julai 24, 2026 mbele ya Rais wa …

Rais wa Simba SC, Mohammed Dewji, amewataka wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kutogawanyika, akisisitiza kuwa Simba ni kubwa kuliko changamoto yoyote inayokabili klabu hiyo na kwamba mabadiliko yaliyopitishwa na wanachama yanapaswa kukamilishwa. Dewji ameyasema hayo leo wakati wa Tamasha la Simba Day lililofanyika …

Na mwandishi wetu, Gazetini NDANI ya muda wake mfupi ndani ya soka la Tanzania, Steve Barker ‘amesepa na kijiji’, akithibitisha kuwa ni kocha wa daraja la juu kwa namna alivyoibadilisha Simba. Katika nusu msimu aliokaa kwenye benchi tangu alipoajiriwa Desemba 19, 2025, raia huyo wa Afrika Kusini amefanikiwa kwenye mam…

RIO, Brazil KWA mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia Programu yake ya Ukimwi (UNAIDS), watu zaidi ya milioni tatu watakuwa na maambukizi ya ugonjwa huo kufikia mwaka 2030. Katika ripoti yake ya hivi karibuni, watu milioni 1.2 walipata maambukizi mwaka 2025, huku wengine 570, 000 wakipoteza maisha. UNAIDS imee…

MIAMI, Marekani HISTORIA inarudisha kilichotokea miaka 16 iliyopita, ambapo timu ya soka ya taifa ya Hispania ilitwaa ubingwa wa Kombe la Dunia ikiwa kwenye ardhi ya Afrika Kusini. Msimu huu, chini ya kocha De la Fuente, mabingwa hao wa EURO 2024 walianza safari yao kwa suluhu (0-0) dhidi ya timu mpya kwenye historia …

Na mwandishi wetu, Gazetini JULAI 18 ya kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya kumbukizi ya mchango mkubwa alioutoa Nelson Mandela katika ulimwengu wa siasa, hasa kwa mapambano na ushindi wake dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini kwake, Afrika Kusini. Umoja wa Mataifa (UN) uliitangaza Julai 18 kuwa maalumu kwa Mandela, ikizin…

MIAMI, Marekani KWA kipindi cha mwezi mmoja wa michuano ya Kombe la Dunia msimu huu wa 2026, Erling Haaland ameongeza wafuasi milioni 29 katika akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram. Kwamba kwa sasa ana wafuasi zaidi ya milioni 70, akitarajiwa kufikisha milioni 322 kufikia mwishoni mwa mwaka 2026. Wakati huo…

MANCHESTER, Uingereza KLABU ya Manchester United imekamilisha usajili wa kiungo wa kimataifa wa Cameroon, Carlos Baleba baada ya kukubali ada ya Pauni milioni 70. Kwa mujibu wa ripoti, Man United wameitangulizia Brighton kiasi cha Pauni milioni 65 kumnasa nyota huyo mwenye umri wa miaka 22. Man United wameboresha eneo…

LONDON, Uingereza WAKATI huu Real Madrid ikijaribu kumshawishi Vinicius JR kusaini mkataba mpya, Arsenal wanaangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil. Huu ni mwaka wa mwisho katika mkataba wa Vinicius Jr, hivyo endapo Madrid hawatomuongeza au kumuuza kipindi hiki, ataondoka bure (akiwa m…

LOS ANGELES, Marekani TAARIFA ya Serena Williams kutaka kurejea katika tenesi imeshangaza wapenzi wa tenesi duniani kutokana na umri mkubwa wa staa huyo. Licha ya umri wake wa miaka 44, Serena ameweka wazi kuwa anataka kurudi katika mechi za ushindani kwa kushiriki michuano ya Queen’s Club itakayoanza Juni 8, 2026 mji…

LONDON, Uingereza MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Christos Tzolis, amekabidhiwa jezi namba 17 kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya England (EPL) na michuano mingine. Arsenal imetangaza usajili wa mchezaji huyo baada ya kukamilisha dili la kumng’oa katika kikosi cha Club Brugge ya Ubelgiji. Tzolis mwenye umri wa miaka …

MANCHESTER, Uingereza USAJILI wake umekamilika baada ya Manchester United kuipa Chelsea kitita cha Pauni milioni 48. Ni kiungo wa Kibrazil, Andrey Santos. Man United imeachana na usajili wa Pauni milioni 35 wa ‘mido’ wa Atalanta ya Serie A baada ya vipimo kuonesha ana changamoto ya majeraha. Santos (23), ametua Old Tr…

LONDON, Uingereza SHIRIKISHO la Soka la Italia (FIGC) limeanza mazungumzo na kocha aliyeondoka Manchester City, Pep Guardiola, likijaribu kumshawishi kuchukua nafasi ya Gennaro Gattuso aliyeondoka kwenye benchi la ufundi la timu ya taifa. Gattuso aliachia ngazi Aprili, 2026, baada ya Italia kufungwa na Bosnia katika m…

BUENOS AIRES, Argentina HIVI unafahamu kuwa marais wa Argentina wamekuwa makini kuhudhuria viwanjani na wengine hubaki nyumbani pindi timu yao ya soka ya Taifa inapocheza mechi muhimu? Ndiyo, kwa utamaduni wa muda mrefu nchini humo, rais anaweza kuipa ‘gundu’ timu ya taifa endapo atakuwa jukwaani. Hii ilianzia wakati …

LONDON, Uingereza MIONGONI mwa nyota wapya waliotua Chelsea majira haya ya kiangazi ni Geovany Quenda, ambaye amekiri kuwa ni shabiki mkubwa wa Cristiano Ronaldo. Quenda alizaliwa barani Afrika katika nchi ya Guinea-Bissau lakini familia yake ilihamia Ureno akiwa na umri wa miaka saba. Ametua Stamford Bridge akitokea …

MILAN, Italia ROBERTO Mancini ameajiriwa na kuikuta timu ya soka ya Taifa ya Italia ikiwa kwenye hali mbaya. Haijafuzu Kombe la Dunia kwa misimu yote mitatu ya hivi karibuni (2018, 2022 na 2026). Mbali na Mancini mwenye umri wa miaka 61, pia Shirikisho la Soka la Italia (FIGC) limemtangaza kocha aliyewahi kuipa Leices…

Na mwandishi wetu, Gazetini SIKU chache tu baada ya taarifa za Diamond Platnumz kuachana na Zuchu, imeibuka video ya bosi huyo wa Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) na kuzua taharuki. Iko hivi; Zuchu ndiye aliyekuwa wa kwanza kutangaza mitandaoni kuwa ameachana na Diamond baada ya kipindi kisichozidi cha mwaka mmoja wa…

MUNICH, Ujerumani BAYERN Munich itakuwa nyumbani kuikaribisha VfB Stuttgart katika mechi ya ufunguzi wa Bundesliga msimu mpya wa 2026-27. Hiyo itakuwa Ijumaa ya Agosti 28, 2026. Je, nani kumfunika Harry Kane, ambaye msimu uliopita aliibeba kiatu cha ufungaji bora akiwa ameingia kambani mara 36? Bayern chini ya kocha V…

LONDON, Uingereza BAADA ya kunusurika kushuka daraja msimu wa 2025-26 wa Ligi Kuu ya England uliomalizika hivi karibuni, Tottenham imeanza maandalizi ya kuja kivingine. Chini ya kocha aliyeajiriwa dakika za mwisho na kuiokoa isishuke daraja, Roberto Derbi, Tottenham iko bize kwenye soko la usajili majira haya ya kiang…

MERSEYSIDE, Uingereza NYOTA huyo wa eneo la ulinzi ameondoka Barcelona na kujiunga na Liverpool majira haya ya kiangazi. Alikuwa nahodha wakati Wacatalunya hao wakitwaa ubingwa wa La Liga msimu uliopita (2025-26). Kwa mujibu wa mkataba wake wa mkopo, Liverpool itaweza kumsajili moja kwa moja mwishoni mwa msimu wa 2026…

MANCHESTER, Uingereza BAADA ya filimbi ya mwisho katika mchezo wao wa Ngao ya Jamii dhidi ya Arsenal jana Agosti 16, 2026, kocha Enzo Maresca alisema bado mapema, hivyo mashabiki wa Manchester City hawapaswi kuwa na wasiwasi. Walifungwa mabao 3-0. Ni kweli ilikuwa mechi ya kwanza ya ushindani kwa Maresca akiwa kocha w…

NEW DELHI, India MAANDAMANO makubwa ya vijana wa Gen-Z nchini India yamemlazimisha Waziri wa Elimu, Dharmendra Pradhan, kuachia ngazi. Hatua ya vijana, wengi wao wakiwa ni wanafunzi, kuingia barabarani ilikuja baada ya Wizara ya Elimu kufuta mitihani kwa kigezo cha maswali kuvuja. Katika ujumbe wao kwa Serikali, vijan…

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Lebanon, Joseph Aoun, alikutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake nchini Marekani, Donald Trump, mapema wiki hii. Ziara ya Rais Aoun ilikuja wakati huu Lebanon ikiishinikiza Israel kuondosha vikosi vyake vya kijeshi Kusini mwa nchi hiyo. Pia, ni ziara ilikuja katikati ya vita kati …

LONDON, Uingereza ARSENAL imeangukia pua katika mbio zake za kuiwania saini ya Vinicius Jr baada ya Mbrazil huyo kusaini mkataba mpya wa miaka sita katika klabu yake ya Real Madrid. Arsenal walishafikia hatua nzuri kwa Vinicius mwenye umri wa miaka 26 lakini winga huyo alibadili uamuzi na kubaki Santiago Bernabeu. Hiv…

NEW YORK, Marekani MAPEMA wiki hii, Katibu Mkuu wa Marekani, Marco Rubio, aliijia juu Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), akiita kuwa ni yenye kuendeshwa kwa misingi ya rushwa na siasa. Rubio alienda mbali zaidi na kutangaza hatua ya Marekani kumuwekea vikwazo Rais wa ICC raia wa Japan, Tomoko Akane, na mwanasheri…

RIYADH, Saudi Arabia BONDIA wa ngumi za uzito wa juu, Anthony Joshua, amempiga kwa KO ya raundi ya pili Kristian Prenga, pambano lililopigwa mjini Jeddah, Saudi Arabia, usiku wa jana Julai 25, 2026. Hayo ni maandalizi ya Joshua kumvaa mpinzani wake mkubwa, Tyson Fury, katika pambano linalotarajiwa kupigwa kabla ya mwa…

LONDON, Uingereza MABINGWA wa Ligi Kuu ya England (EPL) msimu wa 2025-26, Arsenal, wameimarisha safu yao ya kiungo kwa kumsajili Bruno Guimaraes kutoka Newcastle United, usajili uliogharimu Pauni milioni 75. Mbrazil huyo amesaini mkataba wa miaka minne, akiungana na Declan Rice, Mikel Merino, Martin Zubimendi na Marti…

Na mwandishi wetu, Gazetini BAO la kisigino! Ndivyo unavyoweza kuita baada ya Simba kumtambulisha winga wa kimataifa wa Afrika Kusini, Keletso Makgalwa. Nyota huyo aliyecheza Sekhukhune United msimu uliopita, alikuwa kwenye rada za mabingwa wa Ligi Kuu Bara, Yanga, kabla ya Simba kukatiza mbele na kupita naye. Keletso…

Na mwandishi wetu, Gazetini WADAU wa mchezo wa uogeleaji Tanzania wanatarajiwa kunufaika na mafunzo ya kiwango cha kimataifa kupitia programu ya wiki tatu iliyolenga kukuza vipaji vya waogeleaji vijana, kuimarisha uwezo wa makocha wa wazawa, pamoja na kuwaelimisha wazazi kuhusu namna bora ya kuwaunga mkono wanamichezo…

PARIS, Ufaransa MLINDA mlango wa zamani wa timu ya soka ya Taifa ya Ufaransa, Fabien Barthez, ameajiriwa kuwa sehemu ya wasaidizi wa kocha mkuu wa kikosi hicho, Zinedine Zidane. Kwa mujibu wa taarifa, Barthez anakwenda kwenye benchi kumsaidia ‘Zizou’ katika majukumu ya kuwanoa makipa wa timu hiyo. Zidane aliajiriwa wi…

Na Hassan Mwasha KATIKATI ya ushindani wa Kaizer Chiefs, Orlando Pirates, Scottland FC na Pyramids, Yanga imeweza kumnyakua straika aliyeondoka Mamelodi Sundowns, Peter Shalulile. Yanga wameishitua Tanzania kwa usajili wa straika huyo, ikielezwa kuwa wametumia Dola za Marekani 700,000 (zaidi ya Sh bil. 1.8 za Tanzania…

Na mandishi wetu, Gazetini SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema Mkandarasi amekamilisha kwa mafanikio awamu ya kwanza ya kazi za uvutaji wa nyaya katika eneo la Mkambarani, Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni sehemu ya hatua za mwisho za utekelezaji wa Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa Msongo wa Kilovolti 400 kutok…

LOS ANGELES, Marekani MAHAKAMA mjini Nevada, Marekani, imetaka mahojiano ya mtuhumiwa wa mauaji ya rapa Tupac Shakur, Duane Davis ‘Keffe D’ yawasilishwe kama ushahidi wakati kesi hiyo itakaposikilizwa tena. ‘Keffe D’ (63), anashitakiwa kwa kumuua Tupac katika tukio la kummiminia risasi jijini Las Vegas mwaka 1996 na e…

CAIRO, Misri BAADA ya kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia, sasa macho na masikio ya mashabiki ya wapenzi wa soka yataelekezwa katika michuano ya WAFCON 2026. Tofauti na AFCON, WAFCON hushirikisha timu za wanawake kutoka mataifa mbalimbali na msimu huu mashindano hayo yatafanyika nchini Morocco. . Safari hii, timu…

KAMPALA, Uganda NDOTO kubwa aliyonayo Aziz Abdul, ambaye ni mjukuu wa Rais wa zamani wa Uganda, Idi Amin, ni kuiteka dunia kupitia mchezo wa ngumi. Anapigana uzito wa juu. Aziz alikuwa ukingoni jana Julai 29, 2026 mjini Glasgow, Scotland, ambapo alimvaa Damar Thomas wa Uingereza katika pambano la michuano ya Jumuhiya …

MADRID, Hispania Kiungo wa Manchester City, Rodrigo Hernández, amesema kwa sasa anaelekeza akili yake kwenye fainali za Kombe la Dunia, licha ya kuzisikia tetesi za kutakiwa Real Madrid. Mhispania huyo ameeleza kuwa atafanya uamuzi wa hatima yake baada ya kumalizika kwa michuano hiyo ya Shirikisho la Soka la Kimataifa…

MANCHESTER, Uingereza KOCHA wa Manchester City, Enzo Maresca, yuko mbioni kutangaza nahodha mpya wa kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa 2026-27. Man City inahitaji nahodha wa kuvaa kitambaa cha Bernardo Silva ambaye ameondoka klabuni hapo majira haya ya kiangazi na kutua Real Madrid. Wakati huo huo, Man City wanaw…

Na mwandishi wetu, Gazetini MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Emmanuel Nchimbi, amewataka Watanzania kuendelea kudai kupatikana kwa Katiba mpya yenye maridhiano ya kitaifa, akisema ndiyo msingi wa kuimarisha haki za binadamu, utawala bora na demokrasia nchini. Akizungumza wakati wa kufungua Mkutan…

NYON, Uswis MAMBO hayuko vizuri kwa Rais Gianni Infantino. Ameachana na mpango wake wa kuuza hisa za michuano ya FIFA, ikiwamo Kombe la Dunia, baada ya kukosolewa vikali. Kwa mtazamo wa wachambuzi wengi wa mchezo wa soka, ni mpango uliomchafua na hata kuiweka pabaya nafasi yake ya kushinda Uchaguzi ujao wa Machi, 2027…

Na mwandishi wetu, Gazetini MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, ameibuka mshindi tena dhidi ya Jamhuri katika hatua nyingine ya kesi ya uhaini inayomkabili, baada ya Mahakama ya Rufani kutupilia mbali maombi ya upande wa mashtaka yaliyolenga kuruhusiwa kuwasilisha ushahidi wa nyonge…

Na Faraja Mulungu, Gazetini WAZIRI MKUU wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba, ametoa siku 14 kwa wizara na taasisi zote zinazohusika na Kituo cha Kitaifa cha Pamoja cha Oparesheni kupeleka wawakilishi wake ili kituo hicho kianze kufanya kazi mara moja, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kuimarisha …

Na mwandishi wetu, Gazetini SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imekamata dhahabu yenye uzito wa gramu 4,402.20 na thamani ya zaidi ya Sh bilioni 1.2 katika eneo la Kiluvya, Mkoa wa Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya operesheni zinazoendelea za kudhibiti utoroshaji wa madini na kulinda mapato ya taifa. Akizungumza na waa…

Na Malima Lubasha, Gazetini MKUU wa Wilaya ya Serengeti mkoani Mara, Angelina Lubela, amezindua Jukwaa la Vijana (Youth Platform) ikiwa ni hatua ya kuimarisha ushiriki wa vijana katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Lubela alitoa wito huo wakati akizindua jukwaa hilo jana katika Ukumbi wa Chuo cha Ukunga na Uuguzi …

LONDON, Uingereza LEJENDARI wa timu ya soka ya Taifa ya Argentina, Angel Di Maria, amemtaka Lionel Messi kuachana na wazo la kutundika daluga. Di Maria amekuja na ushauri huo zikiwa ni siku chache tu zimepita tangu Messi na Argentina walipopoteza Kombe la Dunia kwa kufungwa na Hispania katika mechi ya fainali. Tangu k…

2–3 September 2026 | Mwalimu J.K. Nyerere Trade Fair Grounds, Dar es Salaam, Tanzania Africa’s agriculture, livestock, and food processing sectors are entering a new era of growth and this September, the industry’s biggest players will gather under one roof in Dar es Salaam. The 10th Africa Agri Expo (AAE 2026), held …

CAIRO, Misri RAIS wa Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF), Patrice Motsepe, amesema hakuna namna ya kumng’oa Gianni Infantino ndani ya FIFA zaidi ya kusubiri Uchaguzi. Motsepe amekuja na kauli hiyo wakati huu Rais huyo wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) akikabiliwa na shinikizo la kujiuzulu baada ya jaribio l…

LONDON, Uingereza ZIPO taarifa zinazodai kuwa Victor Osimhen wa Galatasaray ni miongoni mwa mastraika walio kwenye orodha ya kocha wa Arsenal, Mikel Arteta. Gazeti la UK Telegraph limeripoti kuwa Arsenal kwa sasa wanamtazama zaidi Osimhen kuliko mshambuliaji wa kati wa Atletico Madrid, Julian Alvarez. Taarifa zaidi zi…

Na Mwandishi Wetu, Shinyanga JUHUDI za Serikali za kupambana na ndoa za utotoni zimezaa matunda mkoani Shinyanga baada ya operesheni maalumu kumuokoa binti aliyekuwa amefaulu kujiunga na Kidato cha Tano, lakini akawa ameozeshwa kabla ya kuanza masomo. Operesheni hiyo ilifanyika usiku wa kuamkia Julai 29, 2026 katika K…

ISTANBUL, Uturuki MSHAMBULIAJI wa zamani wa Liverpool, Mohamed Salah, amefunga mabao mawili katika mechi yake ya kwanza aliyoingia ‘first eleven’ akiwa na timu yake mpya ya Trabzonspor ya Uturuki. Salah alipachika mabao hayo akiiwezesha Trabzonspor kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Istanbul Basaksehir. Mchezo huo ni wa L…

Na mwandishi wetu, Gazetini RAIS wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan amesema Afrika inapaswa kuwekeza zaidi katika elimu, ujuzi wa ufundi na uwezo wa kidijitali ili kuwawezesha vijana kuwa wabunifu, wavumbuzi na wazalishaji wa suluhisho, badala ya kubaki watumiaji wa teknolojia zinazobuniwa na wengine. Akizindua Mkuta…

Na mwandishi wetu, Gazetini WAKALA wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) unasimamia Mfumo wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja, ambao umeisaidia Serikali kuhakikisha bidhaa za mafuta ya petroli, zinapatikana nchini kwa uhakika, kwa wakati na kwa gharama shindani. Mwanasheria wa PBPA, Khadija Zuberi, amesema hayo wakati akitoa…

Na mwandishi wetu, Gazetini MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeendesha mafunzo maalum kwa waandishi wa habari kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza uelewa wa umma na wanachama kuhusu huduma, haki na wajibu unaotolewa na Mfuko huo. Mafunzo hayo ya siku mbili…

Na mwandishi wetu, Gazetini KAMATI ya Kitaifa ya Kuratibu na Kusimamia Fedha za Mfuko wa Dunia nchini Tanzania (TNCM) imeidhinisha rasmi ombi la Tanzania la ufadhili wa Mzunguko wa Nane wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Grant Cycle 8 – GC8) lenye thamani ya dola za Marekani milioni 538.6 (takribani Sh trilioni 1.5), kwa …

Na Hassan Mwasha MSIMU mpya wa Ligi Kuu Bara utaanzia Agosti 14, 2026. Ni msimu wa 2026-27, ambao utakuja na sura mpya kabisa katika historia ya soka la Tanzania. Kwa mara ya kwanza, michuano hiyo ya ndani itashuhudia matumizi ya teknolojia ya kumsaidia mwamuzi kwa marudio ya video (VAR) ikitumika. Je, maboresho hayo …

Na mwandishi wetu, Gazetini VICHOCHEO vya maendeleo ni nyenzo muhimu katika kuongeza kasi ya kufikia malengo ya Dira 2050. Kwa kutambua hilo, Dira hii imebainisha vichocheo vitano vya maendeleo, ambavyo ni usafirishaji fungamanishi, nishati, sayansi na teknolojia, utafiti na maendeleo mageuzi ya kidigitali. Je, nini m…

Na Faraja Mulungu Gazetini RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP) si “white elephant”, bali ni mradi wa kimkakati wenye manufaa makubwa kwa Taifa, ikiwemo kuongeza upatikanaji wa umeme, kuchochea uwekezaji na kukuza shughuli za kiuchumi.…

Na Mwandishi Wetu, Gazetini SERIKALI ya Tanzania na Benki ya Dunia zimefanya kikao cha pamoja cha kuhitimisha maandalizi ya kitaalamu ya Programu ya Uendelezaji wa Ushoroba wa Kati wa Maendeleo ya Kiuchumi Utakaoongeza Ajira kwa Vijana (KAZI MPA), inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za ajira nchini…

na mwandishi wetu, Gazetini NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamad Chande, amefurahishwa na uelewa mkubwa ulioonyeshwa na wanafunzi waliopata elimu ya vipimo katika banda la Wakala wa Vipimo – (WMA), kwenye Maonesho ya 33 ya Wakulima Nane Nane. Akizungumza leo Agosti 6, 2026 baada ya kuzungumza na wanafunzi hao al…

WASHINGTON DC, Marekani RAIS wa Marekani, Donald Trump, amesema wanatarajia kukaa mezani na viongozi wa Iran kujadili mustakabali wa vita vyao vilivyoanza Febrauri 28, 2026. Kwa mujibu wa Rais Trump, mazungumzo ya pande mbili hizo yanatarajiwa kufanyika leo Agosti 3, 2026, akidai kuwa ndiyo sababu ya Marekani kusitish…

GILGIL, Kenya MOTO ambao chanzo chake hakijafahamika umeripotiwa kusababisha vifo vya watu 16, wengi wao wakiwa ni wanafunzi, katika shule ya bweni ya Sekondari ya Wasichana ya Utumishi mjini Gilgil. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AFP, mbali ya 16 waliopoteza maisha, wengine 73 wamejeruhiwa na wamelazwa hospitali …

Na mwandishi wetu, Gazetini Tanzania imepata nyongeza ya nguvu katika jitihada za kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi baada ya TaTEDO – Sustainable Energy Services Organization (TaTEDO-SESO) na Ubalozi wa Norway nchini Tanzania kusaini mkataba wa ruzuku wenye thamani ya hadi Krona za Norway (NOK) milioni 30, sawa …

RABAT, Morocco MSHAMBULIAJI wa kati wa timu ya soka ya Taifa ya Wanawake ya Zambia, Barbra Banda, ndiye anayeongoza msimamo wa wafungaji bora msimu huu wa fainali za WAFCON (AFCON ya Wanawake). Michuano hiyo ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), imefikia nusu fainali, hatua ambayo itaanza kuchezwa keshokutwa (Jumatano).…

LOS ANGELES, Marekani MAREKANI imeiondoa Syria katika orodha ya nchi inazoamini zinafadhili vitendo vya kigaidi (SSOT). Hatua hiyo ni mwendelezo wa uhusiano mzuri wa mataifa hayo tangu kuanguka kwa utawala wa Rais Bashar al-Assad nchini humo. Kama itakumbukwa, Al-Assad aliondoshwa madarakani Desemba, 2024, baada ya mi…

Na mwandishi wetu, Gazetini MJADALA wa kiwango cha mashambuliaji wa kimataifa wa Angola, Depu, tangu asajiliwe na Yanga umeshika kasi mitandaoni na hata vijiweni, wengi wakijiuliza; ni usajili uliolipa au uliofeli? Nyota huyo alijiunga na Yanga wakati wa dirisha dogo Januari, 2026, wakati huo ikionekana kwamba Prince …

LISBON, Ureno BAADA ya miaka 10 ya uchumba, hatimaye staa wa soka, Cristiano Ronaldo amefunga ndoa na mpenzi wake, Georgina Rodriguez. Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Ronaldo ndiye aliyeposti picha ya harusi yao iliyofungwa nchini Ureno. Katika picha hiyo, ameposti mkono wake ukiwa juu ya wa b…

Na mwandishi wetu, Gazetini WAKATI maumivu ya kupokonywa Selemani Mwalimu yakiwa hayajapoa, Yanga imeipiga tena Simba kwenye mshono kwa kuifunga bao 1-0 na kutwaa taji la Ngao ya Jamii katika ‘derby’ iliyochezwa katika Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Katika mechi hiyo ya leo Agosti 12, 2026, Yanga ilipata bao h…

Na mwandishi wetu, Gazetini KOCHA wa Azam FC, Florent Ibenge, amegoma kuanika mbinu za kiufundi atakazozitumia katika mchezo wao dhidi ya Yanga. Timu hizo zitakutana kesho Juni 21, 2026 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, ukiwa ni mchezo wa nusu fainali ya Kombe la FA. Akizungumza na waandishi wa habari kuelek…

RABAT, Morocco MSIMU huu wa fainali za Mataifa ya Afrika kwa soka la Wanawake utafikia ukomo Jumapili hii, yaani Agosti 16, 2026. Michuano hiyo inafanyika Morocco. Safari hii, ni timu ya soka ya Taifa ya Wanawake ya Cameroon dhidi ya wenzao wa Malawi. Timu zote zinasaka taji hilo kwa mara ya kwanza. Cameroon walitinga…

LOS ANGELES, Marekani MAGARI zaidi ya 650,000 yaliibiwa nchini Marekani mwaka 2025, licha ya kwamba idadi ya matukio hayo imepungua katika miaka ya hivi karibuni. Wakati huo huo, inaeleza kuwa magari aina ya Hyundai Elantra ndiyo yanayoongoza kwa kuibiwa (21,732 kwa mwaka 2025), yakifuatiwa na Honda Accord (17,797). K…

Na mwandishi wetu, Gazetini MAGEUZI ya Kidijitali ni kichocheo kingine muhimu cha maendeleo katika karne hii ya 21. Kwa maana nyingine, mageuzi ya kidijitali ni fursa nyingine ya kuharakisha maendeleo katika jamii na taifa kwa ujumla. Kwa kutumia teknolojia hizi kwa ufanisi, Tanzania itaongeza ushindani wake, itapanua…

PARIS, Ufaransa PSG imekamilisha usajili wa mshambuliaji kutoka Barcelona, Ferran Torres, na kumkabidhi jezi namba 9 klabuni hapo. Mhispania huyo mwenye umri wa miaka 26, amesaini mkataba wa miaka migano na mabingwa hao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita (2025-26). Ripoti zinaeleza kuwa PSG wamelipa Pauni milion…

Na Mwandishi Wetu, Gazetini Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imeishauri Serikali kuiongezea wataalam Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ili Taasisi hiyo iweze kuimarisha afya, usalama na ustawi wa wafanyakazi nchini. Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hawa Chakoma…

Na mwandishi wetu, Gazetini Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema hakuna taifa linaloweza kubaki nyuma katika dunia ya sasa inayotawaliwa na teknolojia, akili bandia (AI), sayansi ya data, roboti na ubunifu wa kisasa. Akizungumza Juni 4, 2026 katika Chuo Kikuu cha RUDN nchini Urusi, katika mwendelezo wa ziara…

Na mwandishi wetu, Gazetini NI moja ya sekta muhimu yenye fursa kubwa ya kuchangia maendeleo ya nchi. Hii inatokana na utajiri wa rasilimali za madini, zikiwemo dhahabu, almasi, tanzanite, na madini ya kimkakati kama grafiti, lithium, urani, na madini adimu. Madini haya yanazidi kupata umuhimu na thamani kubwa, wakati…

Na mwandishi wetu, Gazetini ANAREJEA! Hatimaye klabu ya Yanga inatarajiwa kumtambulisha kiungo raia wa Burkina Faso, Stephanie Azizi Ki, ifikapo kesho Agosti 15, 2026. Kwa miezi kadhaa sasa, Aziz Ki aliyeondoka Yanga mwaka 2025 na kujiunga na Wydad Casablanca ya Morocco amekuwa akihusishwa na mpango wa kurudi Jangwani…

Na mwandishi wetu, Gazetini SUPASTAA wa muziki wa R&B nchini Marekani, Trey Songz, alikuwa katika Viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es Salaam jana Agosti 14, 2026. Alialikwa katika Tamasha la IMBEJU Sauti Moja na hii inakuwa mara ya kwanza kwa mwanamuziki huyo kutua katika ardhi ya Tanzania. Kwa wasiomfahamu, …

MADRID, Hispania MSIMU mpya wa La Liga (2026-27) utaanza kesho, yaani Jumamosi ya Agosti 15, ambapo Alaves itafungua pazia kwa kuikaribisha Getafe. Gumzo ni kurejea kwa Jose Mourinho katika viunga vya Santiago Bernabeu. Ni kocha aliyewahi kuipa Madrid mataji matatu (La Liga, Copa del Rey na Spanish Super Cup). Mourinh…

Na mwandishi wetu, Gazetini SEKTA ya Madini nchini Tanzania imevutia uwekezaji wenye thamani ya Sh trilioni 9 ndani ya kipindi cha miaka minne, hatua ambayo Serikali inasema imeendelea kuiimarisha Tanzania kama miongoni mwa vivutio muhimu vya uwekezaji wa madini barani Afrika. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesem…

Na mwandishi wetu, Gazetini BAADA ya Yanga kuanza kwa ushindi msimu huu wa Ligi Kuu Bara (2026-27), Simba nayo imejibu mapigo kwa kuitandika Kagera Sugar mabao 2-0. Simba ikiwa ugenini katika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba leo Agosti 16, 2026, imepata ushindi huo kwa mabao ya beki Olivier Toure (Dk. 45) na mshambuliaj…

CARDIFF, Wales WASHIKA Bunduki wa London, Arsenal, wametwaa ubingwa wa Ngao ya Jamii baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Manchester City. Mechi hiyo ya leo Agosti 16, 2026 ilichezwa katika Uwanja wa Millenium, Wales, na Arsenal kupata mabao yake kupitia kwa beki Riccardo Calafiori (Sek. 24), Kai Havertz (Dk. 28) na…

Na Hassan Mwasha, Gazetini ZIPO sababu nyingi za kukufanya uchukue hatua sasa ya kuachana kabisa na mkaa au kuni na kuhamia nishati safi ya kupikia katika matumizi yako ya kila siku hapo nyumbani. Ukiachana na gharama kubwa, uchafuzi wa mazingira na ugumu wa upatikaji wake, matumizi ya mkaa au kuni yamekuwa yakisababi…

Na mwandishi wetu, Gazetini SEKTA hii itachukua nafasi muhimu katika kuendesha maendeleo ya Tanzania, hususan katika maeneo ya biashara, huduma za ukarimu, na huduma zingine za kijamii na kiuchumi. Kuongezeka kwa watu wenye kipato cha kati kutaongeza mahitaji ya biashara na huduma, hivyo kuchochea ajira, kupanua fursa…

Na mwandishi wetu, Gazetini MKUU wa Wilaya ya Temeke, Sixtus Mapunda, amevitaka vyombo vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi katika showroom za magari wilayani humo ili kubaini kama baadhi yake zinatumika kutakatisha fedha zinazotokana na biashara haramu ya dawa za kulevya. Mapunda amesema hatua hiyo ni muhimu katik…

Na Hassan Mwasha SERIKALI za Mitaa hapa nchini zimepitia mabadiliko mbalimbali kwa nyakati tofauti. Mathalan, mwaka 1962, Serikali ilifuta utawala wa kimila na kuanzisha Serikali za Mitaa, Mamlaka za Miji na Halmashauri za Wilaya. Mwaka 1972, mfumo wa Serikali za Mitaa nao ulifutwa na kuanzishwa kwa ugatuzi wa madarak…

Na mwandishi wetu, Gazetini CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimeendelea kuthibitisha nafasi yake kama kitovu cha utafiti, ubunifu na teknolojia nchini baada ya kuwasilisha bunifu mbalimbali zinazolenga kutatua changamoto za jamii katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma. Akizungumza jana, Agosti 7, 2026, b…

MIAMI, Marekani SUPASTAA wa Inter Miami, Lionel Messi, ametozwa faini kwa kosa la kumpiga kofi nyota wa Philadelphia Union, Quinn Sullivan. Mbali na Messi, Ian Fray wa Inter Miami naye ametozwa faini kwa kumkaba koo mchezaji mwingine wa Philadelphia katika mchezo huo wa sare ya mabao 2-2. Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu…

CATALUNYA, Hispania IMEFICHUKA kuwa uongozi wa klabu ya Barcelona unaangalia uwezekano wa kumrejesha kundini mshambuliaji wake tishio, Robert Lewandowski. Lewandowksi aliyeondoka Barcelona majira haya ya kiangazi, kwa sasa amejiunga na klabu ya Chicago Fire. Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa Italia, Fabrizio Romano…

Na mwandishi wetu, Gazetini HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewataja Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais Mstaafu, Dk. Phillip Mpango, na Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, katika kesi yake ya uhaini. Lissu amewataja kama sehemu ya mashahidi wake baada ya ku…

Na mwandishi wetu, Gazetini MABINGWA watetezi msimu huu wa Ligi Kuu Bara, Yanga, wameshinda mechi yao ya pili kwa kuifunga Coastal Union mabao 4-1. Matokeo hayo ni baada ya Yanga kuanza Ligi kwa ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo uliochezwa mkoani Lindi siku chache zilizopita. Katika mchezo huo wa leo Agosti 20, 2026,…

Na mwandishi wetu, Gazetini NI safari ya miaka takribani saba, ikianza kama ndoto iliyobeba maono makubwa ya kuimarisha hali ya upatikaji wa huduma ya uhakika ya nishati ya umeme hapa nchini. Safari ya uwekezaji wa Shilingi trilioni 7.452 za Tanzania iliyoanza Juni, 2019, ikisimamiwa na Shirika la Ugavi wa Umeme nchin…

Na mwandishi wetu, Gazetini KATIKA sehemu iliyopita, aliyekuwa Waziri wa Afya katika uongozi wa Idi Amin, Henry Kyemba, alisimulia kupitia Kitabu chake cha ‘State of Blood: The Inside Story of Idi Amin’ cha mwaka 1977, kwamba ukatili wa kiongozi huyo ulitokana na kabila lake la Kkwa. Kyemba akasema kama yalivyo makabi…

MILAN, Italia MKONGWE wa soka la Brazil, Ronaldinho, amejiunga na klabu ya Ravenna inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu nchini Italia. Ronaldinho (46), alistaafu mwaka 2015 lakini jana Agosti 20, 2026, alitangaza kurudi mzigoni baada ya miaka 11 ya kuwa nje ya soka la ushindani. “Nimefurahi kuwa hapa na marafiki. Tuna tim…

MANCHESTER, Uingereza NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, amewajia juu wachezaji wenzake akisema kupoteza hovyo mipira kulisababisha timu hiyo kufungwa mabao 2-0 na Hull City. Timu hizo zimekutana leo Agosti 22, 2026, ukiwa ni mchezo wa kwanza kwa upande zote msimu huu wa Ligi Kuu ya England (EPL). Semi Aja…

Na mwandishi wetu, Gazetini SIMBA imeendeleza wimbi la ushindi katika mechi yake ya tatu msimu huu wa Ligi Kuu Bara baada ya kuifunga Singida Black Stars mabao 2-1. Clatous Chama alikuwa wa kwanza kuifungia Simba bao, kabla ya Singida kusawazisha kupitia kwa kiungo wake raia wa Zambia, Clatous Chama ‘Mwamba wa Lusaka’…

Na mwandishi wetu, Gazetini KATIKA kujipanga kwa ajili ya msimu ujao wa 2026-27, benchi la ufundi la Simba Queens limewapa mkono kwa kwaheri nyota wake watano, wakiwamo wageni wanne. Simba Queens walitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake Tanzania Bara msimu uliopita (2025-26) baada ya kuifunga Mashujaa Queens m…

LONDON, Uingereza KIUNGO wa zamani wa Chelsea, Ruud Gullit, amemtabiria makubwa Marcus Rashford akisema straika huyo atafanya makubwa msimu ujao (2026-27) wa Ligi Kuu ya England (EPL). Rashford amerejea Manchester United baada ya kumaliza mkopo wake katika klabu ya Barcelona majira haya ya kiangazi. Barcelona walitara…

Na mwandishi wetu, Gazetini MKUU wa Wilaya ya Ubungo, Albert Msando, amekipongeza Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET) kwa kuendelea kuandika na kuibua changamoto za uharibifu wa mazingira, akisisitiza umuhimu wa vyombo vya habari katika kulinda rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa n…

Na Hassan Mwasha, Gazetini AGOSTI 19 ya kila mwaka, Tanzania, kama zilivyo nchi zingine duniani, huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Misaada ya Kibinadamu. Kwa kuyataja maafa hayo kwa uchache, ni pamoja na magonjwa ya mlipuko, moto na mafuriko. Katika kuiendea Siku hiyo kwa mwaka huu, juzi Agosti 18, 2026 lililafanyika K…

CHICAGO, Marekani LIVERPOOL chini ya kocha mpya, Andoni Iraola, imetandikwa mabao 4-2 na Leeds United katika mchezo wao wa mwisho wa maandalizi ya msimu ujao wa 2026-27. Mbaya Zaidi kwa Liverpool, waliruhusu mabao manne hayo ndani ya dakika 25 za mchezo hupo uliochezwa jana Agosti 2, 2026, mjini Chicago. Kabla ya kupi…

Na mwandishi wetu, Gazetini USHINDI wa tatu mfululizo. Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa leo Agosti 24, 2026. Yanga ikiwa nyumbani katika Uwanja wa KMC, imefikisha pointi tisa baada ya kushinda mechi mbili za awali msimu huu wa Ligi Kuu Bara. Katika mchezo wa leo uliochezwa …

MILAN, Italia KUMEKUCHA! Mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa msimu wa 2026-27 itachezwa Agosti 17, 2026, ambapo Udinese itavaana na Como. Inter Milan ya kocha Christian Chivu inaingia msimu mpya ikiwa bingwa mtetezi baada ya taji la Serie A ililobeba kwa tofauti ya pointi 17. Napoli, AC Milan, Atalanta…

LUSAKA, Zambia KIONGOZI wa siasa za upinzani nchini Zambia kupitia Chama cha National Reconciliation Party for Unity, Brian Mundubile, ameyapinga matokeo yaliyomrejesha madarakani Rais Hakainde Hichilema. Katika matokeo yaliyotangazwa na Tume, Mundubile ameshika nafasi ya pili kwa asilimia 38 ya kura, akiachwa mbali n…

Na mwandishi wetu, Gazetini MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, ametangaza kustaafu siasa na utumishi wa umma, akieleza kuwa atajiuzulu nafasi hiyo kuanzia Septemba 4, 2026. Nchimbi amesema leo, Agosti 25, 2026, amemuandikia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.…

Na mwandishi wetu, Gazetini KATIKA sehemu ya tisa, tuliishia pale bi. Madina alipomuomba Yoweri Museveni amruhusu Idi Amin kurudi Uganda. Rais huyo akasema ‘Idi Amin atalipia dhambi zote alizofanya’, akimaanisha kuwa angefunguliwa mashitaka na kufungwa. Endelea … Baada ya muda mrefu wa kuishi kwenye chumba cha wagonjw…

Na Hassan Mwasha, Gazetini HATUA ya Dk. Emmanuel Nchimbi kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais, na kisha kuvulishwa uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) imemuibua mchambuzi wa siasa na Mhadhiri wa Siasa na Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Richard Mbunda, akisema siasa za sasa zimejaa ‘uchawa’, fit…

Na mwandishi wetu, Gazetini KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Asharose Migiro, amesema Halmashauri Kuu ya CCM imeamua kumfukuza uanachama aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Emmanuel Nchimbi, baada ya kubaini ukiukwaji wa Katiba na kanuni za chama. Akizungumza jijini Dar es Sal…

Na mwandishi wetu, Gazetini TUME ya Madini imetoa muda wa siku 30 kwa wamiliki na wawezeshaji wa miradi ya uchimbaji mdogo yenye Mikataba ya Msaada wa Kiufundi kurekebisha mapungufu yaliyobainika katika ukaguzi wa miradi 128, huku ikionya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya watakaoshindwa kutekeleza matakwa yaliyowekw…

Na mwandishi wetu, Gazetini HATIMAYE kiatu cha Dk. Emmanuel Nchimbi katika nafasi ya Makamu wa Rais kimevaliwa na Deogratius John Ndejembi. Ni uamuzi uliotangazwa jana Agosti 26, 2026 na Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Ndejembi (43), atakuwa Makamu wa Rais wa 13 tangu Tanzania ilipopata uhuru wake kutoka…

MONACO, Ufaransa DROO ya ratiba ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu wa 2026-27 ilichezeshwa jana, Agosti 27, 2026 mjini Monaco, Ufaransa. Ligi hiyo kwa sasa inachezwa kwa mfumo wa Ligi, ikishirikisha timu 36. Manchester United waliomaliza msimu uliopita wa Ligi Kuu ya England wakiwa nafasi ya tatu, wanashiriki kwa mar…

Na Faraja Mulungu, Gazetini DEOGRATIUS John Ndejembi ameanza rasmi majukumu yake mapya ya kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuapishwa katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma. Ndejembi ameapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, George Mcheche Masaju, mbele ya Rais wa Jamhuri y…

LONDON, Uingereza ILIMCHUKUA sekunde 31 pekee straika wa Kibrazil, Joao Pedro, kuifungia bao Chelsea katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Fulham, mchezo wa Ligi Kuu ya England (EPL) uliochezwa Jumatatu ya wiki hii, Agosti 24, 2026. Hata hivyo, swali ni je; ataendeleza moto wake huo akiwa na jezi namba 9, ambayo imekuwa ikio…

LAGOS, Nigeria ANAITWA Iyabo Ojo. Ni mwigizaji maarufu nchini Nigeria na mama mzazi wa bibiye Priscilla, ambaye ni mke wa staa wa Bongo Fleva, Juma Jux. Sasa, bi. Iyabo mwenye umri wa miaka 48, amezua mjadala kwa mashabiki wake huko mitandaoni baada ya kusema mwanamke aliye ‘singo’ anafurahia maisha kuliko aliyeolewa.…

Na mwandishi wetu, Gazetini Mkuu wa Wilaya ya Chato, mkoani Geita, Louis Bura, amesema kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi katika Mkoa wa Geita imepelekea uhitaji wa huduma za usalama na afya mahali pa kazi kuongezeka ambapo ameutaka Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kuhakikisha upatikanaji wa huduma za ukagu…
Habari nyingine
Utakuja AFCON 2027?
Viwanja Kenya · Tanzania · Uganda

Msigwa atoa onyo kutumia vibaya vitambulisho vya NIDA

Usiyoyajua kuhusu mauaji ya halaiki ya Rwanda 1994 (3)

Usiyoyajua kuhusu mauaji ya halaiki ya Rwanda 1994 (2)

Usiyoyajua kuhusu mauaji ya halaiki ya Rwanda 1994 (1)
Na mwandishi wetu, Gazetini SIKU chache zilizopita, Mahakama mjini The Hague, Uholanzi, ilimuhukumu kifungo cha maisha mwanaume aliyetambulika kwa jina la Eugen

EU yapiga marufuku nyama kutoka Brazil

Mahakama: Keffe D ndiye aliyemuua Tupac

Benzema avunjiwa mkataba Saudi Arabia

De Paul: Tunamshukuru, tutamkumbuka Messi

Henry: Sijaona wa kuizuia Arsenal

Trump: Tunakwenda ‘kuipelekea moto’ zaidi Iran

Mosimane kupewa mikoba Bafana Bafana
CAPE TOWN, Afrika Kusini MWANDISHI wa habari maarufu wa Afrika Kusini, Robert Marawa, amefichua kuwa kocha mkongwe, Pitso Mosimane, ndiye atakayeinoa timu ya so

Arteta afika ‘levo’ za Ferguson, Wenger

Kigogo wa jeshi Marekani ajiuzulu

Mawaziri Iran, China wakutana

Maajabu ya kulala wikiendi kwa afya yako

Ngalula, Mahindra wafungua fursa mpya za teknolojia kwa wakulima Tanzania

Malisa akamatwa Namanga, hajulikani alipo-Wakili

Messi aaga timu ya Taifa Argentina baada ya miaka…
BUENOS AIRES, Argentina LIONEL Messi ametangaza rasmi kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Argentina, akisema amefikia wakati wa kuachana na jezi hiyo baada ya s

BoT yawataka wasanii kuwa mabalozi wa elimu ya fedha

Gari la watalii latumbukia mtoni Serengeti, wageni watoka salama
Importance of Peace for National Development
Spika wa Bunge la Tanzania, Mussa Zungu, amesema nchi haiwezi kujengwa kwa maandamano na kwamba amani ni jambo muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Akizungumza leo Juni 1, 2026 jijini Dodoma kuhusu umuhimu wa amani katika jamii, Msita amesema maendeleo yanapatikana katika mazingira yenye utulivu na mshikamano, akisisitiza kuwa sehemu yenye maendeleo ni sehemu inayompendeza Mungu.
Kihongosi amewataka wananchi kuendelea kulinda amani na mshikamano uliopo nchini, akisema Tanzania imeendelea kuwa mfano wa utulivu kutokana na umoja na upendo wa wananchi wake.
Kibadeni ameyasema hayo katika mahojiano maalumu, akisisitiza umuhimu wa vijana kutumia vyema nafasi wanazopewa na kushirikiana katika kulinda amani, akibainisha kuwa ustawi wa taifa lolote unategemea uwepo wa amani.
He called on Christians and the wider community to embrace forgiveness, love and peace as essential pillars for building a united and harmonious society.
Ameeleza kuwa amani ni msingi muhimu wa maendeleo ya Taifa, na kusisitiza kuwa bila amani, jitihada zote za maendeleo haziwezi kufikiwa.
Amani ni zawadi kutoka kwa Mungu na ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa. "Mungu ameturuzuku amani, ni kipaji na kipawa. Tuna kila sababu ya kuitunza na kuilinda, kwani bila amani hakuna maendeleo, wananchi hawatakuwa salama, na tutakimbia nchi yetu wenyewe," amesisitiza.
Amesisitiza kuwa Tanzania ni kivutio cha wivu kwa watu wa mataifa mengine, kutokana na amani na utulivu iliyonayo.
Kuhani Baraka pia amewakumbusha waumini na wananchi wote kudumisha amani wakati wa uchaguzi, akisema amani ni nguzo ya maendeleo na msingi wa haki.
Alisema unaweza kudai vitu vyote kama vile barabara za lami, maji, hospital, katiba mpya, mishara mikubwa lakini kukiwa hakuna amani huwezi kuvitumia vitu vyote hivyo kwa kuwa watu watasambatika huko na kule kwa machafuko ya vita.
Tanzania Fuel Prices Surge Over 30% Due to Middle East Conflict
In April 2026, Tanzanian fuel prices soared over 30 per cent in one month due to the Middle East conflict, despite government assurances of adequate reserves.
The Tanzania Revenue Authority (TRA) has introduced a new billing number system for the loading and offloading of fuel at storage depots, aimed at enhancing transparency, boosting government revenue collection and ensuring compliance without disrupting supply.
Nchi kama Saudi Arabia, UAE, Kuwait, Qatar na Iraq zinapoteza njia yao kuu ya kuuza mafuta.
wanunuaji wa mafuta kwa bei ra rejareja yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam watalazimika kuongeza Sh956 katika kila lita moja ya mafuta baada ya bei kufikia Sh3,820 kutoka Sh2864. Kwa upande wa dizeli, lita moja sasa watanunua kwa Sh3,806 kutoka Sh2,858 ikiwa ni ongezeko la Sh948. Kwa upande wa mafuta ya taa, sasa yatanunuliwa kwa Sh3,684 kutoka Sh2,932 iliyokuwa ikitumika Machi mwaka huu ikiwa ni ongezeko la Sh752.
Ongezeko la bei ya mafuta halipo Tanzania pekee, bali hata katika soko la dunia ambapo bei kikomo kwa Aprili 2026, zimeongezeka kwa asilimia 69.98 kwa mafuta ya petroli, asilimia 114.46 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 120.81 kwa mafuta ya taa.
wanunuaji wa mafuta kwa bei ra rejareja yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam watalazimika kuongeza Sh956 katika kila lita moja ya mafuta baada ya bei kufikia Sh3,820 kutoka Sh2864.
Kwa mujibu wa Ewura, ongezeko hilo la bei za mafuta ni janga la kidunia na Tanzania kama sehemu hiyo inachukua hatua mbalimbali kuhakikisha usalama wa upatikanaji wa mafuta nchini na katika bei himilivu ili kupunguza madhara ya kiuchumi na kijamii.
Kufungwa kwa mlango huu muhimu wa bahari kunasababisha athari kubwa kimataifa, hasa kiuchumi na kiusalama: 1️⃣ Kupanda kwa bei ya mafuta duniani
Kufungwa kwake kunasababisha uhaba wa mafuta sokoni. Bei ya mafuta na gesi inapanda haraka, na kuathiri gharama za usafiri, umeme na bidhaa nyingine.
Kufungwa kunaweza kusababisha mvutano au mapambano kati ya mataifa yenye maslahi ya kiuchumi na kiusalama katika eneo hilo.
Tumeona bei zimeshaanza kupanda, tutakaa ndani ya Serikali kuhakikisha tunakabiliana nalo vipi suala hili ili wananchi waendelee kupata mafuta kwa bei nzuri na kudhibiti kupanda kwa gharama za maisha.
Dk Mwigulu amesema: “Tumeona bei zimeshaanza kupanda, tutakaa ndani ya Serikali kuhakikisha tunakabiliana nalo vipi suala hili ili wananchi waendelee kupata mafuta kwa bei nzuri na kudhibiti kupanda kwa gharama za maisha.”
Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa ghala la kupokea na kuhifadhi mafuta lenye uwezo wa kupokea tani 308,110 katika Bandari ya Dar es Salaam ambao umefikia asilimia 30.
The authority attributed the rise to the ongoing geopolitical tensions in the Middle East, particularly involving the United States, Israel and Iran, which began on February 28, 2026, and have significantly disrupted global oil supply.
Wakati huohuo, athari za vita hivyo zimeanza kuhisiwa na wananchi wa Marekani, ambapo bei ya mafuta imeendelea kupanda na kufikia zaidi ya dola 4 kwa galoni, kiwango cha juu zaidi tangu mwaka 2022.
Hali hiyo inachangiwa na usumbufu katika eneo la Strait of Hormuz, ambalo ni njia muhimu inayopitisha takriban robo ya mafuta yanayotumika duniani.
TANZANIA INA MAFUTA YA KUTOSHA,LICHA YA BEI KUPANDA KUTOKANA NA VITA YA MASHARIKI YA KATI
Kwa mwezi Aprili 2026, gharama za kuagiza mafuta (premiums) katika Bandari ya Dar es Salaam zimeongezeka kwa wastani wa asilimia 15.3 kwa mafuta ya petroli na asilimia 10.8 kwa mafuta ya dizeli na hakuna mabadiliko ya gharama kwa mafuta ya taa.
Mabadiliko ya bei za mafuta nchini kwa mwezi Aprili 2026 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na vita inayoendelea Mashariki ya kati tarehe 28 Februari 2026.
In his final political move, Bungara announced his resignation from ACT Wazalendo on February 18, 2026. He formally joined CHADEMA, the nation’s largest opposition party, aligning himself with their boycott of elections they deemed fundamentally unfair.
The Court of Appeal here began hearing a critical revision application from the main opposition party, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) on Tuesday, which seeks to overturn a High Court injunction that has barred it from conducting any political activities since June 2025.
Hatima ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuendelea kuzuiwa kufanya shughuli za kisiasa au kurejea ulingoni sasa ipo mikononi mwa Mahakama ya Rufaa, baada ya zaidi ya siku 283 tangu kilipowekewa zuio hilo.
Most remarkably, just one week before his death, Bungara launched an operation to strengthen CHADEMA in the southern regions.
Most remarkably, just one week before his death, Bungara launched an operation to strengthen CHADEMA in the southern regions. He donated his personal vehicle and fuel to party organisers and handed over resources to young CHADEMA activists, resulting in thousands of people switching from other parties to join CHADEMA within that single week.
Mgawanyiko huo umejidhihirisha kupitia makundi mawili yenye mitazamo tofauti kuhusu mustakabali wa chama.
Sifuna alisisitiza kuwa yuko tayari kusimama imara kulinda misingi ya chama, akipinga kile alichodai ni juhudi za kukisogeza karibu na mamlaka ya serikali.
Gachagua ameanza kujijenga kama sauti mbadala ya kisiasa, hasa kwa vijana, akishambulia sera za serikali kwa madai ya kushindwa kuboresha maisha ya wananchi wa kawaida.
Kutokuwepo kwake katika mstari wa mbele wa siasa za uchaguzi wa 2027 kumeacha pengo ambalo sasa linajazwa na makundi yenye mitazamo tofauti.
All Parliamentary Standing Committee meetings have been suspended today, March 25, 2026, following the death of Isimani MP and Minister of State in the Prime Minister’s Office, William Lukuvi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema taifa limepoteza kiongozi shupavu, mahiri na mzalendo kufuatia kifo cha William Vangimembe Lukuvi.
William Lukuvi afariki dunia kwa mshituko wa moyo
PRESIDENT Samia Suluhu Hassan has announced the death of the former Minister of State in the Prime Minister’s Office, (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities) William Lukuvi, who passed away this morning, March 25, 2026.
Mbunge wa Isiman, William Lukuvi amefariki dunia, huku aliyekuwa mshindani wake katika mchakato wa ndani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa ubunge wa Isimani, Festo Kiswaga, akifunguka mambo atakayoyakumbuka.
Kiswaga, amesema anamkumbuka kiongozi huyo kwa utendaji wake Isimani, kwani aliingia likiwa jipya na halikuwa na hata shule moja ya sekondari, lakini sasa zimefika zaidi ya 10.
Taarifa ya kifo chake imetolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kisuluka, akimnukuu Rais Samia Suluhu Hassan, aliyesema amesikitishwa na anatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki.
Ambassador Kusiluka conveyed condolences from President Samia Suluhu Hassan, who announced the death and sent her sympathies to the people of Isimani and to the Speaker of the National Assembly.
Kifo hicho kimetangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka juu ya msiba huo wa Lukuvi aliyezaliwa Agosti 15, 1955.
Additionally, the Head of State extended her condolences to the Speaker of Parliament, the bereaved family, residents of Isimani Constituency, and all Tanzanians mourning the loss.
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani William Vangimembe Lukuvi amefariki duinia akiwa na umri wa miaka 70.
Lema ametumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kuzungumzia kifo cha Lukuvi akisema: “Tunazaliwa bila kitu, na tunaondoka bila kitu, kifo hutukumbusha unyenyekevu wa maisha.
According to a statement issued by the Parliament’s Communications and Public Relations Unit, Mr Zungu invoked Rule 176 of the Standing Orders of the National Assembly (August 2025 edition) to suspend the sittings.
Reports of the death of the Isimani Constituency MP in Iringa Region, who had served in Parliament since 1995, began circulating earlier in the day before being confirmed by the Chief Secretary, Ambassador Dr Moses Kusiluka.
Mr Lukuvi’s death brings to three the number of MPs who have died during the 13th Parliament since its inauguration by President Hassan.
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mussa Azzan Zungu leo Machi 25, 2026, ameongoza kikao cha dharura cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uongozi kilichofanyika katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma, kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Ismani, William Vangimembe Lukuvi.
Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba, ametoa salamu za pole kufuatia kifo cha William Vangimembe Lukuvi kilichotokea leo Machi 25, 2026.
Rais Mwinyi amesema taifa limepoteza kiongozi muhimu ambaye amelitumikia kwa uadilifu na kujitolea katika nafasi mbalimbali za uongozi kwa muda mrefu.
WAZIRI LUKUVI AFARIKI DUNIA
William Vangimembe Lukuvi ambaye amefariki leo Machi 25, 2026 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania aliyetoa mchango mkubwa katika siasa za kitaifa.
William Vangimembe Lukuvi ambaye amefariki leo Machi 25, 2026 wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, ni mmoja wa wanasiasa mashuhuri wa Tanzania aliyetoa mchango mkubwa katika siasa za kitaifa. Ametumikia nafasi mbalimbali za uongozi serikalini na kujijengea sifa ya uongozi thabiti kupitia utumishi wa muda mrefu serikalini na uwakilishi wake bungeni.
Mpina ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi akizungumza na Mwananchi amesimulia sababu iliyotaka kumfanya kuikataa bajeti hiyo, kwamba Mpango wa Maendeleo ulikuwa unaeleza Serikali itatenga asilimia 35 ya bajeti kutelekezwa kwenye maendeleo lakini yenyewe ikatenga asilimia 22.
Mdee amesema Lukuvi alikuwa akichukua ushauri na mapendekezo ya hotuba za kambi ya upinzani bungeni na kwenda kuvifanyia kazi kwa vitendo.
William Lukuvi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) akiagwa bungeni Dodoma.
Speaker of the National Assembly, Mussa Zungu, has described the death of Minister of State in the Prime Minister’s Office (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities) and Isimani MP William Lukuvi as a major blow not only to his family, but also to the Parliament, government, and Tanzanians at large.
PRIME Minister Mwigulu Nchemba has paid glowing tribute to the late William Lukuvi, saying he has long benefited from the veteran politician’s wisdom, guidance and selfless dedication to public service, especially since his first appointment as Deputy Minister for Finance.
President Samia Suluhu Hassan is expected to join thousands of mourners in Iringa next Tuesday to honour the late Minister of State in the Prime Minister’s Office (Policy, Parliament, Coordination and Persons with Disabilities), who passed away on Wednesday at Benjamin Mkapa Hospital in Dodoma Region.
DODOMA: PRIME Minister Mwigulu Nchemba has paid glowing tribute to the late William Lukuvi, saying he has long benefited from the veteran politician’s wisdom, guidance and selfless dedication to public service, especially since his first appointment as Deputy Minister for Finance.